Hotuba ya Rais Kikwete kwa watanzania mwezi Septemba 2011

Acha habari za enzi hizo wewe! nisubiri kidogo?unadhani nina kazi tu ya kuangalia tbc?muwe specific siku nyingine.

Mnaweka hotuba ya rais saa 4 ili watoto wanaofuatilia tamthilia waangalie?maana watu wazima mida hii wako bize kama si kujaza dunia basi wapo kwenye home library zao kuongeza maarifa.
siku nyngne uwe una subira kdogo..
 
HIvi kulikuwa kuna haja ya hotuba? Mbona sijaona kabisa jipya katika hii hotuba? Si angeacha tu, kweli anakuja mbele ya watanzania kutuambia kwamba alisifiwa sana umoja wa mataifa na kurudia masimulizi ya story zilizokwishatokea?

Tulitarajia hotuba yake ije na suluhisho na si kurudia kilichosemwa au kutokea.
I am sorry kama nipo too rude kwa huyu mtu, but nimesoma hotuba mwanzo hadi mwisho, sijona mahali anapoongelea utatuzi wa matatizo yetu yanayotukabili (eg umeme, kushuka kwa shilingi, ajali mfuliulizio na mikakati ya kuzikabili etc).
 
.............Wakuu tuwe wazi kabisa,mbona inatia hasira? wapi mambo yafuatayo?
  1. Kupanda gharama za maisha...
  2. Kupanda kwa bei ya mafuta kila siku....
  3. Malipo ya Dowans na mikataba mengine feki...
  4. Ajali za kila siku(hili sio kificho,kila siku watu wanakufa hii nchi kwa ajali)
  5. Matatizo ya umeme yasiyokwisha....tulidanganywa kuwa mwezi wa 9 mgao utapungua,badala yake makali ndio yanaongezeka..
Yani hotuba nzima imejaa safari ya marekani wakuu,full kujisifia sifa zisizo na tija wala manufaa kwa watanzania? Ndio maana watu wengi wameacha kusoma au kusikiliza hotuba za huyu jamaa...Kuna nini hapo cha kuleta matumaini? Jamani huyu jamaa tumfanyaje?

Najutia muda wangu niliokaa kumsikiliza na kusoma hotuba hii....
 
Hajui vipau mbele vya nchi na matatizo makuu yanayoisibu nchi anayoitawala, katika busara ya kawaida ningespenda kusikia umeme, malipo ya downs, elimu ya juu na mikopo, mitihani ya kidato cha nne anagalau watanzania hao zaidi ya elfu ishirni rais wao angewatakia mitihani miema hilo ni suala la kitaifa, suala la serikali ya umoja wa kitaifa ya libya nk
 
HIvi kulikuwa kuna haja ya hotuba? Mbona sijaona kabisa jipya katika hii hotuba? Si angeacha tu, kweli anakuja mbele ya watanzania kutuambia kwamba alisifiwa sana umoja wa mataifa na kurudia masimulizi ya story zilizokwishatokea? Tulitarajia hotuba yake ije na suluhisho na si kurudia kilichosemwa au kutokea.
I am sorry kama nipo too rude kwa huyu mtu, but nimesoma hotuba mwanzo hadi mwisho, sijona mahali anapoongelea utatuzi wa matatizo yetu yanayotukabili (eg umeme, kushuka kwa shilingi, ajali mfuliulizio na mikakati ya kuzikabili etc).

Rais hawezi kuongea kila kitu ambacho watu wanataka. Akifanya hivyo basi inabidi atumie siku nzima kwenye TV. Alichofanya ni kugusa matatizo muhimu yanayowagusa watu kwa wakati huu. Suala la umeme na sukari litashughulikiwa na mawaziri husika.
 
Rais hawezi kuongea kila kitu ambacho watu wanataka. Akifanya hivyo basi inabidi atumie siku nzima kwenye TV. Alichofanya ni kugusa matatizo muhimu yanayowagusa watu kwa wakati huu. Suala la umeme na sukari litashughulikiwa na mawaziri husika.

Acha kutetea ujinga mkuu,hapo kuna tatizo gani ambalo kalitolea ufafanuzi?

Kama sio safari ya marekani na uoga wa uchaguzi wa Igunga...tusiwe wavivu hata kufikiri jamani kweli mtu mwenye akili timamu anaona kitu hapo kwenye hii hotuba? Kwa mapunguani sawa wataona mengi tu...shame on you!
 
Mkuu wa nchi unapoona anatoa Hotuba ya jumla jumla tu pasipo kuangalia masuala yanayowagusa karibia asilimia 95 ya watanzania ujue hapo kuna tatizo. Inakuwaje sasa hivi tuna tatizo kubwa la uchumi wa nchi kuwa dhaifu (kwa sababu ya bidhaa kupanda bei, sukari kukosekana kwa makusudi, ajali za magari kuongezeka kwa kasi huku zikiua watu lukuku na mengine mengi) lakini Rais yeye asiseme hata kidogo. Lakini akawiwa kusemea masuala madogo madogo ya uraia wa nchi mbili, tuzo na hata uchaguzi wa Igunga ambapo suala la usalama mfano huko Igunga polisi wangeweza kulisemea.

Hivi tunaposema kwamba, nchi yetu iko kwenye ombwe la uongozi tunakosea? Hivi watu kama akila Shy-Rose wanapohoji 'style' ya uongozi wa huyo jamaa tuseme anaonea mtu? Nakumbuka kampeni za mkuu huyo wa nchi mwaka 2005 alikuja na kauli mbiu ya 'maisha bora kwa kila mtanzania'; kauli ambayo ina uhusiano wa moja kwa moja na masuala ya hali ya uchumi wa jumla na hata wa mdogo ndani ya nchi yetu. Inakuwaje, tunapokuwa na hali hii ngumu leo, Rais huyo anyamaze tena kwenye fursa muhimu kama hiyo anayoipata kwa Taifa zima kukaa na kumsikiliza anawaambia nini?

Bado tunayo miaka minne hadi kufikia uchaguzi mkuu ujao, wasiwasi wangu ni kwamba, tutakuwa na hali gani wakati huo kiuchumi kama taifa endapo anayetuongoza anakuwa kipofu namna hiyo!
 
Kiongozi wetu hajui dira yake katika kutufanya tuwe na maisha bora aliyoyasema mwaka 2005. Yaani hajui cha kutuambia anaotuongoza na bila shaka sasa hatuwezi kufika tuendako badala yake kuishia shimoni! Inasikitisha na inauma sana sana.
 
Simhurumii rais kama ninavyowahurumia wasaidizi wake huko ikulu.
Wamedhamiria kwa dhati kabisa kuidhalilisha hii taasisi ya urais.
MUNGU WAREHEMU HAWA VIBWETERE!
.
 
I thought kutakuwa na news kama kawaida maana nilichelewa za saa mbili mara anakuja huyu mwanachana wa DICOTA nimezima link yangu cause I watch trrough online tool hapa ughaibuni naangalia nyimbo za wazaire sasa namuona Lady Meje anavyo nengua .
 
nafikiri kikwete anafikiri kwa kutumia umasaburi maana hajazungumzia hata wale wanafunzi ambao tumekosa mkopo kwa kwa kuwa bageti ni ndogo na badala yake wanawasomesha watu wa sayansi yeye anazungumzia igunga kwa kuwa ni jimbo la uchaguzi na wanajipanga kuiba kura na si kingine,uyu jamaa na kawambo wametuingiza choo cha kikwele jamani mimi hata cjui tutaishije huku chuoni kama hatuna mkopo hapa ni kurudi kijijini maanna kule ndiko kuna mapinduzi ya kweli kuliko dar.
 
Wewe kwenu ni wapi? kuna watanzania wangapi wanahitaji uraia wa nchi mbili? yaani umefurahishwa na nini wewe hapo? acheni kuwa wabinafsi. Kama aliwajibu akiwa huko ilitosha maana huko ndiyo kwenye hadhira iliyopaswa kusikia kuhusu mambo ya uraia wa nchi mbili sisi tulioko Bagamoyo,Mgeta,Chalinze na Mlandizi hii haikuwa habari ya kutuambia!


Kinyamana nahisi hujamuelewa atwinm52,samahani lakini.........What might be on his mind ni kwamba hii hotuba ya huyu mpangaji wa Magogoni sharobaro ni UPUPU Uliopitiliza kiasi kwamba alichokiona yeye ni uraia wa nchi 2 tu ambao haujashusha bei ya sukari wala mafuta ya taa ya watu wa Igunga ambao usafiri wao wa punda magufuli kasema unavunja sheria,yaani unagundia kumbe serikali yote ni kama wauza bar,ikifika saa 6 usiku kila mtu yupo stimu hata kama hanywi kilevi!!Nawasilisha.
 
huyu mzee sijamuelewa wajameni labda kwa aliyemuelewa atusaidie hotuba yake imetusaidia nini sisi wananchi
 
Back
Top Bottom