TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,914
- 23,075
Hii nayo ni kazi yako ,si kila kitu akimalize yule aliyekupatia hotuba ya Mwalimu Nyerere , kutukumbusha watu muhimu waliolisaidia Taifa letu Tanzania. Tusinung'unike tu tusaidiane pale tunapoona mapumgufu...na askari waliokwenda mstari wa mbele tuwaiteje?
..kuna vijana waliomaliza form 6 wakaenda jkt na kutoka huko wakaenda vitani.
..wapo makamanda walioongoza vita hiyo. Je, tunawakumbuka?
..kwa mfano yuko Gen.Tumainieli Kiwelu ambaye alipewa jukumu la ku-mobilize jeshi la kutekeleza operation ya kuondoa majeshi ya Amini ktl ardhi yetu. Je, tunamuezi? Je, kuna ipo kambi ya jeshi iliyopewa jina lake?
..yuko Brig.Ahmed Kitete [ rip]ambaye vitabu mbalimbali vinamtaja kama operation commander wa zoezi la kuyafukuza majeshi ya uvamizi. Je, tunamuenzi?
..yupo Kanali Rajabu aliyeongoza kikosi cha wahandisi kujenga daraja la muda ili askari wetu na vifaa vyao wavuke mto Kagera. Iddi Amini alilipua na kuvunja daraja la mto Kagera. Je, tuna kumbukumbu naye?
..Kwa ujumla, kuna kumbukumbu yoyote kwa ajili ya tukio hili? Tunawakumbuka waliopoteza maisha? Tunawatunza mashujaa waliorudi, haswa waliopata vilema?