Hotuba ya Rais ya mwisho wa mwezi Februari, 2011

nilishasahau kumbe bado huwa anahutubia? the chap has guts na ni kwa nini he normally refers to Mzee Nyerere not baba wa taifa?

Tuliambiwa jinsi gani alitoka monduli na kupokelewa na Shimbo
tangu hapo yeye hamjui Nyerere kuwa ni Baba wa Taifa.
Hakutakiwa kumwelezea mabaya, bali ajilinganishe naye kwa mazuri sio mabaya
Mtu unajilinganisha naye kwa mabaya kama yuko hai lakini akishakufa huwa hatusemi mabaya(ingawa ni lazima yawepo kwa kila mtu)
 
Sijapata muda wa kuichambua hotuba ya President lakini kwa harakahaka haireflect chochote katika maisha ya kila siku ya mtanzania, ni siasa zilezile za miaka 47, mabomu ya gongo la mboto, kama mambo ya jeshi ni siri inakuwaje mnawashirikisha wamarekani kuchunguza issue ya JWTZ, usalama wa taifa wewe mwenyewe unauingiza matatani usiwalaumu Chadema!

Hali ya chakula, namkumbuka story ya Tanzania is a sleeping giant! in another words the government is totally sleeping ndo maana wanaongelea kilimo kwanza wakati maji ya kunywa tu ni tabu km 12 kutoka ikulu! Njaa itazidi kulikumba taifa maana misingi na dhana nzima ya kilimo ilishavurugwa na hakuna kiongozi wa ccm ana nia ya dhati ya kuhakikisha taifa linatekeleza sera ya kilimo kwanza, shortly maji kwanza na kilimo kifuate, kinachotusumbua sasa si kilimo ni ukame na kama tukitatua tatizo la maji automatically kilimo will be the second, hakauna mahala popote duniani wamefanikiwa katika nyanja ya kilimo kwa kutegemea mvua! Kwa kuwa hata maji ya matumizi ya majumbani bado ni tatitzo sera ya kilimo kwanza mkuu wa nchi usiliongelee na bei za vyakula zitazidi kupaa kwa sababu ya uzalishaji mdogo and as I can see your advisors on agricultural revolution have already misleaded you and your eyes are still closed on that.

Suara la umeme, kimsingi serikali haina utashi wa kulimaliza hili maana inaonekana kuwa ni katika shida na dharura ufisadi unafanikiwa, kama serikali ya ccm ingelikuwa na nia ya dhati ya kutatua hili tatizo 2002 na 2006 ingebakia kuwa historia.

Bei ya sukari mkuu, naona kama unatania. Kwa sasa mfumuko wa bei si kwa sukari ni kwa kila bidhaa inayotumiwa na binadamu na kwa bahati mbaya sukari siku hizi ni kama anasa kwa watanzania tuliowengi, na kushusha bei ya sukari ukiacha bei za bidhaa muhimu kama unga, maji,mafuta ya kupikia, unga mchele, maharage, sabuni, n.k vikiwa juu inaonyesha ni kwa jinsi gani unavyoongoza nchi kwa hisia na si kwa uhalisia wa maisha ya watu unaowaongoza! Wake up this is Tanzania not Europe where coffee and tea are part of life JK!

Usalama wa Taifa
Mkuu kama umeweka jeshi chini ya wamarekani huku unawaogopa chadema na unadai Tanzania ni nchi ya Demokrasia tukuelewe vipi! Isotoshe inaonekana huko busy sana kutatua matatizo ya watanzania wachache especially hapo Ikulu na hupati muda wa kuangalia yanayojiri nchi za wenzako wanaosema wanaongoza kwa demokrasia lakini nguvu ya umma imewaondoa madarakani. Mheshimiwa rais kwa nafsi yako unajua ni jinsi gani umeingia hapo magogoni 2010 kama ni kwa kura halali basi kwa mtu mwadilifu na mwenye akili timamu hawezi kuhofu Chadema badala yake atachapa kazi kuwatumikia wananchi waliomweka madarakani! Kama uliingia kwa kuuhadaa ulimwengu kuwa demokrasia imefuatwa kama tunavyojua wengi wetu fungulia silaha wafuasi wako wapambane na raia kama Gadafi anavyofanya Libya!
 
Hivi kwa nini asingetoa hata fursa kwa wale makameraman na wahariri wanaokuwepo wakati anabwabwaja wakamuulizavijiswali hata vya kumwezesha kukidhi kiu ya watz badala ya huu mfumo wake wa kiimla anasema amemaliza chapeni lapa .
Wananchi kilio chetu cha malipo ya dowans na atueleze mazungumzo ya serikali yake na mwarabu yalifanyikaje wakati alishasema hamjui ina maana alionana na viongozi bila appointment?
Njaa kauli hakuna mtz atakufa njaa tumeizoea huwa inatamkwa na wanakufa vilevile na hakutolewi maelezo yaliyotulia
any way acha niendelee kuangalia mbele mkwere kaaaaaaaaazi kweli kweli
kwa mtazamo huo naona 2015 itakuwa ni mbali sana hata yeye atakuwa analiona hilo pia
 
Kiongozi.. hii hoyuba imekwishasomwa au itasomwa jioni ya leo..???



Labda Invisible atueleze ameipata wapi??


Ina maana siku hizi anatoa hotuba bila kutangaza...ili watu wasiangalie anavyochemka. Inaelekea kisha juwa kuwa wananchi hawampendi tena.
 
Sikutegemea Rais mzima aanze kulalamika lalamika, hiyo ndiyo siasa, ukweli ni kuwa umeshindwa kazi, unatakiwa uondoke, na usifikiri wa tz ni wajinga sana na mpaka leo hawajui kuwa uliiba kura. Ikibidi kuondoka ondoka tu CHADEMA ndio wakombozi wa nchi hii.

Na kweli aisee, CHADEMA mpaka wanakuahidi vitu vya bure , angalia tu mkeo Mbowe mbayaaaaaa!
 
Naona umeongea yote mkuu Paul J,
Nashukru sana kwa mchango wako
Sijapata muda wa kuichambua hotuba ya President lakini kwa harakahaka haireflect chochote katika maisha ya kila siku ya mtanzania, ni siasa zilezile za miaka 47, mabomu ya gongo la mboto, kama mambo ya jeshi ni siri inakuwaje mnawashirikisha wamarekani kuchunguza issue ya JWTZ, usalama wa taifa wewe mwenyewe unauingiza matatani usiwalaumu Chadema!

Hali ya chakula, namkumbuka story ya Tanzania is a sleeping giant! in another words the government is totally sleeping ndo maana wanaongelea kilimo kwanza wakati maji ya kunywa tu ni tabu km 12 kutoka ikulu! Njaa itazidi kulikumba taifa maana misingi na dhana nzima ya kilimo ilishavurugwa na hakuna kiongozi wa ccm ana nia ya dhati ya kuhakikisha taifa linatekeleza sera ya kilimo kwanza, shortly maji kwanza na kilimo kifuate, kinachotusumbua sasa si kilimo ni ukame na kama tukitatua tatizo la maji automatically kilimo will be the second, hakauna mahala popote duniani wamefanikiwa katika nyanja ya kilimo kwa kutegemea mvua! Kwa kuwa hata maji ya matumizi ya majumbani bado ni tatitzo sera ya kilimo kwanza mkuu wa nchi usiliongelee na bei za vyakula zitazidi kupaa kwa sababu ya uzalishaji mdogo and as I can see your advisors on agricultural revolution have already misleaded you and your eyes are still closed on that.

Suara la umeme, kimsingi serikali haina utashi wa kulimaliza hili maana inaonekana kuwa ni katika shida na dharura ufisadi unafanikiwa, kama serikali ya ccm ingelikuwa na nia ya dhati ya kutatua hili tatizo 2002 na 2006 ingebakia kuwa historia.

Bei ya sukari mkuu, naona kama unatania. Kwa sasa mfumuko wa bei si kwa sukari ni kwa kila bidhaa inayotumiwa na binadamu na kwa bahati mbaya sukari siku hizi ni kama anasa kwa watanzania tuliowengi, na kushusha bei ya sukari ukiacha bei za bidhaa muhimu kama unga, maji,mafuta ya kupikia, unga mchele, maharage, sabuni, n.k vikiwa juu inaonyesha ni kwa jinsi gani unavyoongoza nchi kwa hisia na si kwa uhalisia wa maisha ya watu unaowaongoza! Wake up this is Tanzania not Europe where coffee and tea are part of life JK!

Usalama wa Taifa
Mkuu kama umeweka jeshi chini ya wamarekani huku unawaogopa chadema na unadai Tanzania ni nchi ya Demokrasia tukuelewe vipi! Isotoshe inaonekana huko busy sana kutatua matatizo ya watanzania wachache especially hapo Ikulu na hupati muda wa kuangalia yanayojiri nchi za wenzako wanaosema wanaongoza kwa demokrasia lakini nguvu ya umma imewaondoa madarakani. Mheshimiwa rais kwa nafsi yako unajua ni jinsi gani umeingia hapo magogoni 2010 kama ni kwa kura halali basi kwa mtu mwadilifu na mwenye akili timamu hawezi kuhofu Chadema badala yake atachapa kazi kuwatumikia wananchi waliomweka madarakani! Kama uliingia kwa kuuhadaa ulimwengu kuwa demokrasia imefuatwa kama tunavyojua wengi wetu fungulia silaha wafuasi wako wapambane na raia kama Gadafi anavyofanya Libya!
 
Naona sasa JK anaweweseka na kuruka ruka kama kunguru. Amegeuza Magogoni mahala pa kupiga story na kuwaalika wapiga ramli na kamali pamoja na biashara za mfukoni anafikiri atapona. Amegeuza mwelekeo kufikiri wote ni mazezeta kutoka msoga.

Moto wa mageuzi ulioanzia Tunisia hauwezi kuzimwa na mafisadi koko kutoka Msoga au Monduli.

Soma historia, acha kukurupuka mkuu ni nchi zenye utofauti mkubwa sana. Soma historia tangia nchi hizo zinaitwa Abbysynia, ndipo utajua !
 
Labda Invisible atueleze ameipata wapi??


Ina maana siku hizi anatoa hotuba bila kutangaza...ili watu wasiangalie anavyochemka. Inaelekea kisha juwa kuwa wananchi hawampendi tena.
Hiyo mbona ni kitu cha kawaida kabisa, hata USA Hotuba nyingi za Obama huwa zinatolewa mapema tu kabla ya speech yenyewe
hiyo inasaidia wadau mbali mbali kuipitia na kupata maoni yao
kupitia hapo hata ambao hawakupanga kumsikiliza kulingana na shughuri zao wanaweza kumsikiliza
pia ikumbuke si kila mtu anakuwa na TV ilisikilize hiyo hotuba
 
Sijaona rais kama huyu tangu nipate akili.. Kwanza ameiba kura.. Pili hana chakusema zaidi ya blabla tu..

Kwanza hotuba yenyewe siyo ya maana maana hajazungumzia mambo ya maana mfano elimu, afya...

Nadhani ni kwa sababu alikuwa bizi na maandalizi ya kwenye ufaranza kula raha na cote d'ivore kupatanisha mafisadi kama yeye...
 
JK acha hofu,jitetee kwa kuchapa kazi yamkini ukanusuru imani ya wachache ambao hawajaamua kuhama chama...
Mambo ya kukaa na kulalamikia CHADEMA ni uphobia....
If yoou do something people will see and appreciate otherwise complaining will not help..
kama mambo magumu waachie wenzio nao wajaribu.....
Natamani huo ushauri angeweza kuusikia na kuufanyia kazi
 
Tuliambiwa jinsi gani alitoka monduli na kupokelewa na Shimbo
tangu hapo yeye hamjui Nyerere kuwa ni Baba wa Taifa.
Hakutakiwa kumwelezea mabaya, bali ajilinganishe naye kwa mazuri sio mabaya
Mtu unajilinganisha naye kwa mabaya kama yuko hai lakini akishakufa huwa hatusemi mabaya(ingawa ni lazima yawepo kwa kila mtu)

hapo kwenye red,
1- ni dalili ya kushindwa na unatoa sababu zisizo za msingi, nyerere ameacha urais miaka 27 iliyopita lakini bado unajilinganisha naye.

2 - Mtu anayefanya hivyo ni dalili ya kuwa hakupata makuzi safi
 
hii hotuba ni kweli inatia mashaka kama imetoka kwa JK, maana mkuu wa nchi naye analalamika utadhani yuko 'kijiweni' badala ya kutoa mwelekeo wa mambo!!! Hivi walisema baada ya kuondoka January Makamba ni nani vila anamuandalia hotuba siku hizi???? ...ilibidi aweke zake naye au ni ya kutuzuga wakuu maana siiamini1
!!
 
Sijaona rais kama huyu tangu nipate akili.. Kwanza ameiba kura.. Pili hana chakusema zaidi ya blabla tu..

Kwanza hotuba yenyewe siyo ya maana maana hajazungumzia mambo ya maana mfano elimu, afya...

Nadhani ni kwa sababu alikuwa bizi na maandalizi ya kwenye ufaranza kula raha na cote d'ivore kupatanisha mafisadi kama yeye...

Mkuu mbona "KWANZA" zinakuwa nyingi?? Huwa kuna kwanza moja tu. Ukiona mtu yuko hivyo, basi ujue ni wale ambao hulka yao ni ya kulaumu tu. Kwanza hiki, pili hiki, halafu kwanza hiki???
Those a typically baseless allegations to the President.
 
Kuhusu CDM na usalama wa raia sijaona popote pale ambapo wamehatarisha usalama. Mimi naona kwa CDM kuhamasisha wananchi, usalama wa viongozi wabovu na mafisadi unakuwa hatarini.
 
hii hotuba ni kweli inatia mashaka kama imetoka kwa JK, maana mkuu wa nchi naye analalamika utadhani yuko 'kijiweni' badala ya kutoa mwelekeo wa mambo!!! Hivi walisema baada ya kuondoka January Makamba ni nani vila anamuandalia hotuba siku hizi???? ...ilibidi aweke zake naye au ni ya kutuzuga wakuu maana siiamini1
!!

dalili kuu ya kushindwa uongozi ndiyo hiyo. wake up!!spika, pm, president, mawaziri, etc wote ni waliaji tu, hakuna mwenye suluhisho
 
Hapa ndipo mahala pekee( kutokana na heshima yake) unaweza kuongea haya na ukaonekana shujaa, sidhani hata pale kinondoni Slaa anaruhusu lugha hizi..Hongera JF kwa kushusha heshima yako as days zinavyosonga.

Nduka avatar yako huwa inanitisha kusoma thread zako hata kama umeandika maneno ya hekima.

Can you get a replacement please if you dont mind though.

moz-screenshot-1.png
 
Hii hotuba imejaa hofu; imejaa kutokujiamini na imekaa kishari shari. Hivi mbona hajasema kuwa hata Misri walikuwa na Uchaguzi mwaka jana na walikuwa kwenye "katiba" yao ambayo nayo ni sheria kuu ya nchi wakiweka vipindi vya miaka mitano mitano?
 
Heshima mkuu Invisible, Nashindwa kuamini kama hii kweli ni hotuba ya mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata kama mimi siyo mtaalam wa kuandaa hotuba naamini walioindaa hamwamtakii mema rais.

Haiwezekani rais akaongea kwa kulalamika kama mtu wa kawaida badala ya kutoa mwelekeo na maamuzi sahihi. Mheshimiwa rais naomba tu ufahamu kuwa hali ya wananchi siyo nzuri, maisha yamekuwa magumu sana na watu wanalalamika. Bei haijaongezeka kwenye sukari tu ni karibia kila kitu; sasa leo unapoelezea tu sukari na kuonyesha kuwa bei ya shs. 1700 ni sawa hii ni changamoto. Bei za vitu vingi zimepanda katika kipindi cha mwaka mmoja wakati vipato vya watu hasa wanaotegemea mishahara bado viko pale pale.

Hata kama mimi siyo mwanachama/mkereketwa wa CHADEMA lakini maneno yaliyoko kwenye hotuba hii dhidi ya Chadema siyo mazuri sana na nafikiri waandishi wangetafuta jinsi ya kufikisha huu ujumbe lakini kwa njia tofauti.

Sikumbuki kama Januari 2011 tulipata hotuba ya mheshimiwa rais, kama haikuwepo ningetegemea pia azungumzie suala la elimu na hasa matokeo ya kidato cha nne na migomo ya vyuo vikuu.

Vipi kuhusu masula ya kimataifa na hasa yaliyotokea Tunisia, Misri na yanayoendelea Libya na Yemen; anasemaje mheshimiwa rais au ana hofu kuwa inawezekana CHADEMA wataanzisha hiyo kitu kwetu.

Mungu Ibariki Tanzania na Amani yako izidi kutawala katika JINA LIPITALO MAJINA YOTE JINA LA YESU.
 
Huyu mkuu vipi!? anaiogopa chadema kiasi hicho!!!
ANAOGOPA MAPINDUZI YA UMMA!
POLE SANA JK!
 
Viva Chadema..kwa kumtoa nyoka pangoni,
joka halina pa kwenda.. baada ya siku 9 (nadhani zimebaki 6) ni kuponda kichwa chake tuu!
 
Back
Top Bottom