Hoteli ya Sugu: Wafanyakazi wa Serikali wanavyoisaliti Serikali ya Magufuli

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,880
13,164
Hili sakata la kutaka kufunga Hoteli ya Sugu huko Mbeya limeleta hisia nyingi.

Lakini baya zaidi ni lile la the dark side ya watu fulani ndani ya Serikali.

Serikali inaendeshwa na watu.

Na watu hao maafisa ndiyo waliotaka watumie mgongo wa Serikali kubomoa Hoteli hiyo.

Kwa wafanyabiashara tunajua kuna watu-maafisa, wenye mamlaka na wana wivu, au kinyongo na maendeleo ya wananchi, hasa wafanya biashara.

Nimeambiwa huko Mbeya kuna viongozi wa ajabu sana. Pengine Magufuli atembelee Mbeya kujionea vioja cha maafisa au viongozi wake.

Miaka ya 2017 uwekezaji wa maparachichi ulitiwa misukosuko. Mwekezaji mzalendo wa ufugaji samaki kule Tukuyu-Kiwira badala ya Serikali kumtia moyo, kupitia DED wakamfungia mradi karibia miaka miwili bila sababu za msingi. Waliposikia Magufuli anatembelea Mkoa wa Mbeya, wakamfungulia mradi.

Hili ni kielelezo cha watu ndani ya Serikali wenye roho mbaya, na ni mbaya kwa wawekezaji.

Watu wa aina hii wako wengi na idara tofauti kuanzia ma DED, TRA, NEMC, hata baadhi wakuu wa Wilaya.

Hili sakata la Hoteli ya Sugu ni kielelezo tosha cha Watu wasioitakia mema serikali ya Awamu ya Tano.

Maafisa hawa wana msimamo wa kukomoa wafanyabiashara au wawekezaji.

Serikali kupitia Rais anasema hili, wakati baadhi ya maafisa wa Serikali wanatekeleza matakwa yao.

Rais Magufuli kwa kweli inabidi aelezwe tu kwamba kuna wafanyakazi/maofisa ndani ya Serikali yake wanamhujumu.
 
"Na watu hao maafisa ndiyo waliotaka nitumie mgongo wa Serikali kubomoa Hoteli hiyo."

Hebu funguka kidogo hapa, nini kinajiri?
 
Sugu aliwadharau sana watendaji sasa ajipande kwenye kodi maana hawatamuacha salama ajaiita rais huku analialia kushukuru rais og.

Aliifanya mbeya yake upepo umegeuka atulie sindano iingie
Wewe mbuzi kweli kweli, lini Sugu alisimamia serikali hadi watumishi wamuogope? Umesahau mlivyokuwa mnamsweka ndani kila siku hadi mkamfunga jela miezi sita?
 
Sugu aliwadharau sana watendaji sasa ajipande kwenye kodi maana hawatamuacha salama ajaiita rais huku analialia kushukuru rais og.

Aliifanya mbeya yake upepo umegeuka atulie sindano iingie
Hayo ni maneno ya kijinga.
Na inaelekea wewe ni afisa wa Serikali. Serikali hapiashwi kuendeshwa kwa muhali wa mtu kujiamulia na kwa kujikomba.
Zifuatwe taratibu tu.
 
Hili sakata la kutaka kufunga Hoteli ya Sugu huko Mbeya limeleta hisia nyingi.

Lakini baya zaidi ni lile la the dark side ya watu fulani ndani ya Serikali. Serikali inaendeshwa na watu. Na watu hao maafisa ndiyo waliotaka nitumie mgongo wa Serikali kubomoa Hoteli hiyo....

Huo Mchongo una mkono wa "FIVE AGAIN" sema ndio hivyo umebuma.
 
Wewe mwabwa koko kweli hujui mbunge anasimamia halmashauri kupitia nafasi yake kama diwani kwenye halmashauri .wewe ni kilaza uliyesoma ujinga
Wewe mbuzi kweli kweli, lini Sugu alisimamia serikali hadi watumishi wamuogope? Umesahau mlivyokuwa mnamsweka ndani kila siku hadi mkamfunga jela miezi sita?
 
Hayo ni maneno ya kijinga.
Na inaelekea wewe ni afisa wa Serikali.
Serikali hapiashwi kuendeshwa kwa muhali wa mtu kujiamulia na kwa kujikomba.
Zifuatwe taratibu tu.
Ndio utaratibu unaanza na sugu mwambie ajipange si alisema jpm ni mtu mwoga sasa jpm anamsamehe na yeye anashukuru ila sisi kimyakimya tunadeal naye
 
Sugu aliwadharau sana watendaji sasa ajipande kwenye kodi maana hawatamuacha salama ajaiita rais huku analialia kushukuru rais og.

Aliifanya mbeya yake upepo umegeuka atulie sindano iingie
Tukijadili wafanyakazi wa Serikali mlivyo na roho mbaya dhidi ya wafanya biashara wazalendo.

Mnaghushi kodi na tozo ili kutengeneza mazingira ya rushwa.

Rais Magufuli anapaswa kuwaelewa.
 
Sugu aliwadharau sana watendaji sasa ajipande kwenye kodi maana hawatamuacha salama ajaiita rais huku analialia kushukuru rais og.

Aliifanya mbeya yake upepo umegeuka atulie sindano iingie
Nyie ndio walewale nyie wenye roho za kichawi.

Mithali : Mlango 24
17 Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

Mika : Mlango 7
8 Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, BWANA atakuwa nuru kwangu.
 
Nyie ndio walewale nyie wenye roho za kichawi.

Mithali : Mlango 24
17 Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
Hii inaitwa kimyakimya mpaka sugu akimbilie Canada
 
Mwezako sugu alikuwa nashukuru rais kuwa yeye amefuata sheria
Mjinga ni wewe ambaye hujui kuwa kwenye utawala huu hakuna sheria inayofuatwa! Hata hao wabunge ni vikaragosi vya serikali!
 
Back
Top Bottom