Hoteli ya Mgonja? Parrot Hotel

Lifer

Member
Jan 28, 2007
36
27
Kibao mbele ya jengo kinasema:

Proposed Building of Parrot Hotel...
Client: Hassan Hussein Mshana...

Jengo la katikati linaitwa "Arusha Consultants House" limefunguliwa hivi karibuni. Jengo la rangi ya Pink ni "Arusha Golden Rose" la Mama Maeda.

Mmiliki wa hili jengo la Parrot Hotel according to nyaraka za Arusha Municipal Council, ni jamaa mmoja anayefahamika kwa jina la Hassan Hussein Mshana, maarufu mjini Arusha kwa jina la "Shanna Boyz". Huyu bwana Mshana, anajihusisha na biashara ya wholesale ya mafuta ya kupikia na vitu vya matumizi ya kila siku kama Viberiti, Sukari etc. Pia inasemekana kuwa, ana migodi ya Tanzanite huko Mererani, wilaya ya Simanjiro, mkoa wa Manyara. Ujenzi wa hii hoteli ulianza mwanamo mwaka 2005. Kabla ujenzi haujaanza, kiwanja inapojengwa, kilikuwa kikitumika kuuzia mbao wakati wa mchana na kuegeshea Mabasi ya "Air Msae" wakati wa usiku. Inasemekana kwamba, aliyekuwa akiuzia mbao kwenye hiki kiwanja ndiye aliyekuwa amewakodishia wamiliki wa "Air Msae" sehemu ya kuegesha mabasi yao usiku.Kwa jina anaitwa "Kampa" na kabila lake ni Mhaya kutokea Bukoba. Hata hivyo, kiwanja hakikuwa cha kwake (Kampa) bali yeye pia alikuwa amekodisha kutoka kwa wamiliki halali ambao according to nyaraka za office ya registry of lands, northern zone, iliyopo Moshi, ni shirika moja la umma linalofahamika kwa jina la "NEDCO" (National Estates and Design Company)

Habari ambazo hazijathibitishwa zinasema, huyu bwana Kampa, alimtapeli bwana Hassan Hussein Mshana kwa kumuuzia hicho kiwanja wakati akijua fika yeye siyo mmiliki halali wa Kiwanja. Inasemekana kwamba, bwana Mshana aliingia mkenge baada ya Kampa kumpa title feki ya kiwanja iliyokuwa ikionyesha kuwa Kampa ndiye mmiliki, wakati sio(Wamiliki halali ni NEDCO).Baada ya Mshana kununua kiwanja kutoka kwa Kampa, alianza mara moja ujenzi wa Hoteli yake ya "Parrot". NEDCO wenye offiici zao Mkoa wa Dar es Salaam, ndipo wakapata habari kwamba kiwanja chao kimevamiwa na kuna ujenzi kabambe wa hoteli unaendelea.NEDCO walijaribu kumtafuta bwana Kampa wamuulize nini kinaendelea bila mafanikio. Wliposhindwa kumpata Kampa, NEDCO walikimbilia mahakamani na kufanikiwa kupata injunction ya kumsimamisha bwana Mshana asiendelee na ujenzi.Pia walimfungulia Mshana shitaka la "Tresspassing" on their property.Mshana alipokuwa served na injunction ndipo akashtukia kuwa alikuwa kaingizwa mjini na Kampa. Mshana aka retain legal counsel, legal counsel wakamshauri aombe "out of court settlement" na NEDCO.Inasamekana hii settlement ili invlove NEDCO kumuuzia Mshana kiwanja hicho hicho for an "undisclosed" sum of money.Suggesting that Mshana paid for the same plot twice!!

Mpaka leo hii haifahamiki Kampa yupo wapi. Kuna an "outstanding" warrant for his arrest at the Arusha Central Police Station, to face charges of Fraud & Forgery.Anyways, baada ya settlement na NEDCO, Mshana thought his problems were over, kumbe infact they had just began. Manispaa ya Arusha ambao ndio wahusika wa kutoa vibali vya ujenzi, wakamsimamisha asiendelee na ujenzi kwa kuwa ailkuwa akijenga bila "building permit" Habari zisizothibitishwa zinasema kuwa, manispaaa ya Arusha wakati huo ikiwa chini ya Mkurugenzi (Noah Mwaikuka) pamoja na mwanasheria wa manispa "Solicitor general" (Anderson Msumba) pamoja na Engineer (S. Ngagani) walipata amri kutoka the highest levels of government, wampe mara moja kibali cha ujenzi bwana Mshana. Bwana Mshana hatimaye alipata kibali cha ujenzi ndani ya wiki moja(bila kupigwa fine yoyote) akaendelea na ujenzi wake.


