House girl kaniandikia barua ya mapenzi

Sumbalawinyo

JF-Expert Member
Sep 22, 2009
1,282
247
Wife yuko mkoani kwa ajili ya kujifungua. Tuliamua aende huko kwa kuwa ni uzazi wake wa kwanza na hapa mjini hatuna ndugu wa kuweza kusaidia mambo ya kumkanda, kumpikia na huduma nyingine kwa mama mzazi.

Akiwa anajiandaa kuondoka, tuliletewa kasichana kadogo ka kazi umri miaka 16.

Kwa kweli sina mazoea nako na muda mwingi niwapo home nautumia kufanya kazi zangu za ofisini.

Leo asubuhi nilimwambia mtoto aniandikie orodha ya vitu tunavyohitaji kwa matumizi ya nyumbani.

Muda huu ndio binti kanipa hiyo orodha ili kesho nikafanye shopping. Nimeipitia list, na nilipogusa ukurasa wa nyuma ndipo nkakutana na hiyo barua ya mapenzi.

Binti kaanza kwa kunisifia, akamaliza kwa kusema yuko tayari kuwa mpenzi wangu, na anasema tufanye iwe siri mke wangu asijue.

Anadai atahakikisha anamheshimu na kumtii mke wangu.

Hapa nilipo nimechanganyikiwa, maana katoto haka ni kadogo sana sijui ujasiri kameuptata wapi.
 
Hii imekaa kama bongo movie hivi lol

but hongera kwa kuzimikiwa na housegirl...

Ushauri wangu kama umeshtushwa kweli basi mpeleke shule huyo mtoto..
miaka 16 anastahili kuwa shule....
rafiki kwa kuongezea hapo kwenye bongo movie, kama siyo yenyewe basi huo ni uzembe wa baba.........
inakuwaje hg akawa na guts za kukuandikia barua ya mapenzi baba mwenye nyumba?
ameanzaje kwanza........
na anakuhakikishia hatamwambia mkeo.......yaani kaona possibility ya kukataliwa ni almost 0
sijui labda aje mzee mzima Dark City anifafanulie hili kwa ile lugha yetu ya watu wa kale.....
na wewe rafiki inabidi ule uzi wetu urudi hapa kwa lugha mbali mbali........ mimi najitolea kutafuta wakalimani wa kila kabila
 
Last edited by a moderator:
Hii imekaa kama bongo movie hivi lol

but hongera kwa kuzimikiwa na housegirl...

Ushauri wangu kama umeshtushwa kweli basi mpeleke shule huyo mtoto..
miaka 16 anastahili kuwa shule....

Kasije kuwa kalikuwa kachangu mitaa ya uwanja wa Fisi na huko kijijini kamesingizia tu, bali ni kenyeji hapa town.

Nakumbuka mwaka juzi nililetewa house girl ambaye alikuwa ni Bar maid maeneo ya Mbagala na sisi hatukujua na alikuwa na heshima kweli zile za kijijini. tuliishi naye kama miezi miwili,hivi tukijua katokea kijijini na kila akienda sokoni ni lazima ajitande ushungi hasa.

Sasa siku moja nikatembelewa rafiki yangu aishie Mbagala na alipomuona tu alishtuka sana, hakutoka sebuleni na kila akiitwa ili kutumwa alikuwa anatoka lakini uso wake ulitawalaiwa na aibu sana. wakati namsindikiza mgeni ndipo akanijuza kuwa yule binti alikuwa ni Bar maid huko Mbagala na alikuwa anakula vichwa mbayaaa....

Nilipomweleza mke wangu alishtuka sana, lakini tukapanga tuishi naye kwa akili na ikifika mwisho wa mwezi tumruhusu aondoke na tulifanya hivyo lakini hatukumwambia sababu zaidi ya kumweleza kuwa hatuhitaji tena msichana wa kazi.
 
rafiki kwa kuongezea hapo kwenye bongo movie, kama siyo yenyewe basi huo ni uzembe wa baba.........
inakuwaje hg akawa na guts za kukuandikia barua ya mapenzi baba mwenye nyumba?
ameanzaje kwanza........
na anakuhakikishia hatamwambia mkeo.......yaani kaona possibility ya kukataliwa ni almost 0
sijui labda aje mzee mzima Dark City anifafanulie hili kwa ile lugha yetu ya watu wa kale.....
na wewe rafiki inabidi ule uzi wetu urudi hapa kwa lugha mbali mbali........ mimi najitolea kutafuta wakalimani wa kila kabila

Kabisaa..
mtu ukiwa unaonesha sura ya kazi sio tu housegirl...hata officemate hakuletei habari hizo...
sasa huyu housegirl keshamsoma na anajua anachokifanya....kazi ipo...
 
siwezi toka kwangu nikajifungulie home, uvivu tu, tena na hg yupo? Akandwe kawa unga wa maandazi?

Umekula bingo, mle hg, ptuuu!
umeona eeehh!
nilipojifungua mtoto wa kwanza tulikuwa mimi na hubby peke yetu, na home tulikuwa na houseboy....
nakumbuka ile usiku ananipeleka hosp kuna jirani alituona akamwambia mkewe (naona hapa ngoma tayari), wakatuwahi, wakaoffer tuende nao hosp.
usiku huo huo nikajifungua, nikarudi home mchana wake.......... hubby na hb wanapika supu na kubadilisha nepi mtoto.... naoga mwenyewe, navaa mwenyewe, naogesha mtoto wangu mwenyewe
siku ya tatu ndo mdogo wangu (wa kike) akaja kunisaidia.
 
Kasije kuwa kalikuwa kachangu mitaa ya uwanja wa Fisi na huko kijijini kamesingizia tu, bali ni kenyeji hapa town.

Nakumbuka mwaka juzi nililetewa house girl ambaye alikuwa ni Bar maid maeneo ya Mbagala na sisi hatukujua na alikuwa na heshima kweli zile za kijijini. tuliishi naye kama miezi miwili,hivi tukijua katokea kijijini na kila akienda sokoni ni lazima ajitande ushungi hasa.

Sasa siku moja nikatembelewa rafiki yangu aishie Mbagala na alipomuona tu alishtuka sana, hakutoka sebuleni na kila akiitwa ili kutumwa alikuwa anatoka lakini uso wake ulitawalaiwa na aibu sana. wakati namsindikiza mgeni ndipo akanijuza kuwa yule binti alikuwa ni Bar maid huko Mbagala na alikuwa anakula vichwa mbayaaa....

Nilipomweleza mke wangu alishtuka sana, lakini tukapanga tuishi naye kwa akili na ikifika mwisho wa mwezi tumruhusu aondoke na tulifanya hivyo lakini hatukumwambia sababu zaidi ya kumweleza kuwa hatuhitaji tena msichana wa kazi.


Ha haa haa alikuwa anakula vichwa sio?

siku hizi unaletewa housegirl ana Blackberry ....huku mkeo ana Nokia tochi...
housegirl asubuhi anakwambia ' maambo uncle'?
huku kavaa ki pedo lol
 
Kabisaa..
mtu ukiwa unaonesha sura ya kazi sio tu housegirl...hata officemate hakuletei habari hizo...
sasa huyu housegirl keshamsoma na anajua anachokifanya....kazi ipo...
umeona eehhh!
yaani sipati picha hg yeyote aje pale home athubutu hata kuvaa sketi fupi akimuwinda baba mwenye nyumba, sembuse kumkonyeza! ataanzia wapi.................
hapo ndugu angalia tu jinsi ya kujirekebisha, maana siwezi kusema fukuza huyo hg, tatizo unalo wewe.
kama mtoto wa 16 years ameweza kukuandikia baria basi ujue una safari ndefu sana, kama hutabadilika imekula kwako.....
na hapo ndo kwaaaza unaanza, maana huyo ni mtoto wa kwanza, lol!
 
Back
Top Bottom