Hotuba za Rais Magufuli za kichwani zinakera, asome hotuba anayoandaliwa

Uwezo MKUBWA Wa kuhifadhi rejea takwimu za madaraja, kilometa za barabara na samaki
 
anajifanya OBAMA! anaishia kusahau hata katiba inasema nini juu unachokisema.
Hayo mambo awaachie kina Obama, Nyerere tu maana mengine ayaongeayo yanavunja katiba ya nchi. Sasa mfano issue ya v..... Za Mara wizara ya takwimu, Saddamu alikua wa Kuwait, yana muharibia ka hataki kusoma awe anakaa na washauri wamwambie vtu ili asiende çhaka kuchaganya RAIA.
 
Wapo watu wanamshabikia, lakini naamini hata hao wanaoshabikia (hususani watendaji wa serikali na watumishi wa Chama chake) siyo kwamba wanaona anahoyafanya yuko sawa, bali wanafanya hivyo kwa ajili tu ya kulinda tu vibarua vyao, kwa kuwa watendaji karibu wote wa serikali wameshagundua kuwa huyu jamaa haambiliki na wala hashauliki na badala yake anaongoza serikali yake kwa kutumia ubabe na vitisho.......

Utawala wa huyu jamaa unafanana sana na ile hadithi ya yule Mfalme aliyepita mtaani yuko uchi, lakini hakuna mtu hata mmoja aliyethubutu kumtamkia Mfalme huyo yuko uchi, isipokuwa mtoto mdogo mmoja ambaye alimuuliza mama yake kuwa mbona Mfalme anatembea yuko uchi?

Mama wa huyo mtoto alimwonya vikali sana huyo mtoto kuwa asithubutu kurudia maneno yake kwa kusema kuwa Mfalme yuko uchi.......

Ndicho kinachotokea TZ hivi sasa, kwa kuwa Jeshi la Polisi, Msajili wa vyama na vyombo vingine mbalimbali, ingawa wanajua wazi kuwa Mkulu 'anabugi step' lakini kama ile hadithi ya Mfalme aliyekuwa anatembea uchi, watendaji wengi wakubwa wa serikali hapa nchini hawana tena ujasiri wa kumwambia Mfalme kuwa upo uchi...............


mkuu kwa maelezo haya naungana na wewe asilimia mia moja nakumbuka kauli alizotumia makamba kumuasa juu ya kupokea ushauri akatumia kimemo kumfikishia ujumbe nchi inaelekea kubaya kiongozi anasema nahama asiyehama awe tayar kuacha kazi kuna watu mikataba yao ya ajira inaonesha ajira zao zitakuwa dar es salaam ukimtoa nje ya dar lazima umlipe nna uhakika wakienda mahakaman kama wataangalia sheria wanashinda hana washaur huyu aaandaliwe vya kuzungumza atalitia taifa hasara kubwa sna katanguliza ubabe badala ya busara ambayo ni sifa ya uongoz pia.
 
Napendekeza kwa faida ya nchi yetu,waziri wa mambo ya ndani ya nchi akutane na viongozi wa vyama vya upinzani,ili waweke utaratibu wa namna ya uendeshaji wa siasa
 
Watanzania kweli haitapita miaka mitatu lazima tutajuta! Raisi kote duniani ni Alama na Nembo ya Taifa husika kwa kuwaunganisha wananchi! Ila Hapa kwetu naona mkulu amekuwa nembo ya tungo tata na kutugawa kwa misingi ya sisi tuna madaraka wao hawana!
 
Sasa kila mmoja kama anatakiwa kufanya siasa eneo alilo chaguliwa bac JPM hapashwi kufanya siasa Dar sababu hwakumchagua. Aende tu uko dodoma au Chato.
 
Nafasi ya urais ni Tasisi sio one man show.ukisikiliza hotuba za JPM hazionyeshi kama anasoma alichokiandaa/kuandaliwa.anatililika alivyovikusanya na kuviweka moyoni.kila kukicha anaacha maswali kuliko majibu kutokana na speech zake!
Sijawahi ona Rais wa hivi hapa nchini.labda nchi zingine.Rais anakazi za kuli shape taifa kwa kauli zake.sasa anapotawaliwa na mihemuko na kutoa point kichwani nahisi tutaingia Chaka/potezwa huko mbele.hatujui kipi tukiweke kwenye library kama kumbukumbu yenye mashiko.Time will tell.
Mzee Nyerere yule mzee wetu achana nae. Hotuba zake alizozitoa bila kuandikiwa popote, ukizisikiliza leo TBC kipindi cha Hotuba za Baba wa Taifa, sote tunakubali mzee yule alikua na kipaji na maono makubwa! Hotuba za Mzee Nyerere zilikua full msg, hazina ukakasi, zenye ujumbe USIOCHUJA. Mungu amlaze pema mzee huyu peponi-Ameen
 
Back
Top Bottom