Hotuba ya Rais wa Tanzania kuhusu mustakabali wa EAC

Nsaji Mpoki

JF-Expert Member
Nov 5, 2007
396
65
Tuna imani kuwa jana mlisikiliza hotuba ya Rais wa Tanzania kuhusu mustakabali wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Rais ameweka msimamo wazi kuwa Tanzania haina nia ya kujitoa kwenye Jumuiya hiyo pamoja na kuwa marais wa Kenya, Uganda na Rwanda wamekuwa wakiingilia masuala yaliyoridhiwa na nchi wanachama. Amekwenda mbali zaidi kusema marais hao wamekuwa wakifanya mikutano inayoashiria kuitenga Tanzania. Wakenya, Waganda na Wanyarwanda mnasemaje? Mnaona ni sahihi wakati huu hasa baada ya kuwekeza kwa siku nyingi katika umoja huu kufarakana?
 
Tuipe mda hii era nafkiri amefanya busara kubaki bado hatujawa na sababu za kujitoa.
 
ilikua clear kua tushirikiane kama kawaida lakini kuna mambo hatutaki na ndio msimamo wetu kama issue ya ardhi, uhamiaji na ajira...... kwani kuungana mpaka haya yawepo???? tushirikiane kwenye biashara, kurahisisha bidhaa kusafiri kwa urahisi, kuhakikisha hakuna usumbufu kwa bidhaa ktk boda nk
 
TANZANIA NA EAC: Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametuma waziri wake nchini, amesema nchi yake haitaitenga tena Tanzania kwenye masuala yote yanayohusu Jumuiya.
 
Kila tunapojadili muungano nyie Watz hukimbilia suala la ardhi, hivi nani kawaambia hizi nchi zingine hazina ardhi. Tunachotaka ni ushirikiano wa kibiashara, hatuna haja kabisa kuungana kama nchi, hiyo sio sustainable maana kila nchi ina changamoto zake. Sasa hata muungano wa Zanzibar na Tanganyika bado kuna utata hadi leo. Sasa watalii watakua na uwezo wa kuzunguka nchi zote kwa kutumia visa moja, hamna gharama tena. Inakua rahisi ku-market vivutio vya Rwanda ukiwa kwetu Kenya na vilevile vya Kenya ukiwa Rwanda ama Uganda.
Nikitaka fanya consultancy kwa kampuni ya Rwanda ama Uganda, sina haja ya kupitia urasimu wa kiajabu na ghali hata kwa SME (Small Medium Enterprises). Nimeipenda hiyo kauli ya rais Kikwete kwamba hatoki, hivyo basi sisi tutaendelea na tuliyoyanzisha, Tanzania ikiona yana tija basi tutawakaribisha kwa mikono yote wazi.
 
Back
Top Bottom