Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 322
- 645
Kwenye hotuba yake Mwenyekiti wa CCM amezungumza mambo mengi. Lakini ninataka ninukuu mambo mawili.
Jambo la kwanza amesema yeye na viongozi wengine hawana mgombea mfukoni. Jambo la pili amewaagiza viongozi kutenda haki kwenye vikao vya uteuzi na kutokuwakatisha tamaa wengine.
Funzo kubwa kwenye nukuu hizi ni kuwa kijana yeyote mwenye nia ya Udiwani akajaribu bahati yake. Vijana waache kutumia muda mwingi kuwanadi watu, badala yake vijana watumie muda kujitengeneza wao na si kutengeneza watu.
Si hivyo tu, pia vijana waache kuaminishwa na watu wanaopita majimboni kuwa wametumwa na watu wakubwa, hizo ni propaganda za kutafuta huruma za kupendwa.
Kama wewe huna mpango wa kugombea na kazi yako ni kuwanadi watu, basi tumia vizuri hiyo fursa bila kuwaathiri wengine.
My take: Hadi Sasa mwenye uhakika wa kuteuliwa kugombea ni Konde boy tu, wengine huko majimboni wasiwasumbue kuwa wametumwa. Wamejituma!
Jambo la kwanza amesema yeye na viongozi wengine hawana mgombea mfukoni. Jambo la pili amewaagiza viongozi kutenda haki kwenye vikao vya uteuzi na kutokuwakatisha tamaa wengine.
Funzo kubwa kwenye nukuu hizi ni kuwa kijana yeyote mwenye nia ya Udiwani akajaribu bahati yake. Vijana waache kutumia muda mwingi kuwanadi watu, badala yake vijana watumie muda kujitengeneza wao na si kutengeneza watu.
Si hivyo tu, pia vijana waache kuaminishwa na watu wanaopita majimboni kuwa wametumwa na watu wakubwa, hizo ni propaganda za kutafuta huruma za kupendwa.
Kama wewe huna mpango wa kugombea na kazi yako ni kuwanadi watu, basi tumia vizuri hiyo fursa bila kuwaathiri wengine.
My take: Hadi Sasa mwenye uhakika wa kuteuliwa kugombea ni Konde boy tu, wengine huko majimboni wasiwasumbue kuwa wametumwa. Wamejituma!