Hotuba ya Zitto Kabwe katika uzinduzi wa jukwaa la viongozi wa vijiji jimboni

Ubumuntu

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
14,314
10,775
Found this on Zitto's blog; and thought I would share with JF members!!

Hii ni kazi nzuri sana kwa wote waliofanikisha uanzishwaji wa jukwaa hilo; kwani ni kweli kumekua na gap kati ya viongozi wa serikali kuu na serikali za mitaa linapokuja suala la kushirikiana katika kuongoza na kuchochea maendeleo ya jamii husika.
Wasiwasi wangu ni kwamba, kwa jinsi viongozi wa ngazi za mitaa walivyozoea posho za vikao, naanza kuona giza mbeleni. I hope Zitto has an answer to this...

Cheers!!


 

Attachments

  • Zitto na Demokrasia.doc
    44.5 KB · Views: 187
Found this on Zitto's blog; and thought I would share with JF members!!

Hii ni kazi nzuri sana kwa wote waliofanikisha uanzishwaji wa jukwaa hilo; kwani ni kweli kumekua na gap kati ya viongozi wa serikali kuu na serikali za mitaa linapokuja suala la kushirikiana katika kuongoza na kuchochea maendeleo ya jamii husika.
Wasiwasi wangu ni kwamba, kwa jinsi viongozi wa ngazi za mitaa walivyozoea posho za vikao, naanza kuona giza mbeleni. I hope Zitto has an answer to this...
Cheers!!

Inatia moyo kuona kuna viongozi wanaothubutu na wanaojitoa kweli kuleta maendeleo ya watu kwaajili ya watu. Nimesoma hotuba yake na nimefurahishwa na approach yake...1: kabla ya kukurupuka alifanya utafiti kwanza na baada ya utafiti ikaja resolution ya kuunda jukwaa. 2:Anatambua kazi ya kutengeneza ajira ni yakisera zaidi kuliko kutupa jukumu hilo kwa raia kama mwenyewe anavyoainisha "...kuhakikisha tunabuni vyanzo vipya vya mapato ili Halmashauri yetu iwe endelevu (innovation stage). Ndio maana ni muhimu kuhakikisha kwamba (i) tunaanzisha eneo la viwanda vidogo vya kusindika mazao ya michikichi pale kijiji cha Mahembe ili kuzuia mise kupelekwa eneo la SIDO katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji na hivyo kutengeneza ajira kwa watu wetu na kuwezesha Halmashauri kupata mapato (ii) ....."

Kutengeneza ajira....Ili kupata mapato na siyo kupata mapato ili kutengeneza ajira....Big up Zito!

Viongozi wengi Tanzania wanaenda in opposite direction kwamba wanataka kupata mapato kabla ya kutengeneza ajira..ndiyo maana kila siku hakuna maendeleo. Huwezi kupata out put bila kuwa na in put..Hapa tunapata hivi Innovation i.e sera sahihi itakayo zalisha ajira kuanzisha eneo la viwanda vidogo ili kusindika michikichi; available resource pale ni michikichi sikwamba technology ya kuzalisha wese haipo no...ambacho hakikuwepo ni sera sahihi ya jinsi ya ku produce mawese badala ya kuwa kazi ya household Zito anaipeleka into firm level kisera kwa kuweka eneo laviwanda vidogo ili aweze kuwa coordinate wasindika michikichi na pia ku-concentrate financial resources kidogo walizonazo ziweze kuwa na significant impact...Lakini ili kufikia hapo ilibidi afanye utafiti kwanza wa jinsi ya kuileta...You see these are existing theories on how to create jobs ambazo kweli ndo zitaongeza kipato cha locals; kwa kutumia micro policies zao za Kigoma na resources zao natural na man made....

Nilitaka kunyambulisha hilo tu kuonyesha how it make a difference kuwa na kiongozi aliyeelimika siyo kwa vyeti bali kwa ujuzi...Big up comrade Zitto Mungu akuinue...Nialike Kigoma nije nikupige tough kidogo!
 
Mkuu naona inabidi uwe na mtaji ili kutengeneza ajira. Capital ni muhimu,900,000$ a month?.... lazima halmasahauri ipate tax kutoka kampuni inayomiliki hiyo meli. At least 1% (9,000$) na kutunisha mfuko wao wa SIDO. Kuna macomrades magamba na ma-comrades magwanda.
Big up comrade Zitto!!...... from comrade magamba!
 
kweli Zitto ameamua kuwatumikia watu wake kama kiongozi na wengine (viongozi) waige mfano wake Big Up ZITTO na cdm
 
Sasa mnakoelekea huko ni kama Korea ya Kaskazini au China ya Marehemu Mao. Mnaabudu watu mpaka mnapitiliza. Ni hiyo fanatical following hii ndiyo inawafanya kuandika hata mambo ambayo siyo news. Yaani Zitto kutoa hotuba jimboni kwake ni issue? Kwani zi ndiyo kazi ya siasa?
 
Zitto ni mfano mzuri wa viongozi tunaowahitaji ili nchi iendelee. Mungu ambariki aendelee kulitumikia taifa letu vizuri
 
Sasa mnakoelekea huko ni kama Korea ya Kaskazini au China ya Marehemu Mao. Mnaabudu watu mpaka mnapitiliza. Ni hiyo fanatical following hii ndiyo inawafanya kuandika hata mambo ambayo siyo news. Yaani Zitto kutoa hotuba jimboni kwake ni issue? Kwani zi ndiyo kazi ya siasa?

Heshima kwako mkuu!! Ni vyema ukaisoma kwanza hotuba hiyo kishak aribu tuichambue. Ukisoma naamini utaelewa maana ya mimi kushare hotuba hii.
Cheers!

 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom