Hotuba ya Bajeti wizara ya Nishati na madini 2017/2018

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,571
A. UTANGULIZI

  1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea, kujadili na kupitisha mpango na makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18.
  2. Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema sisi Waheshimiwa Wabunge wote na hivyo kutuwezesha kuendelea na utekelezaji wa majukumu yetu ya kitaifa ndani na nje ya Bunge. Kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu, Bunge limeendelea kutekeleza majukumu yake ya kikatiba likiwemo la kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  3. Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kuwapongeza kwa dhati viongozi wetu wa kitaifa kwa jinsi wanavyojituma katika kutatua matatizo na changamoto mbalimbali za Taifa letu na hatimaye kuwaletea wananchi maendeleo. Viongozi hao wameendelea kutoa miongozo ambayo kila mara imekuwa ikilenga kuwaondolea wananchi kero mbalimbali katika maeneo yao. Dhamira hii imedhihirika wazi kwa jinsi Serikali ya Awamu ya Tano inavyoshughulikia masuala yenye maslahi ya kitaifa yakiwemo ya vita dhidi ya rushwa, madawa ya kulevya, ubadhirifu wa mali za Umma, malipo hewa pamoja na kurudisha uwajibikaji Serikalini.
  4. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongeza Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali yake jinsi anavyochukua hatua za kusimamia na kulinda rasilimali za Taifa hasa madini.
  5. Mheshimiwa Spika, naomba pia kumpongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kazi yake nzuri anayoendelea kuifanya tangu alipoteuliwa. Aidha, nampongeza Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) kwa jinsi anavyoendelea kusimamia kwa karibu shughuli za Serikali tangu Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani. Ni wazi kuwa Viongozi wetu hao wa kitaifa kwa kipindi kifupi walichokaa madarakani wamefanya kazi nzuri na kubwa kwa kutoa na kutekeleza miongozo makini ya kulisaidia Taifa letu. Tuwaombee wote kwa Mwenyezi Mungu ili waendelee na kasi hiyo ambayo imekuwa ni chachu ya mabadiliko katika nyanja mbalimbali na hatimaye nchi yetu iweze kupiga hatua za kimaendeleo kwa kasi kubwa zaidi.
>>Soma Zaidi>>
 
Si ndio inasemekana alikuwa mwanasheria wa Tanesco..nimewaza tu je alisaini mikataba au alishauri nini kuhusu kuibiwa?
KUIBIWATANESCO ; AU MADINI, KUNA MWANASHERIA WA WIZARA , TMAAA NA AG . NDO ANAIDHINISHA
 
Si ndio inasemekana alikuwa mwanasheria wa Tanesco..nimewaza tu je alisaini mikataba au alishauri nini kuhusu kuibiwa?
Hajawai kuwa mwanasheria wa TANESCO alikua mwanasheria wa Wizara, na mikataba hua inasainiwa na Waziri kwa kusimamiwa na Mwanasheria wa Serikali.
Kwahiyo wakubwa wakiamua ww huku chini huna la kufanya mkuu
 
Waziri wa Viwanda , Biasharana Uwekezaji, Charles Mwijage leo Alhamisi amevaa viatu vya Profesa Sospeter Muhongo kwa kusoma bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini bungeni.

Mwijage anavaa viatu hivyo baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa Profesa Muhongo kama waziri wa wizara hiyo kutokana na kushindwa kusimamia vizuri wizara.

Hilo lilitokea baada ya Rais Magufuli kupokea ripoti ya kamati ya kwanza ya kuchunguza makontena 277 ya mchanga wa madini yaliyozuiliwa kusafirishwa kugundua kuwa kuna madini mengi yanapitishwa kwenye mchanga huo.

Waziri Mwijage ambaye katika Serikali ya Awamu ya Nne aliwahi kuwa Naibu Waziri Katika Wizara ya Nishati na Madini atakuwa na kazi nzito katika bajeti hii kutokana na sakata la mchanga huo ambao wabunge wamekuwa na maoni tofauti tangu Rais Magufuli alipochukua uamuzi wa kuzuia makontena hayo.

Chanzo: Mwananchi
1a5f0aa3333475b9ebb293e28f32a42c.jpg
 
Ka sio maneno yenu mengi, hata miye ningeenda kusoma tu. Si imeandikwa kiswahili?? Kusoma sio kitu, tatizo kutendewa kazi bajeti yenyewe. Tz kila kitu chaweza bakwa tu. Kama unaomba 100 ukapewa 23 tu si ubakaji huo ni nini na huku unaambiwa umetenda chini yaufanisi.
 
Mwijage atakimbia mjadala, we subili utaona!!! Kuna makombala makalimakali mithiri yayale ya Korea kas! Hatayahimili huyu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom