Hotuba ya Leo ya Mh Rais Dr John Pombe Magufuli unaweza kwenda kuombea mkopo World Bank bila Riba

Frey Cosseny

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
1,984
1,405
Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ambaye pia ni Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli amesema nchi za kiafrika si maasikini hivyo ziache kujitangaza kuwa ni duni mbele ya mataifa mengine.

“Tusikubali kusafirisha tu malighafi nje ya Afrika, hii inaatufanya tuwe tunasafirisha ajira. Nchi zetu si masikini, narudia tena nchi zetu si masikini tunao utajiri wa kutosha kwenye madini, mafuta na ardhi yenye rutuba .


Vitu vyote vinavyotufanya tuwe matajiri tunavyo, kwanini tushindwe kupiga hatua,” alisema Rais Magufuli.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo, Rais Magufuli amesema mbali ya kuwa na rasilimali nyingi lakini bado Afrika inalalamika hali duni ya kiuchumi.

Rais Magufuli amesema Tunaagiza sukari, magari na mafuta katika nchi za mbali huku tukijua baadhi ya mataifa ya SADC yanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nafuu. Ndio maana katika mwaka wangu wa uongozi nimeamua kuongozwa na kaulimbiu ya mazingira bora ya viwanda, ufanyaji biashara na kutengeneza ajira.

Vievile, fursa nyingi za kibiashara zinapelekwa katika mataifa ya mbali huku baadhi ya nchi zinazozalisha bidhaa nzuri ikiwemo magari na bidhaa nyingine za viwanda zikiachwa mbali ya kuwa na bidhaa bora na zilizo karibu.

Aidha, Rais Magufuli aliigeukia Sekretarieti ya SADC na kuitaka ieleze kwanini uchumi katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo unashindwa kufikia viwango vya kukua. Kwanini kwa miaka 10 lengo la kuondokana na tatizo la kiuchumi halijafikiwa.

Awali Rais Magufuli akielezea changamoto zinazoikabili jumuiya hiyo na kushindwa kufikia baadhi ya makubaliano, Rais Magufuli alisema changamoto ya kwanza ni vurugu za kisiasa, kutokamilika ahadi za kubadili uchumi na ukosefu wa taarifa za fursa katika nchi wanachama.

“Bado hatujafanikiwa katika ukuaji wa uchumi, niseme kweli bado tunasuasua. Na tusipibadilika hatutaweza kufanikiwa katu. Bado tupo nyuma katika lengo letu la kiuchumi, uhaba wa taarifa unasababisha tunashindwa kujua wapi pa kuuza bidhaa zetu,” alisema Dr John Pombe Magufuli

FB_IMG_1566046229264.jpeg
 
Mimi hizi tenzi zenu toka nakua naskiaga hii nchi sio maskini..labda kama ww ndo umesikia jana!...fanyeni vitu kwa vitendo sio mingonjera yenu tumeichoka!Eti nchi hii sio maskini🙂! ni maskn lakutupwa!maana viongozi wanajilimbikizia mali kwao wanatuacha makapuku tunakufa kias hatuna uwezo hata wa kujitibu😏😏! Nyau nyie!
 
Data.hupikwa to look good on paper.

Hujiulizi vita vya Trump na China kuhusu ushuru wa bidhaa kwa sababu tu Trump kaweka.10% tariff ya import za China, sasa zamani ilikuwa iko % ngapi? Sisi kwetu karibu kila kitu ni 25% kwenda juu na hatuzalishi.

Ukweli ni kwamba Tariffs (kodi) zinawekwa juu sana ili mabeberu waone tunakusanya kodi kubwa on paper ili tukopesheke. Lakini kiuhalisia bidhaa ni za thamani ya chini na hatukopesheki kwa sababu.uwezo wa kulipa hatuna. Na hiyo ndio tabia ya wafanyabiashara wengi wa Tanzania kupika data.za kuombea mikopo.
 
Mzee bado anatatizo kwenye matamshi nimemsikia

(1) Neno Leaders anatamka kama "Readers",
(2)Leadership anatamka Readership
(3) Elections kuna mahali kasema "(E)rections"
(4) Kuna sehemu anapaswa atamke "s" anaiacha
(5)Brother anatamka Blother

Bado inabidi aendelee kujipiga msasa, improvement inaanza kuonekanaonekana kwa mbali
 
Yew,o zOTE="Missile of the Nation, post: 32528246, member: 490108"]
Mzee bado anatatizo kwenye matamshi nimemsikia

(1) Neno Leaders anatamka kama "Readers",
(2)Leadership anatamka Readership
(3) Elections kuna mahali kasema "(E)rections"
(4) Kuna sehemu anapaswa atamke "s" anaiacha
(5)Brother anatamka Blother

Bado inabidi aendelee kujipiga msasa, improvement inaanza kuonekanaonekana kwa mbali
[/QUOTE]
Uwezo wa mtanzania katika kuchambua hakika ni mkubwa.
 
Mzee bado anatatizo kwenye matamshi nimemsikia

(1) Neno Leaders anatamka kama "Readers",
(2)Leadership anatamka Readership
(3) Elections kuna mahali kasema "(E)rections"
(4) Kuna sehemu anapaswa atamke "s" anaiacha
(5)Brother anatamka Blother

Bado inabidi aendelee kujipiga msasa, improvement inaanza kuonekanaonekana kwa mbali
Mkuu suala la lugha mi sioni kama ni ishu sana. Mfano rais wa Comoro kifaransa chake ni cha kawaida sana kulinganisha na cha rais wa Madagascar lakini haimaanishi kwamba raid wa Madagascar anamzidi wa Comoro kiutendaji.
Kujua lugha ni suala dogo sana kitu muhimu in kuwa na maono na kuweka juhudi kuyafikia maono yako.
 
Kuandikiwa na kusoma nayo ni improvement kwa kweli
Mzee bado anatatizo kwenye matamshi nimemsikia

(1) Neno Leaders anatamka kama "Readers",
(2)Leadership anatamka Readership
(3) Elections kuna mahali kasema "(E)rections"
(4) Kuna sehemu anapaswa atamke "s" anaiacha
(5)Brother anatamka Blother

Bado inabidi aendelee kujipiga msasa, improvement inaanza kuonekanaonekana kwa mbali
 
Huyu Katibu Mtendaji wao Mama Stergomena L. Tax huu mwaka wa sita yuko hapo hapo. Zije sura mpya aisee maana ni kama vile anaenda kazini tu kama routine lakini sio kutatuta changamoto mbali mbali ambazo haziishi kila leo.
 
Sisi bado mno kiuchumi na kama hatuwezi kupambana kushusha Production Cost hatuendi popote.

Sukari inatoka nchi ya mbali kama El Salvador jirani kabisa na Mexico mtu wa Bukoba anaipata kwa bei ndogo kuliko ya mlangoni kwake Kagera Sugar. Incredible.

Sisi ni blaa blaa tu za kisiasa hatuna lolote.
 
Mkuu suala la lugha mi sioni kama ni ishu sana. Mfano rais wa Comoro kifaransa chake ni cha kawaida sana kulinganisha na cha rais wa Madagascar lakini haimaanishi kwamba raid wa Madagascar anamzidi wa Comoro kiutendaji.
Kujua lugha ni suala dogo sana kitu muhimu in kuwa na maono na kuweka juhudi kuyafikia maono yako.

Huyo rais wa Madagascar amesoma kwa kiwango cha PhD kwa kutumia lugha ya kifaransa katika masomo yake?
 
Back
Top Bottom