Hospitali zituheshimu wateja, mnatuibia sana

Yaani wamefanya kamtaji ukiwa na cash tabu kwenye Bima nao wanapiga juzi nimemaliza kusikilizwa na daktari napewa nisaini zile karatasi zao nawauliza hizi nasaini baada ya kumaliza matibabu na kuchukua dawa iweje nipewe now? tukabishana kidogo nikaona nisaini nafika pharmacy dawa kama tatu hazimo na nimeshazisaini nikawarudia wazitoe wakagoma ili kuepusha shari nikaacha lipite tu since my 1st twin alikuwa ana homa ila kuna baadhi wanaiba huko Bima pia.
Utaratibu ni kusign fomu ya bima baada ya matibabu na sio vinginevyo.
 
Utaratibu ni kusign fomu ya bima baada ya matibabu na sio vinginevyo.
Soma tena
Hawakukuandikia fomu nyingine ya kupata hizo dawa kwenye Pharmacy ya Bima mtaani?

Endapo hizo dawa wanazosema hawana halafu baadae wazijaze watakipwa na Bima. Hapo ndipo upigaji maana watalipwa kitu ambacho hawajakitoa
Hawakuniandikia kabisa yaani niliondoka tu kuepusha shari maana nilikuwa na mtoto
 
Jana nimeenda hospital moja hapa Tegeta kibaoni, na imeshajijua maana ipo peke yake pele kibaoni. Waanapiga bei kubwa sana wateja wao, kujiandikisha tu pale ni 7,500/= na sijui ni yanini maana hata file hupewi mambo yote yapo kwenye system za computer. Baada ya hapo anakwambia inachofuata ukamuone daktari, kumuona daktari ni 15,000/=. Dokata anakupa vipimo ukafanye, achana na gharama za vipimo hizi sibishani nazo.

Noma ilikuja baada ya vipimo vyote tukaandikiwa sindano 3 na dawa za kutuliza maumivu. Tuliambiwa gharama za sindano moja ni 37,000/= Hapo ndio kengele ikalia kichwani na kujua hapa kuna shida. Nikaomba niandikiwe ni sindano gani ili nichome mbele kwa mbele, hapo dokta akaanza kukataa anasema harusiwi kutoa hicho kitu inaweza kumletea shida kikazi, ilileta ubishi mkubwa sana kwakuwa mimi nimeshalipa kukuona na kila kitu kitoka kwako nimeshalipia na gharama za vipimo hapa niandikie hizo dawa mi niondoke, ndio kwa mbinde nikapewa majina ya hizo dawa.

Nikaenda pharmacy ipo opposite tu na hiyo hospital hizo dawa hapo wanauza 7,000/= tu na lile bomba la sindano ni 500/= Nikamlipa nesi 3000 nikachomwa sindano yaani 10,000/= nikawa nimepata tiba ambayo ilibidi nilipe 37,000/=

HOSPITALI MUWE NA HURUMA NA WATEJA WENU, MTU AKIUMWA ISIWE NAFASI YA KUMPIGA, SIO POA KABISA
Hiyo hospitali nilienda last week SAA tatu usiku nilitoka saa saba na robo usiku wagonjwa wengi then kulikuwa na daktari mmoja. Nimetoka nakuta Malaya kama wote pale stendi ya bajaji
 
kuna hospitali moja iko dar mjini ya kina chakorii,aisee hata kama ukiwa na maleria moja ukienda pharmacy lazma upewe dawa mpaka 10 za kumeza na wengine unakuta mpka dawa 15 yani ukiumwa mara 20 kwa miez 6 basi unafungua pharmacy
 
Kuna hospitali wanaitwa wauguzi wanaulizwa mbn dawa hizi na hizi hamziandiki zimejaa store tu. Kuna siku et jamaa kaandikisha cheti wanapigiana simu huyo anapesa fanya kweli. Hivi hii ethic kweli?.
Mtu unaenda unasema unaumwa kifua unaambiwa upime UTI na Malaria, hujasema unaumwa kichwa wala kupandisha homa.
Kuna dogo nilimpeleka hospital ana vipele mwilini, but aliambiwa apime UTI na Malaria.

Sent from my Infinix X623 using JamiiForums mobile app
Hahahaa
 
Yaani wamefanya kamtaji ukiwa na cash tabu kwenye Bima nao wanapiga juzi nimemaliza kusikilizwa na daktari napewa nisaini zile karatasi zao nawauliza hizi nasaini baada ya kumaliza matibabu na kuchukua dawa iweje nipewe now? tukabishana kidogo nikaona nisaini nafika pharmacy dawa kama tatu hazimo na nimeshazisaini nikawarudia wazitoe wakagoma ili kuepusha shari nikaacha lipite tu since my 1st twin alikuwa ana homa ila kuna baadhi wanaiba huko Bima pia.
na hii tabia ya ku sign kabla naona ipo Sana unasign kabla ya matibabu
 
Kwani specialist nini bwana, mimi ni specialist lakini hata bure unaweza kuniona..............unakuwa specialist ili uwahudumie watu kwa maarifa ya kiwango cha juu siyo ulipwe pesa nyingi. Haya mambo ndo yanafanya watu wanashindwa kuhimili gharama za matibabu hospitali wanakimbilia kwenye miti shamba. Kwa case ya huyu mleta mada yeye tayari ameshalipia kumwona daktari na vipimo nk. iweje apigwe tena cha juu kwenye dawa? acheni ku complicate mambo utafirkiri nyinyi hamtaugua wala kufa......
barikiwa mkuu siku hizi udaktari sio wito ni business
 
Sahihi kuna kipindi nilipeleka binti wa kazi kupata matibabu nikaandikiwa dawa. Hizo dawa alikuwa anywe kwa miezi miwili alikuwa na tatizo la upungufu wa damu unaojirudia mara kwa mara. Kwa sababu nilipungukiwa hela ikabidi nilipie dawa za wiki mbili. Baada ya dawa kuisha nikaona uvivu kurudi hospital nikaenda phamarcy dawa nilizouziwa Tsh 22000 nikanunua kwa Tsh 8000.
Ukweli hospitali zinatupiga hela sana.
 
Sijaelewa hapa kwenye kumuona Daktari 46000/-

Au unamaanisha ni pamoja na Vipimo na Dawa??
agha khan kildaktari unayemuona kutokana na sifa zake ana bei yake.

kuna dr specialist wa tumbo kumuona ikikuwa 54k au 56k kama sikosei. Ila sikujuta kumuona yule dk kwa kweli......
 
Back
Top Bottom