Makaro
JF-Expert Member
- Jan 9, 2013
- 615
- 136
Hakuna siku ktk maisha yangu nimeumia kama leo, moyo umesinyaa, nafsi imedhoofika, mwili umepauka, dhamira imenyauka.
Nimetambua ukweli ni mchungu, ukakasi wake unapenya mpk mifupani.
Huyu ndiye kiongozi pekee niliyeamini/ninayeamini ndiye atatusuuza mioyo yetu.
Slaa utadumu kwenye moyo wangu, siwezi kamwe kupuuza kitokachp kinywani mwangu. Nitakua mnafiki wa kwanza kunyanyua ulimi wangu na kukutusi.
Naumia zaidi waTZ tunaingia miaka mingine mi5 ya maumivu.
Mungu atuoneshe chaguo sahihi, Mungu atupe nguvu.
Mbowe na genge lako, mlaaniwe hata kizazi cha 7.
Matusi yote mliokuwa mnampa, leo amekuwa mungu wenu. Mabadiliko mbele kwa mbele. Wananchi wameshaamua