Hoteli ya kitalii aliyozindua Rais Kikwete yabomolewa

rais anatumiwa vibaya.....hata yule kaburu aliyezuia Kamati ya Bunge ana mtindo wa kutumia vimemo vyenye sahihi ya Kikwete, kufacilititate deal zisizohusiana na biashara zake..
 
mwenye hoteli ni mkorofi tu! Kabla ule ukuta haujaisha aliwekewa x. si wapitaji tuliona, lakini yeye akapaka rangi na kuendelea. wakati mwingine ujue watu wanadharau sana. Naunga mkono kwa walichokifanya Tanroad, Na iwe fundisho kwa wengine.
 
Na pia hata contractor aliyejenga ile hotel pamoja na consultant wake kuna haja ya kuwa na hofu nao. Pamoja na profession waliyo nayo wamekubaliana kujenga barabarani! Hii ni kudharirisha profession zao. Board zinazosimamia watu hawa zinatakiwa kuwamlika zaidi.
 
kinachotakiwa kitazamwe ni timing ya kubomoa na mda, je kubomoa siku mbili baada kuzinduliwa ni sahihi, walikua wapi siku zote? hakuna taratibu za kuzuia ujenzi kabla (injuction order) kama wako sahihi? na cha kubomoa usiku je(tanroad wanafanya kazi kwa shift za usiku pia)? nadhan suala la kukomoana liko zaidi kuliko kufata sheria, mimi ni mkazi wa arusha, kuna majengo mengi yaliyopo ktk uzio wa barabara mbona hayabomolewi kwa mfano kuna vituo vya mafuta kwenye njia hiyohiyo ya dar-arusha-nairobi vilivyopo karibu ya barabara kuliko hiyo hotel, je vituo vya mafuta si hatari zaidi ya hotel? mbona havivunjwi? sio kama natetea uvunjaji wa sheria, sheria inakua na maana tu kama inakua msumeno kwamba inakata kotekote haibagui na sio upendeleo(double standard).
je iyo barabara inajengwa lini? mpaka mda wanataka kupanua barabara mwekezaji uyu mzawa si atakua amerudisha investment yake? achilia mbali families zitazokua zimefaidika na nchi kiujumla?
 
Kwani tatizo ni rais kufungua hoteli? Huyu mwekezaji inaelekea alikuwa tayari na demolition order na ndiyo akataka kufanya usanii wa kujificha nyuma ya wigo wa "Hoteli imefunguliwa na Rais." Suala si rais kafungua hoteli, suala si mbona jirani hawajabolewa. Suala ni je amejenga ndani ya road reserve? Suala ni je alishapewa demolition order? Kuwa mwekezaji MZAWA hakumpi blank cheque ya kufanya atakalo. Kajenga parking kwenye sehemu isiyoruhusiwa na sheria imefuatwa. Asitake kutubabaisha.

Amandla.......


Naungana na Fundi Mchundo kuwa tatizo la msingi hapa ni mmiliki wa hoteli hii kujenga eneo la parking ya hoteli yake kwenye hifadhi ya barabara wakati akijua kuwa huu ni uvunjaji wa sheria.

Nashawishika kuamini kuwa huyu mwekezaji alijua nia ya TANROADS kubomoa sehemu hiyo (kwani alishapewa demolition order) ila akadhani kuwa kwa kumwalika Rais kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi basi TANROADS wangefyata mkia.

Huu ni mfano mmoja wa maamuzi magumu, aliyokuwa akisema Jaji Warioba, ambayo inabidi serikali na vyombo vyake viyafanye ili nchi iweze kwenda mbele. Huu utamaduni wa kutokujali sheria na taratibu tulizojiwekea umechangia kwa kiasi kikubwa hali ya mambo kuwa kama ilivyo sasa.

Labda tujiulize swali la msingi hivi ufunguzi wa hoteli binafsi unahitaji mkuu wa nchi aufanye?
 
