Hotuba ya Rais ililenga kukataza wateuliwa na watendaji kuacha kuanza kutafuta urais wafanye kazi na hatanii

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,911
51,902
Raisi akifikia muhula wake wa pili kulikuwa na mazoea ya wabunge na mawaziri kuanza kampeni mitandaoni nk na kutwa kushindana kuunda mitandao ya kujenga makundi ya kampeni ya kuutaka uraisi badala ya kufanya kazi

Raisi Hilo kaonya watu wafanye kazi na ninavyomjua hatanii he mean business

Kipindi Cha pili ambacho huwa Cha mwisho Cha utawala wa Raisi wa awamu husika viongozi wengi wa serikali na taasisi zake kulikuwa na tabia ya kujiunga mikundi ya watarajia kutia Nia za kugombea uraisi kazi zikawa haziendi kutwa Ni kujinadi Ohhh fulani ndie anafaa na vikao visivyoisha vya kampeni za chinichini na kelele vyombo vya habari na mitandaoni

Raisi Magufuli hatanii na atatumbua kweli wateuliwa wote chapeni kazi no kazi tu Hakuna kingine sababu lengo lake anataka kuachia mchapa kazi hasa sio domokaya anayeota Ikulu tu wakati performance Ni zero ndio maana kasisitiza performance na hatanii
Wabunge na mawaziri na wateuliwa chapeni kazi hasa huko mbele mchapa kazi Sana ndie aweza pokea kijiti mbeleni awe wa bara au Zanzibar

Tamanio lake sio kuacha madaraka kwa genge la wapiga porojo na wasio perform anataka akabidhi kijiti kwa mchapa kazi hasa ambaye anatilia maanani maslahi ya walio wengi

Hivyo wabunge , mawaziri na watendaji chapeni kazi
 
Huyu jamaa ajiandae kisaikolojia, muda wake unakwenda kuisha na anamalizia kwa vikwazo vitakavyo haribu mambo yote ya maendeleo aliofanya.

Mpaka anamaliza muda wake Cement 35,000/=, Petrol Kwa Lite 10,000/=, Sukari 5,000/=, Chumvi 2,000/=.

Rais wa wanyonge, sasa baada ya kumaliza muda wake "Ole Wao", nasema "Ole wao wanyonge" tusisikie wanamtukana au kumtolea maneno ya shombo. Maana alikua kwaajili yao kuwanyonga kabisa.
 
Jamaa inamuuma sana kuona anaenda kumaliza muda wake!
Wala alichofanya Ni kuwaambia Live kuwa Kama mtu anategemea kupokea kijiti kigezo kikuu namba moja Ni Performance.How you perform or you performed kwenye nafasi yako uliyopewa ili kila anayeiota akumbuke hilo kwanza na ajifanyie self assessment mwenyewe
 
Awamu hii Raisi ajaye atapokea kijiti kwa performance sio mavyeti aliyojaza kabatini au uwezo wa kuongea Ni performance tu hivyo kila mteuliwa au mtendaji awe mbunge,waziri nk a perform hasa.

Zanzibar Rais Mwinyi kaonyesha njia kamchagua aliyekuwa mkuu wa wilaya kijana mchapa kazi hasa kuwa makamu wa Raisi wa Zanzibar hivyo huko mbele haiwezi kuwa ajabu hata mkuu wa wilaya au mkoa mchapakazi kupewa kijiti Cha ugombea uraisi.Magufuli na Mwinyi wameanza kuonyesha njia kuwa viongozi wasiishi kwa mazoea wachape kazi hasa kwenye nafasi walizopewa performance ndio itakuwa mwamuzi.
 
Wala alichofanya Ni kuwaambia Live kuwa Kama mtu anategemea kupokea kijiti kigezo kikuu namba moja Ni Performance.How you perform or you performed kwenye nafasi yako uliyopewa ili kila anayeiota akumbuke hilo kwanza na ajifanyie self assessment mwenyewe
Hiyo siyo kazi yake,NEC ndio watakaoamua!Anaongea utafikiri yeye ndiye anayeteua na wajumbe wengine ni picha tu!
 
Nachompendea Raisi Magufuli ni kwamba msukuma huyu anaakili nyingi 'nadhani ni matokeo ya kula samaki sato' na ujasusi anaujua na anautumia sana kwenye uongozi wake

Mpaka sasa naamini kabisa:

Moja; anajua wanasiasa bomu, wasiofaa kuwa Raisi wa nchi japo wanautamani uraisi ama wapambe wao wanatamani wawe Raisi wa nchi

Mbili; anajua wanasiasa waliojianda na wanaendelea kujiandaa kufukuzia uraisi wa nchi, kwa kukujenga mtandao (wa viongozi wastaafu, wajumbe*, viongozi wa dini)

*Mtandao wa wajumbe wa NEKII, na mtandao wa wajumbe wa MKUTANO HIGH
 
Moja; anajua wanasiasa bomu, wasiofaa kuwa Raisi wa nchi japo wanautamani uraisi ama wapambe wao wanatamani wawe Raisi wa nchi

Mbili; anajua wanasiasa waliojianda na wanaendelea kujiandaa kufukuzia uraisi wa nchi, kwa kukujenga mtandao (wa viongozi wastaafu, wajumbe, viongozi wa dini)
Ni kweli ndio maana kawawashia taa kubwa za hazard za spidi ya Gari kuwa nawaona hapo mlipo!!! Wawe chamani ,serikalini ,kwenye taasisi zake, bungeni , mahakamani au nje ya hivyo vyombo!!

Mwenye maskio askie alichosema na anamaanisha hatanii na Hana mpango wa kutania
 
Dk ,Magufuli kaanza mapema kuwaonya wale wapiga filimbi wa hamelini wajipigia tarumbeta au wapigia tarumbeta wengine na kuunda makundi ya kuchafuana kuwa nafasi hiyo haipo awamu hii

Wewe chapa kazi uwe mbunge,mteuliwa wa raisi ,diwani au mtendaji wa srikali au taasisi zakePerformance yako kwenye nafasi yako ndio vitaamua mwisho wa siku iwe kwenye nafasi uliyowahi kupewa au uliyonayo sasa

Awamu hii ya Mgufuli haitaki makelele inataka performance
 
Back
Top Bottom