Crimea
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 24,883
- 33,400
Wakuu nmesikiliza hotuba ya Maalim Seif baada ya kuapishwa, nikiri tu kwamba huyu mzee ana busara sana. Seif anajua kwamba Zanzibar ni zaidi ya ACT Wazalendo na CCM,.
Na kwa hotuba hii kama wataenda jinsi walivyo leo nauhakika Zanzibar itapiga hatua sana.
Ningekuwa karibu na JPM ningemshauri awaite Seif na Mwinyi Ikulu ya bara waje wagonge glass kutwa nzima au yeye mwenyewe anaweza kujipeleka Ikulu ya Zanzibar wakagonge glass huko, hakika watu watatiwa moyo na Wabelgiji watanuna sana.
Kingine, kwa kuwa Zitto ameshajirudi ni wakati sasa wa Rais kumpa ubunge na ikiwezekana Wizara kabisa ili tujenge nchi. Haya mengine ya kushirikiana na kina Amsterdam tutawasamehe kina Zitto.
Jioni njema wakuu.
Na kwa hotuba hii kama wataenda jinsi walivyo leo nauhakika Zanzibar itapiga hatua sana.
Ningekuwa karibu na JPM ningemshauri awaite Seif na Mwinyi Ikulu ya bara waje wagonge glass kutwa nzima au yeye mwenyewe anaweza kujipeleka Ikulu ya Zanzibar wakagonge glass huko, hakika watu watatiwa moyo na Wabelgiji watanuna sana.
Kingine, kwa kuwa Zitto ameshajirudi ni wakati sasa wa Rais kumpa ubunge na ikiwezekana Wizara kabisa ili tujenge nchi. Haya mengine ya kushirikiana na kina Amsterdam tutawasamehe kina Zitto.
Jioni njema wakuu.