Katika hili TANROADS pamoja na kumkomoa mwekezaji wa Hotel hii pia WAMEMDHALILISHA Mkuu wa kaya hii. Haiwezekani Rais afungue hotel leo kesho TANROADS waje kuvunja tena usiku wa manane kama vile ni wevi!!!!

Kwa mantiki rahisi kabisa hebu tujiulize. Huyu mwekezaji alianza kujenga lini? Tanroads walikuwa wapi muda wote?Haiwezekani kuwa Hotel hii imeota kama uyoga in a single night na kesho yake JK akaja kuifungua. Nasema haiwezekani!

Kwa hiyo watu wa USALAMA WA TAIFA wanatakiwa wachemshe ubongo ili kubaini au kujua nini maana ya kitendo hiki!! Ni kweli Tanroads wamevunja kwasababu amejenga kwenye road reserve au wamefanya kazi hii kwa msukumo wa watu fulani ili kumdhalilisha Rais??? Yawezekana kabisa kuna mkono wa mafisadi au wale walio kinyume na JK wametumwa ni kumdhalilisha makusudi.

Wanausalama kazi kwenu.
 
1. Rais alienda kufungua hoteli na siyo kitu kingine na hoteli ilifunguliwa na inafanya kazi. Nasema Rais hajakashifiwa.
2. TANROADS walienda kubomoa uzio ambao ulijengwa kwenye Road reserve baada ya kuwa wametoa notice kisheria.Notice haikuwa ya kuvunja hoteli bali uzio. Walichofanya TANROADS ni sahihi. Hawakubomoa hoteli iliyofunguliwa na Rais. Rais hajakashifiwa. Kashfa ni yake mwenye hoteli kwa kukaidi maagizo ya TANROADS.
3. Hoteli bado iko intact. Anachotakiwa kufanya ni kujenga uzio eneo linalokubalika kisheria. Mimi ni mkazi wa Baraa na ninayo nyumba upande huo huo ambako hoteli hiyo ilipo. Nilipokamilisha kujenga nyumba yangu which is 50 metres from the centre of the road, uzio wa ukuta nilikuwa nimejenga ndani ya road reserve kiasi cha mita moja. Nilipewa notice na manispaa wakati huo ya kuuondoa ukuta. Ukuta-mind you- siyo nyumba. Sikubisha. Nilichukua mafundi nikawapa kazi ya ‘kubomoa' ukuta kwa kutoa tofali moja baada ya nyingine hadi ukuta ukawa haupo tena. Matofali hayo hayo nikajengea ukuta mwingine mita 10 ndani zaidi. Hakuna kilichoharibika. Nilitimiza wajibu wangu kwa kuwa raia mtiifu wa sheria.
4. Sasa swali nauliza. Kashfa kwa Rais hapo iko wapi? Baadhi ya wanasiasa wanataka uongozi wa mkoa uwajibike kwa kumpotosha Rais kweli wako sahihi?
5. Ninakumbuka mwaka 1971 Rais Nyerere alikwenda kufungua jengo la IPS likiwa linamilikiwa na AgaKhan, siku ya pili jengo hilo likataifishwa na serikali iliyokuwa chini ya Nyerere na akapewa Msajili wa Majumba. Nyerere hakukosea. Yeye alialikwa kufungua jengo. Lakini sheria ya Acquistion Buildings Act ya 1971 ikachukua mkondo wake. Mlio watu wazima huenda mnalijua hilo. Sasa JK kaenda kufungua hoteli na hoteli bado inafanya kazi kashfa hapo iko kwa JK au kwa mwen ye hoteli? Jamani let us be objective. Aliekashifiwa hapo ni Bwana Tarimo wala siyo Kikwete.
 
Big up! Marigwe! You have shown your maturity in sensitive issues. Rais hayupo kuvunja SHERIA YA NCHI. Big up TANROADS kwa maamuzi MAGUMU. VILAZA wengine wasingeweza.
 
headline_bullet.jpg
Ina thamani ya Shilingi bilioni 10
headline_bullet.jpg
Tanroads: Ilijengwa barabarani

HotelSnow%281%29.jpg

Baadhi ya wanakijiji wakisafisha mabaki ya sehemu ya mbele ya Hoteli ya Snow baada ya Wakala wa ujenzi wa Barabara Nchini (Tanroads), kuvunja sehemu hiyo mkoani Arusha jana.

