Hospitali zetu na majibu yasiyo sahihi - it happened to me.

Tsidekenu

Senior Member
May 7, 2009
141
39
Bandugu,

siku chache zilizopita - nilikwenda hospitali ya mikocheni kwa ajili ya matibabu. Kutokana na dalili nilizokuwa nazo daktari alishauri nipime vipimo mbalimbali ikiwemo kipimo cha sukari. Kipimo cha sukari kilionyesha nina sukari 16.5, yule lab technician akashtuka kweli akaniuliza kama nina tatizo la sukari, nikamwambia hapana sijawahi kuwa na hilo tatizo. Pia akaniuliza umeshakula? ni kamwambia of course nimeshakunywa chai maana muda huo ulikuwa ni kama saa sita hivi mchana, akasema hebu ngoja tupime tena ambapo majibu ya mara ya pili yakaonyesha ni 14.2 basi akaniambia ndio hivyo kisukari kina kunyemelea hivyo nenda kwa daktari akakupe ushauri.

Kufika kwa daktari akaniambia hii sukari sio nzuri lakini kwa kuwa nimeshakula, niende kesho yake asubuhi kabla sijala kitu chochote tupime tena tuone ikoje ndio tuamue ufanye nini. Nikaandikiwa madawa mengine kwa ajili ya vilivyoonekana kutokana na vipimo vingine nilivyopima nikaondoka zangu.

Kesho yake asubuhi niliamkia mjini kwa shughuli zangu zingine na nikaamua kwenda Burhani kupima, kwa kuwa nilishaambiwa nisile kitu, ni kawa kweli mtiifu sikula kitu chochote. Majibu yakaonesha sukari ni 5.4, na daktari akanieleza kuwa hii ni sawa haina tatizo. Lakini out of curiosity nikasema ngoja nirudi pale pale mikocheni nikapime tena bila kula kitu chochote. Kufika wakanipokea vizuri wakanipima na majibu yakaonyesha sukari ni 15.0. Yule mpimaji akaniambia majibu ni hayo una kisukari. Duu nikamwambia hii inawezekanaje? Nikamweleza scenario yote kuanzia ya jana yake (mpimaji hakuwa yule aliye nipima jana yake) na nikamuonyesha majibu ya burhani. Nikamwambia mi nafikiri hii mashine yenu ni mbovu, akasema haiwezekani hizi mashine hazitoagi majibu ya uongo, unless labda kama kuna mtu alikosea strips sijui etc (aliniambia maneno ya kitaalam kidogo). Lakini akasema ngoja ajipime na yeye aone majibu yatakuaje. Alipofanya hivyo majibu yake yakasoma 11.5 akasema kweli kuna kitu sio sawa hapa ikabidi amuite in charge ambapo wakawa wanajiongelesha hapo, wakijaribu kufikiria what could be the issue, pia wakagusia kwamba wakati mwingine mashine za kupimia huwa hazifanani. To cut a long story short, tulikubaliana kuwa niende tena nikapime hapo tuone majibu yatakuaje. Bado sijaenda tena (mambo yaliingilia but nitafuatilia)

My take;
- kwa madaktari/lab technician - je inawezekana majibu yakatofautiana kutokana na aina ya kipimo kinachotumika?
- mimi nafikiri mashine yao ni mbovu - wataalamu nisaidieni kama kuna any explanation to this variation if we rule out ubovu wa mashine.

NB; Nasisitiza kuwa vipimo vya siku ya pili nilivifanya nikiwa sijala kitu chochote.
 
