Hotuba ya Rais, June 2012, live on TBC 1

Kweli ****** hana utawala. Hotuba anayotoa ni ileile tuliyo ichambua Jf tangu jana. Hapa anatumia desa
 
Hili swala la madaktari analiongelea wakati spika amesema jambo likiwa mahakamani haliruhusiwi kuongelewa au ni kwa wabunge tu au rais yupo juu ya mhakama!?
 
Raisi wa madesa!! Ukimchek utadhan anatoa akilini mwake Kumbe kuna screen ya desa mbele!! Mh shame. Ngoja tutamsikia akijigonga swala la ulimboka.
 
hotuba yake nimeisoma yote na nimeshawishika kuwa huyu kikwete yuko nyuma ya mpango mzima wa kumdhuru ulimboka hasa nikisoma aya ''hii Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali.Na, kuhusu mgomo, Mahakama Kuu imekwishatoa amri ya kusitisha mgomo. Anayekaidi amri ya Mahakama ananunua ugomvi na mhimili huo wa dola ambao wenyewe una mamlaka ya kumtia adabu mtu huyo. ''


...halafu imejaa uchonganishi...jk hajui tofauti ya MAT na chama chama cha madaktari
 
Kikwete ni muongo. Tabia mojawapo ya muongo aliyekubuhu anapobanwa ni kuwagawa wanaomsuta kwa kuwachonganisha wajione wako tofauti. Anasema "wanapodai nyongeza posho na mshahara wakumbuke kuwa kuna fani nyingine hawapati kabisa" Nyuma ya pazia wafanyakazi wanagawanywa. Matokeo ni kuwa wafanyakazi wajinga hawatawaunga mkono madaktari,....dhaifu...atapata nguvu.
 
Anajaribu kupindisha UKWELI anaoujua kuhusu Rais wa Chama cha madaktari (MAT), Namala Mkopi kuwa aliagizwa akawatangazie madokta waache mgomo ambao MAT haujitisha.
MAT ni professional association na haikuitisha mgomo.
Madaktari waliunda chombo kinachotambuliwa na wao wenyewe Jumuiya ya Madaktari kilichokuwa chini ya Ulimboka.
Kwa nini serikali haikuishitaki hii jumuiya, ambayo ndo iliitisha mgomo.
Kinyume chake ni mbinu chafu za kummaliza Ulimboka.
 
Back
Top Bottom