Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mahakama ya Mwanzo , Maromboso jijini Arusha imemkuta na kesi ya kujibu mtuhumiwa wa kesi ya wizi wa sh, milioni 7 inayomkabili Kijana wa kazi (house boy) William Mlewa(22) akituhumiwa kumwibia Mwajiri wake, Anjela Charles ambaye ni Mbunge wa zamani wa bunge la Afrika mashariki (EALA).
Hakimu wa mahakama hiyo, Neema Mchomvu alidai kuwa ushahidi wa upande wa mashtaka umekamilika kwa mashahidi sita kuwasilisha ushahidi wao hivyo mahakama imemkuta mshtakiwa na kesi ya kujibu na kumtaka kujipanga kwa ajili ya utetezi.
Hakimu alimsomea mshtakiwa vipengele vitatu vya utetezi na kumtaka kuchagua kimoja wapo kati ya kujitetea binafsi,Kuwa na mashahidi au kukaa kimya jambo ambalo mtuhumiwa alianza kuangua kilio akiomba ahurumiwe yeye bado ni mdogo na baadaye alichagua kukaa kimya na kuiachia mahakama iendelee.
Ndipo hakimu alipodai kuwa hukumu ya kesi hiyo itatolewa Juni 19 mwaka huu na kumtaka mtuhumiwa na Mlalamikaji kufika bila kukosa.
Awali Shahidi wa Tano ,katika kesi hiyo iliyounguruma mwishoni mwa wiki iliyopita,James Joseph ambaye ni mtunza mazingira kwa mlalamikaji,alidai kwamba alimsikia mtuhumiwa akimwambia Mlalamikaji kwamba yeye ndiye alikuwa akichukua fedha hizo chumbani kwa boss wake baada ya kumvizia akiwa jikoni.
Alieleza mahakama hiyo kwamba siku ya tukio akiwa nyumbani kwa Mlalamikaji alikuja William akitokea nje na kuwauliziamama (Mlalamikaji) alipo na baada ya kumfahamisha kwamba yupo stoo ndipo alipomfuata na kumwambia kwamba amsamehe yeye ndiye ameiba fedha hizo.
Alisema kuwa alimwona Mlalamikaji akitokea kwenye chumbani cha stoo akiwa ameongozana na mtuhumiwa huku Mlalamikaji akimtaka Wiliamu kueleza maneno aliyomwambia.
Ndipo nilipomsikia mtuhumiwa akimwomba msamaha Mlalamikaji akidai kwamba yeye ndiye ameiba fedha hizo na ghafla nilimwona mtuhumiwa akiinama na kutumbukiza kichwa kwenye Sufuria la uji wa Moto na kuunga vibaya.
Hata hivyo mzee mmoja wa baraza alimuuliza Shahidi iwapo alishuhudia Mtuhumiwa akiiba fedha hizo,jambo ambapo shahidi alishindwa kuthibitisha.
Naye shahidi wa sita, Amon Ngairo(32)ambaye ni fundi bomba alieleza kuwa alimsikia Mtuhumiwa akimweleza Mlalamikaji kuwa yeye ndiye amekuwa akiiba fedha hizo kwa kumvizia akiwa ametoka chumbani kwake.
Kesi hiyo imeahitishwa hadi juni 19/mwaka huu siku ambayo mahakama hiyo itatoa hukumu.
Ends....
Hakimu wa mahakama hiyo, Neema Mchomvu alidai kuwa ushahidi wa upande wa mashtaka umekamilika kwa mashahidi sita kuwasilisha ushahidi wao hivyo mahakama imemkuta mshtakiwa na kesi ya kujibu na kumtaka kujipanga kwa ajili ya utetezi.
Hakimu alimsomea mshtakiwa vipengele vitatu vya utetezi na kumtaka kuchagua kimoja wapo kati ya kujitetea binafsi,Kuwa na mashahidi au kukaa kimya jambo ambalo mtuhumiwa alianza kuangua kilio akiomba ahurumiwe yeye bado ni mdogo na baadaye alichagua kukaa kimya na kuiachia mahakama iendelee.
Ndipo hakimu alipodai kuwa hukumu ya kesi hiyo itatolewa Juni 19 mwaka huu na kumtaka mtuhumiwa na Mlalamikaji kufika bila kukosa.
Awali Shahidi wa Tano ,katika kesi hiyo iliyounguruma mwishoni mwa wiki iliyopita,James Joseph ambaye ni mtunza mazingira kwa mlalamikaji,alidai kwamba alimsikia mtuhumiwa akimwambia Mlalamikaji kwamba yeye ndiye alikuwa akichukua fedha hizo chumbani kwa boss wake baada ya kumvizia akiwa jikoni.
Alieleza mahakama hiyo kwamba siku ya tukio akiwa nyumbani kwa Mlalamikaji alikuja William akitokea nje na kuwauliziamama (Mlalamikaji) alipo na baada ya kumfahamisha kwamba yupo stoo ndipo alipomfuata na kumwambia kwamba amsamehe yeye ndiye ameiba fedha hizo.
Alisema kuwa alimwona Mlalamikaji akitokea kwenye chumbani cha stoo akiwa ameongozana na mtuhumiwa huku Mlalamikaji akimtaka Wiliamu kueleza maneno aliyomwambia.
Ndipo nilipomsikia mtuhumiwa akimwomba msamaha Mlalamikaji akidai kwamba yeye ndiye ameiba fedha hizo na ghafla nilimwona mtuhumiwa akiinama na kutumbukiza kichwa kwenye Sufuria la uji wa Moto na kuunga vibaya.
Hata hivyo mzee mmoja wa baraza alimuuliza Shahidi iwapo alishuhudia Mtuhumiwa akiiba fedha hizo,jambo ambapo shahidi alishindwa kuthibitisha.
Naye shahidi wa sita, Amon Ngairo(32)ambaye ni fundi bomba alieleza kuwa alimsikia Mtuhumiwa akimweleza Mlalamikaji kuwa yeye ndiye amekuwa akiiba fedha hizo kwa kumvizia akiwa ametoka chumbani kwake.
Kesi hiyo imeahitishwa hadi juni 19/mwaka huu siku ambayo mahakama hiyo itatoa hukumu.
Ends....