Mama kazingua leounajua sijaamini kabisa,yaani wizara ya elimu kaisamaraizi hatari!
Kwa hii hotuba Watumishi wa Umma tuendelee kukaza mkanda,huyu si yeye!
TUMECHOKA maneno Sasa tunataka MATENDO.
Anaongea vitu hata havifanyiki!!!
Mama anafanya siasa Mipasho.

kwa kweli. Mipango na maongezi ni mengi sana. Wengi hatuna uhakika wa utekelezaji wa mambo yote hayo. Nahisi pia anapenda makofi, kama ni hivi pana shida hapa. Zitakuwa zinatafutwa hotuba tu za kuhakikisha kuna makofi kutoka kwa audience baaasi!!
 
Mama ashauriwe mambo ya mitandaoni aachane nayo. Haya ya mitandaoni ni madogo sana kwake kumuumiza kichwa.
 
tupunguze mipango tudeal na machache tunayoweza, tunashika shika mengi sana kwa pamoja.....hii inaitwa kudanda danda...
Ndio naona Mama analuck hili. Anamipango lukuki. Inabidi yeye na team yake wawe realistic na mipango hii. Na si kila hotuba aseme mipango 100!! Aongee tu kiufupi mambo ya msingi kwa muelekeo wa serikali yake.

Hizo details ataziongea akiwa kwenye baraza la mawaziri au akiwa kwenye sekta husika (mfano akiwa ziarani). Hii mipango mingi nahisi itaishia kwenye karatasi za hotuba tu , mwisho Watanzania waishie kuwa disappointed.
 
Price tag mbele ya Mtutu wa Bunduki ni nini zaidi ya kusurender? Sema mmechukia Mama alipotaja neno Demokrasia.
Wala akuna aliechukia.kinachotakiwa watanzania wote twende na mama akipitishwa tena na CCM kugombea 2025 pia twende nae ili atimize kikamilifu mchakato wa demokeasia,atutaki wenyeviti wa kudumu kwenye vyama vya siasa.

Mtakumbuka shuka kumekucha.
 
..mimi nilisema atcl haina tija.

..na nilisema toka wakati wa jk.

..sasa hebu tueleze kama wewe unaamini atcl ina tija.
Na kosa kubwa zaidi ilikuwa kuipa 'monopoly'. Hilo linasababisha kusiwe na ubunifu kwasababu hakuna competition. Usafiri wa anga ulikuwa mzuri sana kabla ya ATCL na nadhani ilikuwa bora kuimarisha mazingira ya uwekezaji kuliko kinachoendelea sasa hivi.
..Stieglers nimesema niko 50/50. Inaweza kuwa na tija kama tumejenga kwa mkopo wenye masharti nafuu.

..Je, wewe unafahamu kama mkopo wa kujenga stieglers ni wa masharti nafuu? Mbunge wako anafahamu?
Aliyesaini mkataba kaondoka na hatujui katuachia msala gani. Hivi kwanini hawa Wabunge hawadai kuona mikataba? Kwanini wananchi ambao ni walipa kodi wasione mikataba?
..Sgr nimeonya kwamba tuwe waangalifu kwenye mkopo. Pia nimeonya Sgr kwamba faida iko kwenye mizigo, na siyo abiria.

..Je, tuna mkakati wa kuwa na viwanda vitakavyozalisha shehena / mizigo ya kutosha ili Sgr iendeshwe kibiashara?

..Kama Tazara inaendeshwa kwa hasara, je ni makosa wananchi kuwa na wasiwasi kuhusu hatima ya Sgr?
Hili swali hakuna anayejiuliza. Hivi kwanini Tazara inajiendesha kwa hasara? Na kipi kitakuwa tofauti na sgr?

Sikatai miradi lakini hatuna akili za kuhoji ! Tunashangilia tu hatujifunzi kutoka historia
 
Ushachukua kadi ya ccm mpya?
Njoo tujiunge mwamba ccm ni ile ile
Yaani mama ndo kwanza ana mwezi na siku tatu mnataka awe kaigeuza Tz kuwa kama China.

Halafu jiwe miaka kumi mliona haimtoshi mkaanza upuuzi wa kuilawiti demokrasia ili atawale 'milele'

Tuachieni mama yetu anatosheleza, mnaomtaka jiwe njia ni nyeupe, kamba na sumu za kila aina zimejaa tele.
 
Ukimaliza hate kwa Magu mtamgeukia mama nae hafai...
Hata Kikwete alikuwa afwazali ya Magu pale mwanzoni...

Akija mwingine tutaimba bora ya huyu kuliko mama
Lakini nikizikumbuka enzi za MAGU,naona Mara 100 MAMA hata akivurunda hatafkia nusu ya Magu
 
Awamu ya Sitta,Awamu ya Sitta kweli.

Mimi sina imani kubwa na uongozi wa huyu Rais.

Watu wengi wamemsifu katika mitandao lakini hajawaona.

Kila nafsi inayoleta taabu katika mitandao itaonja mauti. Mange Kimambe aliweka picha ya watu wanakimbia kwa taharuki kubwa porini.
Akasema" hivi ndivyo ilivyokuwa ndege ilipofika Chato kwa mara ya kwanza."

Haya mambo ya utani ya kawaida katika mitandao ndiyo unatamka Fatwa.

Haya mambo siyo conspiracy theory. Conspiracy theory watu watakuambia Magufuli bado hajakufa.
 
Mama anasubiri aukwae uenyekiti wa ccm ndio aanze kutengeneza legacy yake.
Hotuba ya bungeni alilenga kuwafurahisha wana ccm.
 
Sidhani kama atawateua wanawake katika nafasi mbalmbali kwasababu ni wanawake, I am made to believe that rais samia is above this!!! Wanawake watateuliwa kufuatana na uwezo wao; lakini kama atakuwa anawateuwa kwa sababu ya kuwa wanawake, atakuwa amewadhalisha na kuwadharau sana!
 
Lakini hili litawezekanaje bila kubadili sheria mbaya zilizopo? Mtu anakamatwa bila uchunguzi kukamilika, matokeo yake wanaishia kumbambikizia kesi.
 
Baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya ukatibu mkuu iliyodumu kwa siku 30 na kupewa ubunge.

Bashiru hajaonekana hadharani mara tu baada ya kuapishwa mpaka leo.

Je, yuko wapi kiongozi huyu mahiri na mjamaa?
 
Back
Top Bottom