Mkuu kabla ya kurule out kuwa una sukari au la tembelea maabara au hospital kana tatu nne
haijalishi kuwa unatumia gharama ila usije ukaanza kujipa ugonjwa ambao hauna
na ambao utakucost sana kujilipua kwa madawa ya sukari wakati hauna hiyo kitu
Maana kuambiwa tuu kuwa unanyemelewa na kisukari hapo hata mapigo yako ya moyo nafikiri yalibadilika
So mkuu nakushauri tembelea maabara au hospital nyingine ili ulinganishe majibu yao na yale ya mwanzo na ikiwa majibu yatatoka kama hayo ya Burhani ujue kabisa kuwa mashine ya Mikocheni itakuwa na matatizo
 
Nb .kwani tumebisha kwamba ulikula mkuu iyo siku ya pili
pole hii ndo tz
kuna hosp ukienda lazima uambiwe una typhod,nyingine lazima uwe na malaria nadhani inategemea wana stock kubwa ya dawa zipi kwenye store yao. Hapo stock ya diabetes ni kubwa so shurti kila mgonjwa aambiwe ana sukari ili apunguze mzigo
mjini hapa
 
Maana kuambiwa tuu kuwa unanyemelewa na kisukari hapo hata mapigo yako ya moyo nafikiri yalibadilika
So mkuu nakushauri tembelea maabara au hospital nyingine ili ulinganishe majibu yao na yale ya mwanzo na ikiwa majibu yatatoka kama hayo ya Burhani ujue kabisa kuwa mashine ya Mikocheni itakuwa na matatizo

we usipime, hakuna siku nilikuwa karibu na MUNGU wangu kama ile siku, nikiomba through out the day and night. nafikiri ningekuwa naomba hivyo siku zote basi maisha yangu yangekuwa mazuri sana.
 
Pole sana kaka....kwangu mimi kisukari ni zaidi ya UKIMWI. Yaani hapo ni sawa na mtu kakuambia kipimo cha UKIMWI kimeonyesha una maambukizi, halafu mwingine anakumbia huna!

Nadhani tatizo hapo ni kukagua vifaa...Ukiangalia guidelines za Good Laboratory Practise zinashauri kila siku kucalibrate upya machine za biochemistry na kuzitest ukitumia standard control...haya hayafanyiki kwenye lab nyingi tu. Na matokeo yake ndio hayo. Angekuwa mtu hasiye mdadisi angeshaanza uguza kisukari wakati hana!
 
we usipime, hakuna siku nilikuwa karibu na MUNGU wangu kama ile siku, nikiomba through out the day and night. nafikiri ningekuwa naomba hivyo siku zote basi maisha yangu yangekuwa mazuri sana.

Kweli kabisa na ni jambo la ajabu kwa mtu kama huyo ambaye umemuamini kiasi hicho kukupa majibu ambayo kwa kweli yanakupeleka uanze kufikiria upya maisha yako
Na ni hatari sana kwa watu ambao tumewaamini kuanza kutupa majibu kama hayo ambayo kwa kiasi kikubwa ni kuanza kutukatisha tamaa
Na angekuwa mwingine angeanza dose ya sukari mapema tuu bila hata kujisumbua kumbe hata dalili zenyewe za sukari huna
Pole sana mkuu zingatia ushauri huo
 
Nadhani tatizo hapo ni kukagua vifaa...Ukiangalia guidelines za Good Laboratory Practise zinashauri kila siku kucalibrate upya machine za biochemistry na kuzitest ukitumia standard control...haya hayafanyiki kwenye lab nyingi tu. Na matokeo yake ndio hayo. Angekuwa mtu hasiye mdadisi angeshaanza uguza kisukari wakati hana!

yani hapa najiuliza sijui na majibu ya vipimo vingine yapo sahihi kweli? au ndo kama "smile" alivyosema kukiwa na stock ya dawa fulani basi watu wote mtaambiwa mna huo ugonjwa ili tu wauze dawa. maana si haba niliacha 40,000 hapo.
 
Pole sana kaka....kwangu mimi kisukari ni zaidi ya UKIMWI. Yaani hapo ni sawa na mtu kakuambia kipimo cha UKIMWI kimeonyesha una maambukizi, halafu mwingine anakumbia huna!

