Hotel ya Mount Meru Arusha yaua mwanafunzi

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mwanafunzi Criff Laiza [12] anayesoma darasa la Tano shule ya msingi Sekei katika halmashauri ya Arusha, amekufa maji wakati akiogelea kwenye bwawa la maji yenye kina kirefu katika hotel ya kitalii ya Mount Meru iliyoko jijini Arusha wakati wa sherehe ya X-mass .



Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 12 jioni wakati marehemu na watoto wengine wakiogelea katika hotel hiyo ikiwa ni sehemu ya kusheherekea sikukuu ya X-mass .



Kaimu meneja wa hotel ya Mount Meru , Eric Mgenya akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi na atalitolea ufafanuzi baada ya polisi kukamilisha upelelezi wa tukio hilo .
 
Hilo bwawa nililiona kama vile linafanyiwa matengenezo hivi karibuni.

RIP mtoto....

Ila heading ya thread ibadilishwe...imekaa kishigongo sana
 
Hii hotel inatembea vibaya mpaka ikamkanyaga marehemu!vichwa vya habari vingine ovyo mpaka vinakutoa kwenye msingi wa habari yenyewe!
 
Watoto wa siku hizi ni watundu sana... Wanataka wafanye kila kitu ambacho watu wazima wanafanya... Hawataki kufanya mambo yanayoendana na umri wao... Najua hapo Bwawani kuna kina cha kuogelea watoto wa umri wake, lakini yeye atakuwa amekaidi kwa kutaka sifa... Kwa namna hii acha wafe tu... Tutazaa wengine kuliko kulea watoto watukutu na wakaidi...
 
Back
Top Bottom