.......Story continues later, where I will talk about the connection between Hassan Hussein Mshana and former Permanent secretary - Paymaster General, Ministry of Finance, Tanzania (Gray.S. Mgonja). I will also talk about how Initially, The Contractors Registration Board of Tanzania (CRB) and later the Engineers Registration Board (ERB) of Tanzania tried to stop the construction of this "Parrot Hotel" bila mafanikio, due to powerful forces within government always intervening on behalf of Mshana........ stay tuned...
 
Last edited:
Lifer

very interesting story!

You never went to bed last night? Look at the posting time: Lifer Today, 02:53 AM
 
Hongera Lifer kwa kazi nzuri endelea kutuhabarisha juu ya hawa mafisadi!!
 
Mkuu Lifer good analysis.Hili jengo karibu wakaazi wote wa mji wa Arusha wanajua linamilikiwa na G Mgonja tatizo linakuwa jinsi ya kumlink na umiliki.Hassan Hussein Mshana hana ubavu wala wazo la kuwa na jengo kama hili anatumikia wakubwa.

Hii issue kwa kiasi kikubwa inafanana sana na umiliki wa Kibo Hotel ambayo mheshimiwa B P Mramba anaimiliki kwa siri.Baada ya kustukiwa nasikia ameamua kumuuzia Uhuru kenyatta.

Serekali ikitumia vyombo vyake vyema kama UWT na TRA bwana Hassan Hussein Mshana hatakuwa na ujanja wa kuendelea kutudanganya.

Mkuu Lifer tunasubiri nondo zako kwa hamu.
 
Shana Boyz enzi zao walikuwa na Maduka ya jumla,Magari na Mabasi ktk mji wa Moshi na Arusha... Nilishangaa kuwa ni nani aliyeporomosha ilo ghorofa ambalo limejengwa chini ya Kiwango kumbe ni wao... Wakishirikiana na Gray???
 
Last edited:
Kweli mtandao wa mafisadi ni mkubwa kwni kutokana na analysis hapo juu ni kuwa ujenzi ulikuwa unasimamishwa na mara unafufuka kwa kupitia ofisi zenye madaraka makubwa kuliko manispaa ya Arusha (Mkuu wa Mkoa? TAMISEMI? Ofisi ya Waziri Mkuu? Wizara ya Sheria? Wizara ya Miundo Mbinu? Ofisi ya Raisi? ...... nachoka....). Tunasubiri maelezo ya nyongeza kuhusu kuhusuka kwa Gray Mgonja ili tukonect dots na kujua hiyo nguvu kubwa ilitokea wapi??
 
Hilo jengo nililiona Arusha kwa mara ya kwanza nikashangaa litakuwa na ghorofa ngapi kwa sababu lilikuwa linaenda juu tu. Halafu nikashangaa jengo kubwa namna hiyo mbona limejengwa kwenye kiwanja kidogo tu? lakini nafikiri limesimama muda mrefu na nilisikia wanasema eti linahusishwa na EPA sijui kama ni kweli
 
anyways, baada ya settlement na nedco, mshana thought his problems were over, kumbe infact they had just began.manispaa ya arusha ambao ndio wahusika wa kutoa vibali vya ujenzi, wakamsimamisha asiendelee na ujenzi kwa kuwa ailkuwa akijenga bila "building permit" habari zisizothibitishwa zinasema kuwa, manispaaa ya arusha wakati huo ikiwa chini ya mkurugenzi (noah mwaikuka) pamoja na mwanasheria wa manispa "solicitor general"(anderson msumba) pamoja na engineer (s.ngagani) walipata amri kutoka the highest levels of government, wampe mara moja kibali cha ujenzi bwana mshana.bwana mshana hatimaye alipata kibali cha ujenzi ndani ya wiki moja(bila kupigwa fine yoyote) akaendelea na ujenzi wake.

bravo,bado tunasubiri,! Move yenyewe
hii inaonyesha kuwa mtandao wa kifisadi ni mkubwa sana,na unwahusisha watu wengi, inawezekana wakati mwingine tunatumiwa na mafisadi bila kujua,unaweza kuona kuwa unamsaidia baba, mjomba,kaka ,dada au shangazi labda kwa mawazo ya kulipa fadhila au kwa uaminifu wa kijamaa kumbe unatumika bila kujua.
 
Heshima mbele mkuu Lifer...very good background, mwenyewe nililiona jengo hilo December Last year, nilijuliza viswali vingi sana!

Please please...tuletee full nondo!
 
Back
Top Bottom