How African Leaders Underdeveloped Africa; Akina Kwame,Nyerere,Mandela,Lumumba wakitutizama wanalia

Sodoku

JF-Expert Member
Feb 3, 2016
1,095
2,429
Nilipomsoma Walter Rodney na Kitabu chake How Europe Underdeveloped Africa kuna mambo nlikubaliana naye na mengine mengi sikukubaliana naye.ulikuwa ni ule ule mwendelezo wa miaka yote ya malalamiko, uonevu n.k nilimwelewa alipenda kutujulisha namna gani ambavyo tulinyonywa na kurudishwa nyuma kiuchumi,utamaduni n.k

Miaka mingi baadaye afrika inatawaliwa na waafrika wenyewe. miaka zaid ya miaka 50 ingawa yeye walter rodney ali publish kitabu chake 1972. Namshukuru aliweza kuandika alichoandika kutusaidia kihistoria. Miaka zaidi ya 40 baadaye Afrika bado ni ile ile yenye wakoloni weusi. Hawa wameonesha kuwa ni wabaya sana pengine zaidi ya hata ya weupe. Miaka 40 baadaye viongozi wa afrika wanahusika katika kuinajisi afrika kuiba pesa na wkend akuficha nje ya afrika, kuuana, kufungana, kuua tembo, kuuza madini, kuuza madawa ya kulevya kuwaumiza waafrika wenyewe.

Miaka 40 baadaye kama lumumba angeweza tizama kinachoendelea katika nchi za Afrika angeumia sana kujilaumu kwa kuifia Afrika isiyotambua mchango wake. Kama angeiona kongo ya sasa. Angetembea tembea mpaka Afrika ya Kati, angeenda huku kusini mwa Afrika,Afrika Mashariki,Afrika Magharibi na maeneo mengine angejikuta ana huzuni ya kifo.

Miaka hii hatuna wazungu wa kuwalaumu. ni waafrika wenyewe wanaotesa waafrika wenzao kwa uroho wa madaraka, ulevi,ushetani n.k waafrika wamekuwa kila baada ya miaka kadhaa wanachagua mungu wa kumtumikia. Marais wa afrika wamekuwa miungu watu wakijitajirisha wao na familia zao. Wakiwatesa wananchi wao kwa njaa kwa kuwapiga na polisi wanaolipwa kodi za wananchi hao.

Nyerere alishaanza kuchoka na maisha haya. Hakuwa mkamilifu lakini alikuwa na maono. Viongozi wa sasa wa afrika wanaongozwa na matumbo yao, wanaongozwa na jazba. Najiuliza akina Kwame Nkurumah wangeangalia afrika ya sasa wangesemaje? Nchi zetu zimeduwaa tunauana na kukomoana. Tumekuwa na siasa chafu za kizandiki,kinafiki ,kifisadi na kishetani.

Miaka hii hatuna wazungu wala waarabu wa kuwalaumu. Hawa walitupeleka utumwani na kututesa n.k miaka hii hatuna akina Chief Mangungo wa Msovero. Ambaye maskini hakujua kusoma wala kuandika.
 
Nakubaliana na wewe kabisa..wafrica tumelogwa na ubinafsi,uchu wa madaraka,ukatili kwa. ndugu zetu kwakutumia jesh hii nikujinufaisha wao wenyew
 
Hujui historia, maendeleo yanahitaji muda Uingereza iliendelea baada ya miaka 400 ya Utumwa wa Triangular 1450-1850.Unapozungumza nchi za Afrika hazijaendelea baada ya miaka 40-50 ya uhuru unakosea!!
 
hao ulowataja hapo juu hawalii lolote wao ndio anko tom walosaidia kuidumaza africa,wazungu mara zote walikuwa akichagua wa kumpa nchi baada ya ukoloni,vigezo vilikuwa awe anapendwa na watu wake na anajua kuongea english na aweze kujibu "yes sir"
viongozi walokuwa na uchungu na ustawi wa africa wote hawakuishi muda mrefu wala hawakupata umaarufu wowote

ukitaka kupima siasa za dunia mara nyingi ipe mtazamo afrika kama shamba la bibi viongozi wanaotakiwa kuongoza africa mara nyingi wanatakiwa kuwa na uwezo wa kuwadhibiti waafrika wenyewe kwa mateso na vitisho, na hii ipo mpaka leo
 
Huyu wa kwetu ndio anatuonyesha chuki za waziwazi hataki wabunge wa ccm wapendane na upinzani....na visasi kibao visivyoisha
 
pia kuna kitabu cha rene dumont kinaitwa false start in africa( afrika inakwenda kombo) ni huruma kwa afrika yetu
 
Hujui historia, maendeleo yanahitaji muda Uingereza iliendelea baada ya miaka 400 ya Utumwa wa Triangular 1450-1850.Unapozungumza nchi za Afrika hazijaendelea baada ya miaka 40-50 ya uhuru unakosea!!

Sungusungu sikubaliani na wewe hata kidogo, Uingereza kuendelea baada ya miaka 400 haiwezi kuwa na sisi Africa tusubiri hadi miaka 345 toka sasa ndipo tuendelee, miaka ile level ya technology ilikuwa duni sana pamoja na mambo mengi ndio maana wakachukua muda mrefu, ila dunia ya leo maendeleo yanaweza yakapatikana ndani ya miaka michache tu. Utasemaje kwa nchi kama South Korea, Malasia ambazo tulikuwa level moja ya maendeleo wakati wa uhuru na leo zipo ulimwengu mwingine kabisa kimaendeleo? wao miaka 50 wameweza sisi hadi tusubiri miaka 400 kwakuwa Uingereza walitumia muda huo kupata maendeleo?

Africa tuna tatizo la ombwe la uongozi na wengi wetu pamoja na wanaotuongoza ni shortsighted . Kwa style hii hata miaka 400 ijayo AFRICA itabaki nyuma tu endapo hatutabadilika kifikra.

Jaribu kufikiria mfano mdogo tu tena wa kijinga.....wa ujenzi wa barabara ya mwendo kasi eneo la Mapipa hadi Fire, kwa mtizamo wangu finyu ningelikuwa mhusika kuanzia mapipa hadi fire pangenyanyuliwa barabara iwe juu ili kupisha maji kupita chini, lakini hilo hawakuliona, barabara ya zege imejengwa na miundombinu mingine ya gharama, jana mvua ya muda mchache tu barabara ikajaa maji, magari hayakuweza kupita kwa muda. Hicho ni kipande kidogo tu tunashindwa kuona mbali, je nchi ingekuwa kama Netherlands ambayo eneo kubwa lipo chini ya usawa wa bahari ingekuwaje mvua zikinyesha? wenzetu wana miundo mbinu iliyojengwa miaka na miaka na mababu zao kwa mawe enzi zao na hadi leo ndio inatumika, yote hiyo kwakuwa waliona mbali. Sisi Africa kazi tunayo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom