Hotuba ya Rais Karume kwenye Sherehe za Mapinduzi Zanzibar:The Best Ever!

Kwa wazanzibari na sio kwa wazanzibara

Kwa vile hakuna wahindi au mafisadi papa Zanzibar? Hao wakina Raza, Yasmin Aloo n.k. ni wazanzibara? Au mnataka kuwafanyia kama mnavyowafanyia wangazija! Ni hii sumu ya ubaguzi ndiyo inawarudisha nyuma na si machogo kama mnavyodai.

Amandla......
 
Kinachonihangaisha mimi kwenye sherehe hizi za Mapinduzi Daima ni itifaki inavyovurugwa. Rais wa JMT anaonekana mdogo kwa Rais wa SMZ! Hili liko hivi kwa muda mrefu tu tangu enzi za Mwalimu. Katiba ya JMT inawekwa kando kwenye sherehe hii!
 
CCM watamsaidia Kibaraka wao Mrema kupata jimbo analolitaka ili waoneshe sura mpya ya UPINZANI. Kwania akili za wana CCM tunazifahamu kwa muda mrefu sasa. Hayo yote Mrema anayoyasema yanatokana na mafunzo anayopewa na CCM.
 
Kinachonihangaisha mimi kwenye sherehe hizi za Mapinduzi Daima ni itifaki inavyovurugwa. Rais wa JMT anaonekana mdogo kwa Rais wa SMZ! Hili liko hivi kwa muda mrefu tu tangu enzi za Mwalimu. Katiba ya JMT inawekwa kando kwenye sherehe hii!
.
Zile Sherehe za Mapinduzi, sio sherehe za muungano, ni sherehe za ile nchi ilikuwa Zanzibar kabla ya muungano, kwa hiyo kihalali Tanzania is nothing, na Kikwete there is nobody, ila wamempa tuu heshima.

Vivyo hivyo Karume akija huku bara, he is nobody, ila tuu amepewa heshima ya recognition kiprotocali na ni waziri asiye na wizara maalum ili aingie cabnet ya huku, nasikia alisusaga hata kuja kwenye vikao hivi.

Kwa hili WildCard, you are damm right, how can The President of URT be second to rais wa kijisehemu cha nchi hiyo, ama nchi jina tuu iso dola?.
 
tukizungumzia kugombea nadhani ni dhana pana kidogo,inawezekana asigombee phyisically,lakini akawa ameshamteua mtu wa kuenforce kile anachoamini,na anachokitaka,hivyo uwepo wa Karume iwe nje au ndani katika kutekeleza muafaka wa Zanzibar na mambo mengineyo yahusuyo Zanzibar ni wa lazima,mpende msipende.
 
.
Zile Sherehe za Mapinduzi, sio sherehe za muungano, ni sherehe za ile nchi ilikuwa Zanzibar kabla ya muungano

Hapo naona Pasco unaendeleza ule ukoloni wako, kwa kusema Zanzibar si nchi tena baada ya Muungano.

Zanzibar ni nchi hata baada ya muungano...licha ya Pinda kusisitiza kama Zanzibar si nchi.

Taifa hili la Zanzibar lipo na wananchi wake bado tuko hai, na wala halitaondoka katika ardhi ya dunia.Licha ya ndoto za Pinda za kulifuta taifa hilo duniani.

Cheers...
 
Hapo naona Pasco unaendeleza ule ukoloni wako, kwa kusema Zanzibar si nchi tena baada ya Muungano.

Zanzibar ni nchi hata baada ya muungano...licha ya Pinda kusisitiza kama Zanzibar si nchi.

Taifa hili la Zanzibar lipo na wananchi wake bado tuko hai, na wala halitaondoka katika ardhi ya dunia.Licha ya ndoto za Pinda za kulifuta taifa hilo duniani.

Cheers...
Nchi hiyo haipo! si ndio ule mjadala ulivyoishia. Au kuna mwingine uliisha tofauti?
 
Tangu lini dhahabu, almasi n.k. vimekuwa vya watu wa bara peke yao? Mapato yake yote si yanakwenda kwenye wizara ya fedha ambayo ni ya muungano? Jeshi,mabalozi, vyuo vikuu si vyote vinahudumiwa kutokana na mapato hayo? Vyote hivi si vinatoa huduma kwa Zanzibar pia? Mahospitali nayo si yanahudumiwa kutokana na mapato hayo? Wazanzibari si wanapata huduma katika hizi hospitali kama mtanzania mwengine yeyote? Mimi ningeelewa kuwa hayo madhahabu, matanzanite, gesi, pamba, kahawa ni vya watu wa bara peke yao kama wangekuwa na wizara yao ya fedha na bajeti yao peke yao. Katika hali iliyopo sasa, si sahihi kusema kuwa hivyo ni vya bara. Wakitaka iwe hivyo basi tuwe na wizara ya fedha yetu kama ilivyo Zanzibar. Hapo nasi tutafaidika na hayo madini kama vile wenzetu wanavyofaidika na karafuu yao!

Amandla......

Ndugu Matumizi ya Serikali yanafanywa kwa kupitia Bajeti. Naomba nijibu maswali mawili
!. kwenye kikao kule Dodoma Waziri gani wa Wizara huwasilisha Bajeti ya Wizara za Zanzibar na tunajuwa kuwa Wizara ya Fedha haitumii fedha bila idhini ya Bunge.
2. Ule wakati wa Bajeti kule Baraza la Wawakilishi uliwahi kusikia lini kuwa Wizara ya Fedha ya Muungano imetowa Fedha za kugharamia hiyo Bajeti?


Naomba unipe majibu hayo ili tuendelee na hayo ya Mabalozi, Hospitali na vyuo.
 
[/LIST]Mimi kwa kawaida yangu ni kama tomaso huwa siwaamini sana wanasiasa
tatizo si kusema tatizo ni kutenda inapofika kwenye utekelezaji wako tayari hata kupinga walichosema jana yake,

Kwanza kauli yake 'hatogombea kwa mjibu wa katiba ' ni sawa, lakini ina maana ingekuwa si katiba alikuwa bado anataka kuendelea, je katiba ingasema vipindi kumi ina maana asingepisha wengine angekuwa raisi maisha? nina wasi wasi na kauli hiyo nasubiri vitendo.

Vile vile si mara ya kwanza kutoa hakikisho la uchaguzi huru na wa haki Zanzibar kila mara viongozi wamekuwa wakiimba hilo hata Komandoo Salimin ndio ulikuwa wimbo wake wa kila siku hatujasahau eti kila uchaguzi unapokuja wenyewe ni mashaidi wa vurugu za Zanzibar zikiongozwa na jenjewedi na polisi, sipingi kama kweli ana nia nzuri lakini nasubiri utekelezaji wake.

Rais Karume amesema mara ngapi kwamba kila Mzanzibar mwenye sifa ya kupiga kura ataandikishwa kila mwenye ZaID ataandikishwa matokeo yake nini masheha ndio wamekuwa waamuzi wa nani aandikishwe wakiongozwa na ma-DC yote yamekuwa yakifanyika kupingana na kauli za rais sijui ni kitu gani special alichofanya leo kinifanye niamini, ndo maana nimesema mimi ni kama tomaso.

Kuhusu suala la mafuta na gesi kuwa ni ya Zanzibar tu au la, hili sina uhakika nalo zaidi kwa sababu hata hayo mafuta ndo bado yanatafutwa hadi yatakapopatikana. Siwezi kwa sababu sijui yatapatikana wapi Unguja, Pemba, Mafia au Lindi sasa yakipatikana Mafia sijui wazanzibar watasema yao au yakipatikana baharini sijui mipaka ya Rep. of Tanzania inaishia wapi. Whatever the case kama dhahabu huwa inaenda hazina basi chochote kitakachopatikana kwenye mafuta na gesi kiende hazina, nafikiri hazina wana fomula ya mgawanyo wa kila kitu.


Nakubaliana nawe kuwa wanasiasa hawaaminiki lakini si huwa tunawachaguwa baada ya kusikiliza ahadi zao? Basi hatuna budi kuwasikiliza na pili kwani hapo nyuma si alikuwa muwazi kueleza tunayoyaona mabaya? Basi ni hatuwa kuwa sasa angalau anazungumza mazuri, natufarijike kidogo tukingojea hali halisi.

Ama hili la Mafuta na Gesi , kutopatikana au kupatikana muungwana hangojei matokeo kueleza msimamo wake na Zanzibar huo ni msimamo wao iwapo yatatoka Bara yatakuwa ya Bara peke yao na yakitoka Zanzibar yatakuwa yao peke yao, pana tabu hapo?
 
Nakubaliana nawe kuwa wanasiasa hawaaminiki lakini si huwa tunawachaguwa baada ya kusikiliza ahadi zao? Basi hatuna budi kuwasikiliza na pili kwani hapo nyuma si alikuwa muwazi kueleza tunayoyaona mabaya? Basi ni hatuwa kuwa sasa angalau anazungumza mazuri, natufarijike kidogo tukingojea hali halisi.

Ama hili la Mafuta na Gesi , kutopatikana au kupatikana muungwana hangojei matokeo kueleza msimamo wake na Zanzibar huo ni msimamo wao iwapo yatatoka Bara yatakuwa ya Bara peke yao na yakitoka Zanzibar yatakuwa yao peke yao, pana tabu hapo?

Wapi wazanzibari wametamka kuwa mafuta yakipatikana bara yawe ya bara peke yao na sio ya Muungano?

Amandla......
 
Ndugu Matumizi ya Serikali yanafanywa kwa kupitia Bajeti. Naomba nijibu maswali mawili
!. kwenye kikao kule Dodoma Waziri gani wa Wizara huwasilisha Bajeti ya Wizara za Zanzibar na tunajuwa kuwa Wizara ya Fedha haitumii fedha bila idhini ya Bunge.
2. Ule wakati wa Bajeti kule Baraza la Wawakilishi uliwahi kusikia lini kuwa Wizara ya Fedha ya Muungano imetowa Fedha za kugharamia hiyo Bajeti?


Naomba unipe majibu hayo ili tuendelee na hayo ya Mabalozi, Hospitali na vyuo.

Na wewe nawe unasema nini tena? Wote tunajua kuwa waziri wa SMZ hana nafasi katika bunge la JMT. Wote tunajua bajeti ya wizara za ulinzi, mambo ya nje zinapitishwa na bunge la JMT na si Baraza la mapinduzi. Hizi wizara zinasimamia masuala ya Muungano na si bara peke yake. Lini tumeambiwa na waziri wa fedha zanzibar kuwa mchango wa SMZ kwenye wizara hizi ni kiasi fulani?

Serikali ya JMT haitoi fedha moja kwa moja kwenye bajeti ya SMZ bali kwa njia mbadala. Kwa mfano kwa miaka mingi serikali ya JMT iliibeba serikali ya SMZ kwa kuruhusu watu waingize bidhaa kupitia Zanziba bila kulipia ushuru unaotakiwa. Serikali ya JMT kwa kupitia shirika lake la Tanesco imekuwa iki-subsidize bei ya umeme kwa wazanzibari. Kwa kuwaruhusu wazanzibari kutumia hospitali, shule n.k. ambazo si za Muungano, serikali ya JMT nawa-subsidize wazanzibari. Serikali ya JMT kwa kutoa mikopo kwa serikali ya SMZ inapokwama inawasaidia wazanzibari maana tunajua kuwa hata siku moja hamtakuja lipa.

Mnabebwa sana na serikali ya JMT na bahati mbaya mnajisahau na kuona sasa ni haki yenu!

Amandla.....
 
By the way hotuba kamili ni hii:

Edit:
Removed the text and put it in pdf...reason text too long.
 

Attachments

  • hotuba.pdf
    125 KB · Views: 169
Naona hata wanachama na wapenzi wa CUF wameunga mkono muafaka huo, kama inavyoonekana kwenye picha hii, ambapo wanacuf wakipita mbele ya Rais Karume...

i1415_Cufon46yrsofSMZ.JPG


Picha kwa hisani ya Father Kidevu

Kazi ipo na huu muafaka bandia kwa pande zote mbili.Hakuna muafaka afrika ni unafiki mtupu!siku zote mlikuwa wapi kufanya huo muafaka?why now Karibu na uchaguzi Mkuu?
 
Nchi hiyo haipo! si ndio ule mjadala ulivyoishia. Au kuna mwingine uliisha tofauti?

Lini nchi ya Zanzibar imekufa?Nyie acheni mchezo wenu wa kitoto huo, Zanzibar ni moja ya nchi kongwe barani Afrika.Zanzibar ni nchi ipo tokea hata hicho kijinchi chenu cha Tanganyika, musianze dharau zenu.

Nchi ya Zanzibar ipo, na bendera yake itaendelea kupepea milelele.Nchi iliyofutwa na kupotea ni Tanganyika tuu, lakini Zanzibar bado ipo.
 
Nimefarijika kuwa akina Tomaso tuko wengi. Hata siku moja siwezi kumuamini mwanasiasa. Siasa ni kusema kile watu wanataka kusikia wakati huo hata kama kitu hicho unajua ni ndoto za alinacha. Kwangu mimi sikiliza hotuba za wanasiasa wakati mwingine ni sawa na kuangalia watoto wanaocheza kidari po! Nothing is real and genuine! Tusubiri hadi Oct tuone.
Yes, ni ngumu sana kuwaamini wana siasa maana wameamua kusema lolote lile tunalotaka kulisikia bila kujari litakuwa na matatizo gani mbele ya safari.
 
Zanzibar si nchi piga ua PM alishamaliza mtapiga kelele sana hata rais wa Zanzibar ndani ya muungano is a ceremonial president tu akija ndani ya muungano ni sawa kama RC. Tatizo la waZenji ni wabishi huwa hawataki kuelewa mambo waliomba wimbo wao wakapewa wakaomba bendera yao wakapewa rais wao apigiwe mizinga haya nasikia hata timu ya taifa eti wanataka kama bara itatoa wacheza 10 na wao watoe 10 hata kama hawana uwezo ajabu kweli kweli.

Ubishi wenu utawamaliza kwanza wenyewe kwa wenyewe hampendani mnajiita kuna waunguja na wapemba sasa tukiwaacha si mtamalizana hata Mwalimu Nyerere kuna wakati alisema angekuwa na uwezo angekisukuma kisiwa hiki kiende mbali baharini maana kimemchosha kila siku kuomba kitu kipya na yeye alichoka nasi kuna siku tutachoka kuwabeba.
 
Wapi wazanzibari wametamka kuwa mafuta yakipatikana bara yawe ya bara peke yao na sio ya Muungano?

Amandla......
Poleni sana. Tatizo ni kuwa hamtaki kuuulewa huu mfumo wa Muungano wetu wenyewe. Zanzibar wanataka mafuta yakionekana Zanzibar yawe ni ya Zanzibar (ambayo ipo kwa mujibu wa mfumo). Na yakionekana Mafia au Songea au Biharamulo hayo ni ya Tanzania-kwa sababu hakuna kitu Bara au Tanganyika. Hivyo vimefutwa. Hamtaki kuelewa tu jamani?
 
Mr.Froasty said:
Hapa unaonekana kuonesha kama huu ni ubaguzi, lakini hii hoja haina mshiko.Chukulia mfano Hong-Kong na wachina wa kawaida.Ukiwa wewe ni mchina wa kawaida kuingia Hong-Kong ni sawa na unakwenda Europe, ni lazima ufanyiwe control za immigration na kila kitu.

Lakini alieko Hong-Kong, anaingia sehemu zengine za China kama kawaida.

Sasa hii sio bahati mbaya, kwani wakiachiwa hao wachina wote watakimbilia Hong-Kong na athari zake zinajulikana.

Sasa na Tanganyika kuwekewa vizingiti Zanzibar ni sawa kabisa, kwani watanganyika wote hawawezi kuingia visiwani humo.Ni sehemu ndogo, na ardhi yake ni ndogo.Watanganyika 0.5Mil tuu wahamie Zanzibar, tayari hiko ni kishindo na visiwani huwezi hata kujamba.


Aidha kwa suala la dhahabu na madini mengine Zanzibar inanufaika vipi?Mie sioni jinsi wanavyonufaika.Hii ni general case ya muungano kuwa unanufaisha Tanganyika tuu na kuiwekea guu Zanzibar isiende mbele wala isifurukute.Bajeti yote ya Tanzania ni kuhusiana na Tanganyika tuu, sijawahi kumsikia JK akisema bajeti hii ni kujengea barabara kule Msuka (North-Pemba).

Sasa FUTA wacha wazenji wale peke yao acheni uroho, kuleni Tanzanite....hamushibi?

Mr.Froasty,

..tunachotaka ni usawa ktk muungano huu. kama suala hilo haliwezekani baina ya Tanganyika na Zenj ni bora Muungano uvunjwe.

..ninachosema mimi ni kwamba Wazenj wawekewe masharti yaleyale wanayokumbana nayo Watanganyika wanapofika Zenj.

..nakumbuka majuzi hapa kuliibuka suala la vibali vya kazi Zenj. ilielekezwa kwamba Watanganyika watakuwa-treated kama raia wengine wa kigeni ktk masuala masuala ya kazi Zenj. yaani Mtanganyika anakuwa hana tofauti na Msudan,Mnigeria etc.

..kama ni mashirikiano ktk muungano, basi yasielemee kwa wa Tanganyika kama ilivyo sasa hivi.

..kwa mfano: kama mnadai Zenj ni ndogo sana, na uwezo wake ni kupokea wahamiaji 1000 tu kwa mwaka toka Tanganyika, basi Tanganyika nayo isipokee Wazenj zaidi ya 1000 kwa mwaka.

..kwasasa hivi Mzenj akiingia Tanganyika anakuwa na haki zote kana kwamba amezaliwa upande huu. lakini hilo haliwezekani kwa Watanganyika kwanini? kwanini hakuna usawa ktk muungano huu?

..pia si kweli kwamba Wazenj hawafaidiki na madini na rasilimali nyingine zinazopatikana huku Tanganyika. Wazenj wana uwezo wa kumiliki ardhi huku Tanganyika. kuna maeneo ktk miji ya Tanganyika ambako Wazenj wana majumba makubwa makubwa, mashamba makubwa, biashara, na hakuna anayewasumbua.

..pia Wazenj wanayo haki ya kumiliki machimbo ya madini[dhahabu,tanzanite,ruby,... yoyote yale yanayopatikana Tanganyika. sasa hii habari kwamba waZenj hawafaidiki na "dhahabu" za Tanganyika yanatoka wapi?

NB:

..kuhusu suala la bajeti ni kweli huwezi kusikia suala la barabara za Zenj ktk bunge la muungano. hii ni kwasababu suala la barabara siyo la muungano. lakini inaposomwa bajeti ya wizara kama ulinzi, au ile ya mambo ya ndani, basi Zenj iko-included humo. hapa ni suala la kuelewa tu wizara zipi zinashughulika na masuala ya muungano.

..nilitegemea ungekwenda mbali zaidi na kuuliza kwanini wabunge toka Zenj huhudhuria na hupokea posho za vikao vya bunge vinavyozungumzia masuala yasiyo ya muungano?
 
Back
Top Bottom