Nadhani tatizo hapo ni kukagua vifaa...Ukiangalia guidelines za Good Laboratory Practise zinashauri kila siku kucalibrate upya machine za biochemistry na kuzitest ukitumia standard control...haya hayafanyiki kwenye lab nyingi tu. Na matokeo yake ndio hayo. Angekuwa mtu hasiye mdadisi angeshaanza uguza kisukari wakati hana!

Riwa nyingi ya maabara hizo ni kutafuta pesa na sio kutoa huduma zile kweli za kiuchunguzi na kukupa majibu sahihi.
Kuna maabara kila uendapo pale ni lazima uambiwe either una malaria au typhoid na ukishaambiwa hayo ni lazima tuu upewe dose ya hayo magonjwa
Sasa unajiuliza mbona kila nikija hapa naambiwa tuu haya magonjwa
Wengi wamekuwa wafanyabiashara na sio kusudi lile halisi la kutoa majibu sahihi kwa wagonjwa na magonjwa yao
Unapomuambia mtu ana typhoid na aanze dose ya huo ugonjwa wakati hata dalili zake hana ni hatari sana kwa mtu huyo

BTW Mkuu Riwa kuna maswali nilikuuliza hujawahi kunipa majibu mkuu
 
pole sana kaka....kwangu mimi kisukari ni zaidi ya ukimwi. Yaani hapo ni sawa na mtu kakuambia kipimo cha ukimwi kimeonyesha una maambukizi, halafu mwingine anakumbia huna!

Nadhani tatizo hapo ni kukagua vifaa...ukiangalia guidelines za good laboratory practise zinashauri kila siku kucalibrate upya machine za biochemistry na kuzitest ukitumia standard control...haya hayafanyiki kwenye lab nyingi tu. Na matokeo yake ndio hayo. Angekuwa mtu hasiye mdadisi angeshaanza uguza kisukari wakati hana!
mimi hata huwa siamini kama kunalab nzuri tena huku tanzania .maana hamna uniformity ya majibu.kila maabara watakupa majibu yao while damu ni ileile wanapima
craap
 
mimi hata huwa siamini kama kunalab nzuri tena huku tanzania .maana hamna uniformity ya majibu.kila maabara watakupa majibu yao while damu ni ileile wanapima
craap

Wako kibiashara zaidi na sio kutoa ile huduma halisi ya kuchunguza ugonjwa wa mgonjwa husika
We ukienda pale kulingana na dalili zako kama unaumwa kichwa, mwili kuchoka, mafua watajua tuu hapa ni malaria au typhoid
So majibu yatakapotoka ni hayo hayo tuu
 
Si vipimo tu mkuu, hata wataalam wetu nao wanatia shaka.
Kwanza sijui wanajisikiaje wanapoona watanzania wamekosa imani na utaalam wao hadi wanatimukia nje kwa matibabu.
Utaalam naona pia imekuwa tatizo kubwa mtu ukienda hospital unalundikiwa madawa na DR wa kwanza ukienda hospital nyingine anashangaa uwingi wa mdawa na aina ya dawa ulizopewa, hujakaa sawa nayeye anakurundikia ya kwake.

Unakunywa hayo madawa wee nafuu no, mara yanakuletea side effect unabadilishiwa.

Kwakweli TZ sasa hivi intisha na hasa kwenye sector hii ya afya ma dr ni mawakala wa makampuni ya madawa, so ukigusa tu office yake unamadawa lundo bila kuchunguza vizuri ugonjwa wako na bila kutathimini side effect ya hizo dawa.

Kwa kweli kazi ipo sector imechakachuliwa!
 
Si vipimo tu mkuu, hata wataalam wetu nao wanatia shaka.
Kwanza sijui wanajisikiaje wanapoona watanzania wamekosa imani na utaalam wao hadi wanatimukia nje kwa matibabu.
Utaalam naona pia imekuwa tatizo kubwa mtu ukienda hospital unalundikiwa madawa na DR wa kwanza ukienda hospital nyingine anashangaa uwingi wa mdawa na aina ya dawa ulizopewa, hujakaa sawa nayeye anakurundikia ya kwake.