HotelCrest.jpg

Hoteli hiyo ilivyokuwa kabla ya kuvunjwa.

remove.jpg

box_on.jpg

box_off.jpg

add.jpg




Hoteli ya kimataifa ya Snow Crest iliyojengwa kwa gharama ya Sh. bilioni 10 imevunjwa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Arusha, kwa maelezo kuwa imejengwa ndani ya eneo la barabara.
Tukio hilo limetokea siku mbili baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzindua hoteli hiyo na kutoa wito kwa wafanyabiashara wazawa kuwekeza katika sekta ya utalii.
Tanroads ilishikilia msimamo kuwa ingeibomoa hoteli hiyo iliyopo eneo la Ngulelo, kandokando ya Barabara Kuu ya Arusha-Moshi, ikidai kuwa imeingilia eneo la barabara kinyume na sheria.
Mkurugenzi Mtendaji wa hoteli hiyo, Wilfred Tarimo, akizungumzia tukio hilo, alisema wafanyakazi wa Tanroads walifika juzi usiku wa manane wakiwa na askari sita wenye silaha na tingatinga na kubomoa eneo la mbele na maegesho ya hoteli hiyo.
“Nilipigiwa simu usiku na wasaidizi wangu kuwa hoteli inavunjwa, nilifika na sikuamini nilichokuwa nakiona kwa macho yangu, hoteli imevunjwa na kutokea kwa uharibifu mkubwa,” alisema Tarimo.
Aliongeza kuwa tukio hilo lilisababisha wageni zaidi ya arobaini waliokuwa wamefikia hotelini hapo kupatwa na hofu ya kupoteza maisha au mali zao.
“Mimi kama mwekezaji mzawa nilikuwa najitahidi kuwekeza katika utalii, nimeumizwa na kufedheheshwa sana na tukio hili, kila mwenye uwezo wa kufikiri anaweza kuwauliza Tanroads walikuwa wapi mpaka Rais azindue hoteli ndio waje wavunje?”alihoji Tarimo.
Aidha,Tarimo alihoji ni kwanini hoteli hiyo tu ndiyo ivunjwe wakati kuna majengo mengine katika eneo hilo.
Akizungumzia tukio hilo aliyewahi kuwa Meya wa Manispaa ya Arusha na Diwani wa Kata ya Baraa eneo ilipo hoteli hiyo, Paul Laizer, alihoji uhalali wa Tanroads kufanya zoezi la uvunjaji usiku alihoji: “Kama kweli walikuwa wakifanya jambo la haki ni kwa nini walifanye zoezi hilo wakati wa giza kwanini wasifanye mchana kweupe,” alihoji.
Chama cha Mawakala wa utalii kimepokea tukio hilo kwa masikitiko makubwa na kusema kuwa halikuwa la haki.
Katibu Mtendaji wa chama hicho, Mustafa Akuunay, alilisitiza kuwa Tanroads haikuwajibika ipasavyo na kwa wakati unaofaa na picha inayojitokeza inaacha maswali mengi yasiyo na majibu.
Akuunay alihoji ni kwanini hoteli hiyo ikalengwa na majengo mengine kuachwa.
“Ni kwanini tingatinga limeacha majengo mengine na kuvunja hoteli pekee kuna nini hapa kinachofichwa,” alisema.
Aidha alisema kuwa hatua hiyo itapunguza idadi ya watalii wanaozuru kaskazini mwa nchi na kuleta fedha za kigeni na ajira kwa Watanzania huku ikikatisha waazawa tamaa ya kuwekeza katika sekta hiyo.
Mgogoro wa hoteli hiyo na Tanroads umekuja baada ya wakala huo kudai kuwa imeingiliwa katika eneo lake ambalo linatajiwa kutumika katika upanuzi wa njia nne za barabara kati ya Arusha-Moshi katika siku zijazo.
Hali hiyo ndio iliyoifanya Tanroads kutaka uongozi wa hoteli hiyo kuibomoa kabla ya Novemba 10, mwaka huu.
Meneja wa Tanroads Mkoa wa Arusha, Desdatus Kakoko, alisema jana kuwa ataitisha mkutano na wanahabari kuelezea kuhusu sakata hilo.
Hoteli ya Snow Crest yenye hadhi ya juu, ina vyumba 83 na imeasisiwa na kumilikiwa na wafanyabiashara watatu wazawa.
Hata hivyo, haikuweza kufahamika ilikuwaje uongozi wa Mkoa wa Arusha kumruhusu Rais kufungua hoteli hiyo Ijumaa iliyopita bila kujua kuwa hoteli hiyo ilikuwa katika mgogoro na Tanroads.




CHANZO: NIPASHE


Niliuliza hivi karibuni kwamba Muungwana alikuwa anakwenda kuzindua hoteli moja arusha na kuhoji uhalali wa hoteli hiyo, au kama inahusiana na wale wanaotajwa kwa ufisadi. bahati mbaya thread ile sikuiona na sielewi kama ilihamishiwa kwingine. Sasa mambo ndiyo hayo tena, siku mbili tu baadaya sherehe za uzinduzi inabomolewa.
Hivi mamlaka zinazohusika zikuwa wapi mpaka hoteli hii inajengwa kwenye eneo la barabara, halafu wakasubiri imezinduliwa ndipo wakaibomoa? au ilikuwa inajengwa usiku na kuhamishwa asubuhi kiasi kwamba watu walikuwa hawaioni hadi ilipozinduliwa ndipo wakaiona?
Nadhani kuna walakini mahali fulani. Mwenye dondoo naomba atusaidie jamani. tunakwenda wapi tanzania.

Kuna habari zinasema kuwa Rostam Aziz karibia anajitoa katika umiliki wa New habari corp,mlioko huko jikoni tupeni taarifa zaidi.Hili litakuwa jambo la maana sana mafisadi kuachia vyombo vya habari.
 
Mkuu Jayfour.

Sio lazima uandike kimombo. Naona kiswahili kingeeleweka zaidi. JF =GT

tunaitaji watu kama nyie 60 kuelimisha wana jamii forums kwamba watu wanaitaji kuelewa kinachoandikwa
 
politically its a shame kw rais,wasaidizi wake wameonyesha udhaifu mkubwa.....rais hakuwa na ulazima wa kuzindua hoteli ambayo afta few days inavunjwa,coz hata kama ni kukomaa kwa TANROADS kwa kuchukua maamuzi magumu,si kila mwananchi ataona ni sawa......akili za wabongo zinatofautiana...
 
Huo ndio ukweli wenyewe. Japo kuwa nchi inahiatji wawekezaji wazalendo kama hawa waliojenga hotel nzuri kama hiyo, lakini vile vile tunataka wawekezaji hawa wawe wanaheshimu sheria mbali mbali zilizowekwa na mamlaka za nchi yetu. Kwakuwa hawa walivunja sheria basi hapa sheria imechukua mkondo wake. Hata hivyo nawapa pole kwa hasara walioipata


Ukweli ndio huo, kama walifikiri kwa kumualika Raisi ndio kukwepa sheria hapo wamekosea.Kwa hiyo mimi nawachukia watu wanaotaka kuhusisha swala hili la kubomolewa kwa ukuta tena uzio na zinduzi wa Rais.Ukuta umebomolewa kwa sababu sheria za barabara zimekiukwa na Rais amezindua kwa sababu amealikwa ili kuwatia moyo wawekezaji wazalendo.Mambo haya mawili yanajitegemea. La pili watu wanalikuza sana Hoteli haikubomolewa ni uzio uliobomolewa na hapa waandishi wawe wakweli na sio washabiki ili wananchi wapate mambo ya kweli.Mimi huu nasema ni uchochezi.
 
Back
Top Bottom