Hotuba za Wafanyakazi zimejaa malalamiko na makasiriko dhidi ya serikali, zimejaa uzuni na maumivu

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Hotuba za wafanyakazi zimejaa malalamiko na makasiriko dhidi ya serikali, zimejaa uzuni na maumivu. Wanasoma hotuba Kama hizi kwa mara ya Kwanza toka mwaka 2016 ndoto zakuandika uhalisia wa Watumishi zilipozimwa rasmi.

Kwa namna zilivyoandaliwa ni Kama wanamategemeo makubwa na Rais mpya bila kujua malalamiko yao yanahitaji zaidi fedha kuliko kitu kingine.

Kwa Hali ilivyo na namna alivyoeleza Mhe. Rais ni wazi kimeumana. Walijiwekea matumaini makubwa ila ukweli ni kwamba uwezo ni mdogo ukizingatia idadi ya wafanyakazi na idadi ya Watanzania wenye mahitaji mbalimbali..

Niwashauri tu kwa wakati mwingine hotuba Kama hizi wawe wanazisoma mwaka mmoja kabla ya mwaka wa uchaguzi, kipindi hicho wanasiasa huwa wepesi kutoa ahadi nakuzitekeleza ila kwa Sasa 2021 kinachofanyika nikuruhusu malipo ya madeni yao, ongezeko la kisheria (annual increment) na malipo ya posho chache zilizokatazwa na awamu iliyopita.

Shime wafanyakazi, msilaumu kwa kiu yenu kutokatika. Hali ya uchumi ni mbaya na Mhe. Rais amesema kweli tupu kulingana na uwezo wa serikali yake kulipwa.

Cha mwisho, wakati ninyi wachini mliolalamika na kubeba mabango mkiongezewa 20,000 to 30,000 mabosi wenu watalipwa ngongeza zaidi ya laki mbili kwa sababu ya ukubwa wa mishahara. Ninyi mmepambana wao wakajificha lakini manufaa yake ni makubwa kwa waliojificha kuliko walioandamana na mabango juu
 
Mishahara Hakuna nyongezaaa woyoooooo...........

Jamani mama alishasema yeye na mwendazake ni kitu kimojaaaaa...... wafanyakazi vumilieni tuuu, kaahidi mwakani mambo yatakuwa poaaaaa.........
 
Hotuba za wafanyakazi zimejaa malalamiko na makasiriko dhidi ya serikali, zimejaa uzuni na maumivu. Wanasoma hotuba Kama hizi kwa mara ya Kwanza toka mwaka 2016 ndoto zakuandika uhalisia wa Watumishi zilipozimwa rasmi.

Kwa namna zilivyoandaliwa ni Kama wanamategemeo makubwa na Rais mpya bila kujua malalamiko yao yanahitaji zaidi fedha kuliko kitu kingine.

Kwa Hali ilivyo na namna alivyoeleza Mhe. Rais ni wazi kimeumana. Walijiwekea matumaini makubwa ila ukweli ni kwamba uwezo ni mdogo ukizingatia idadi ya wafanyakazi na idadi ya Watanzania wenye mahitaji mbalimbali..

Niwashauri tu kwa wakati mwingine hotuba Kama hizi wawe wanazisoma mwaka mmoja kabla ya mwaka wa uchaguzi, kipindi hicho wanasiasa huwa wepesi kutoa ahadi nakuzitekeleza ila kwa Sasa 2021 kinachofanyika nikuruhusu malipo ya madeni yao, ongezeko la kisheria (annual increment) na malipo ya posho chache zilizokatazwa na awamu iliyopita.

Shime wafanyakazi, msilaumu kwa kiu yenu kutokatika. Hali ya uchumi ni mbaya na Mhe. Rais amesema kweli tupu kulingana na uwezo wa serikali yake kulipwa.

Cha mwisho, wakati ninyi wachini mliolalamika na kubeba mabango mkiongezewa 20,000 to 30,000 mabosi wenu watalipwa ngongeza zaidi ya laki mbili kwa sababu ya ukubwa wa mishahara. Ninyi mmepambana wao wakajificha lakini manufaa yake ni makubwa kwa waliojificha kuliko walioandamana na mabango juu

7d5b5f9a-fff6-4f1c-906e-8d6c5911f69a.jpg
 
Ukweli mchunguu pesa hakuna ndio ukweli wenyewe ngoja tujenge Daraja kwanza..!
 
Ila ameongea honest talk, katoa sababu za msingi kwa nini hajaongeza. Ngoja tuvumilie mpaka mwakani!


Kuongeza mshahara sio jambo la kukurupuka
Tuendelee kuchapa kazi kuongeza pato la taifa mwakani nyongeza iwepo

TRA, BRELA, TIC, TBS, Wizara ya viwanda na biashara, Halmashauri na agency nyingine zote za serikali ni muda wenu sasa kuchapa kazi....... punguzeni urasimu, wahudumieni wateja kwa wakati ili wakapambane huko kwenye private sector pato la taifa liongezeke na liwe stable ili watumishi wa umma wapate nyongeza ya mishahara

Kazi iendelee
 
Ukweli mchunguu pesa hakuna ndio ukweli wenuenwe ngoja tujenge Daraja kwanza..!

Mchungu kweli

Tuelewe tuu kwamba Kujenga daraja ni onetime cost ila kuongeza mishahara ni budget ya kila mwezi.

Hapohapo tukubali hawa watumishi wa umma wanaotakiwa kuongezwa mishahara wao wanato huduma zaidi kwa jamii na sio wazalishaji mali useme wameongeza uzalishaji kwa kiasi fulani sasa wanaweza kutumia ile nyongeza kujiongezea mishahara

Ni ngumu rais kupandisha mishahara itakayogharimu ongezeko la budget kwa makisio ya trilion 1.5 au 2 kila mwezi ilhali haioni hiyo pesa itakakotokea


Tuendelee kuchapa kazi na kufikia yale makusanyo yaliyoagizwa mishahara itapanda
 
Back
Top Bottom