Hotuba ya Rais Xi Jinping wa China kwenye Mkutano wa Kilele wa COP26 yatoa mwanga wa matumaini

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,031
VCG31N1350886400.jpg

Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi (COP26) umeanza huko Glasgow, Scotland, ukikaribisha viongozi, wataalamu na wanaharakati mbalimbali duniani ambao watajadili na kutafuta njia za kupunguza mabadiliko ya tabianchi. Katika kipindi hiki cha wiki mbili za majadiliano na mazungumzo, nchi shiriki zitaafikiana juu ya njia kali zaidi za kupunguza utoaji wa hewa ya ukaa ili dunia ipate nafasi ya kufikia malengo ya kukomesha kuongezeka kwa joto duniani yaliyowekwa kwenye mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP21) mjini Paris mwaka 2015.

Kwenye mkutano huu viongozi wa mataifa mbalimbali yenye uchumi mkubwa duniani, walikamilisha majadiliano ya siku mbili ambayo yameweka msingi wa kazi za mkutano wa mabadiliko ya tabianchi wa Umoja wa Mataifa huko Glasgow, Scotland, kwa kutoa ahadi ya kusawazisha utoaji wa hewa ya ukaa kufikia katikati ya karne hii.

Athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi sasa ndio zinajidhihirisha wazi na kushuhudiwa katika maeneo mengi hasa ya Afrika. Athari hizi zinazindua watu duniani kutoka kwenye usingizi mzito, kwamba hatua za haraka zinahitajika kuchukuliwa na jamii ya kimataifa. Vilevile jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kufufua uchumi duniani, hizi ni changamoto zilizopo mbele yetu ambazo ni lazima kukabiliana nazo kwa pamoja.

Viongozi mbalimbali walitoa hotuba kwenye mkutano huo na kueleza namna walivyojizatiti katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Lakini hotuba iliyonivutia zaidi ni ile aliyoitoa rais Xi Jinping wa China kwa njia ya maandishi kwenye Mkutano wa Kilele wa COP26, ambayo imegusia mambo mengi, yakiwemo kutoa mapendekezo matatu kwa wadau.

Mapendekezo hayo, kwanza ni kushikilia makubaliano ya pamoja. Katika pendekezo hili rais Xi anajaribu kusisitiza kwamba wakati tunapokabiliana na changamto duniani kama vile mabadiliko ya tabianchi, basi pande zote duniani ni muhimu sana kuwa kitu kimoja na kuwa na jukwaa moja la ushirikiano. Wahenga wanasema “kidole kimoja hakivunji chawa” hivyo zile nchi ambazo zinajitenga au kutotaka kushiriki kwenye juhudi za pamoja katika wakati huu mgumu, zitazorotesha mapambano haya. Nchi zinatakiwa kukubaliana, kuzidi kuamianiana, kuongeza ushirikiano na kufanya kazi pamoja ili kuifanya dunia iwe mahali salama.

Pendekezo la pili ni kuchukua hatua halisi. Wahenga wanasema penye nia pana njia. Hivyo rais Xi hapa anajaribu kuziasa nchi mbalimbali kwamba zinatakiwa kutilia maanani na kujua kwamba sasa dunia ipo katika hali mbaya na ya hatari, bila ya kuchukua hatua halisi za kugeuza mwelekeo, kweli dunia itaelekea kubaya. Kwenye mkutano kama huu, viongozi wengi mara kwa mara wamekuwa wakitoa ahadi nyingi, lakini ikija kwenye suala la uchukuaji wa hatua halisi, hapa ndio ugumu unapoonekana. Nchi za Afrika zimekuwa zikikabiliwa na hatari kubwa sana zikiwemo, ukame na janga la njaa kutokana na uhaba wa mvua. Kwa hiyo nchi zilizoendelea hazipaswi kujiangalia kwa upande wao tu, bali pia zinatakiwa kutupia jicho na kuzisaidia nchi zinazoendelea.

Pendekezo la tatu ni kuharakisha mageuzi ya kijani. Tunafahamu kuwa nchi nyingi kwa sasa zimeingia kwenye zama ya sayansi na teknolojia, kwa kuonelea hilo rais Xi anashauri ni bora kudhibiti na kutumia sayansi na teknolojia katika kugeuza na kuboresha sekta za nishati na rasilimali pamoja na kuendelea kusukuma mbele marekebisho ya muundo wa viwanda, kukuza uchumi wa kijani na kutumia njia mpya ambazo zitaunganisha maendeleo na uhifadhi wa mazingira.

Mabadiliko ya tabianchi tayari yameshaiharibu dunia. Kwa hiyo mkutano wa COP26 wa Glasgow ni muhimu sana, kwani kwenye mkutano huu viongozi wamenuia kuweka malengo mapya ya kupunguza utoaji wa hewa ya ukaa sambamba na mipango ya kuyaunga mkono, kama ilivyokubaliwa mjini Paris mwaka wa 2015.

Wahenga wanasema “Maneno yawe mafupi vitendo viwe virefu”. Tunatarajia viongozi sio tu watakuwa wanatoa ahadi hewa, bali watachukua hatua halisi kwa pamoja za kutekeleza na kukabliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuilinda dunia, ambayo ni makazi yetu sote.
 
Kikubwa pesa zitakazotolewa na EU kutoka kwenye budget yake i-reflect uhalisia wa huo mradi wa kupunguza gesi ukaa sio iishie kwenye OC
 
Kwa kuwa wao ni mataifa yanayoharibu hali ya hewa duniani kwa manufaa yao na faida hawajali na wataendelea kutoa ahadi nyingi

Wapo baadhi wanajitahidi kama kutengeneza magari ya umeme nk.Ila mchina ndio na muhindi ndio waharibifu wakubwa wasiosikia kabisa. Tuone miaka 10 ijayo watatupeleka wapi
 
HUYU MTOA MADA NI KIBARAKA WA WANYONYAJI NA WABAGUZI WAKUBWA WACHINA
 
China ndio inaongoza kwa uchafuzi wa hewa lkn rais wake hajahudhuria mkutano na badala yake anawapa notice wenzake.kwa mwanzo huu,tushashindwa tayari
 
Back
Top Bottom