Unakunywa hayo madawa wee nafuu no, mara yanakuletea side effect unabadilishiwa.

Kwakweli TZ sasa hivi intisha na hasa kwenye sector hii ya afya ma dr ni mawakala wa makampuni ya madawa, so ukigusa tu office yake unamadawa lundo bila kuchunguza vizuri ugonjwa wako na bila kutathimini side effect ya hizo dawa.

Kwa kweli kazi ipo sector imechakachuliwa!

Ndo maana wengi wanapewa madawa ya magonjwa ambayo siyo yao au uchunguzi haufanyiki mgonjwa anapewa dawa za home wakati may be figo hazifanyi kazi au ana kidole tumbo au ana amoeba ila yeye analundikiwa dawa za malaria
Ni aibu sana na ndo maana kweli wengi wanakimbilia kutibiwa nje ya nchi maana hapa hakuna lolote la maana
 
si vipimo tu mkuu, hata wataalam wetu nao wanatia shaka.
Kwanza sijui wanajisikiaje wanapoona watanzania wamekosa imani na utaalam wao hadi wanatimukia nje kwa matibabu.
Utaalam naona pia imekuwa tatizo kubwa mtu ukienda hospital unalundikiwa madawa na dr wa kwanza ukienda hospital nyingine anashangaa uwingi wa mdawa na aina ya dawa ulizopewa, hujakaa sawa nayeye anakurundikia ya kwake.

Unakunywa hayo madawa wee nafuu no, mara yanakuletea side effect unabadilishiwa.

Kwakweli tz sasa hivi intisha na hasa kwenye sector hii ya afya ma dr ni mawakala wa makampuni ya madawa, so ukigusa tu office yake unamadawa lundo bila kuchunguza vizuri ugonjwa wako na bila kutathimini side effect ya hizo dawa.

Kwa kweli kazi ipo sector imechakachuliwa!
umeona eeeh yaaani ni mawakala wa madawa hawa jamaa .inategemea ni zipi zipo nyingi store na zimekaribia kuharibika,kama ni za typhoid basi watu woooote tutapewa dozi hiyo
upuuzi
 
Riwa nyingi ya maabara hizo ni kutafuta pesa na sio kutoa huduma zile kweli za kiuchunguzi na kukupa majibu sahihi.
Kuna maabara kila uendapo pale ni lazima uambiwe either una malaria au typhoid na ukishaambiwa hayo ni lazima tuu upewe dose ya hayo magonjwa
Sasa unajiuliza mbona kila nikija hapa naambiwa tuu haya magonjwa
Wengi wamekuwa wafanyabiashara na sio kusudi lile halisi la kutoa majibu sahihi kwa wagonjwa na magonjwa yao
Unapomuambia mtu ana typhoid na aanze dose ya huo ugonjwa wakati hata dalili zake hana ni hatari sana kwa mtu huyo

BTW Mkuu Riwa kuna maswali nilikuuliza hujawahi kunipa majibu mkuu

Samahani...nikumbushe kwenye thread gani, au PM?
 
daah pole sana aisee, huko ndo kucheza na afya za watu sasa! Hivi ni kwa vile wamezoea kuona maiti kila siku kiasi kwamba hawajali uhai wa mtu?

Mimi niliwahi kutibiwa malaria hospitali moja, sikupona nikarudi tena wakasema nifanye vipimo kadhaa ikiwapo UTI na sikupatwa na kitu lakini afya ikazidi kudorora na mbaya zaidi walinidunga midawa ya UTI hata bila kukutwa na hilo tatizo...
Yote tisa kumi ni siku nilofanya kipimo fulani cha dawa sijui mnaita widal blood test? Nikapewa majibu ya mtu mwingine....
Nilihama na hospitali na mpaka leo 'the so called daktari wa magonjwa ya kina mama' ambaye humpati kirahisi (hapi miadi) sitaki hata kumwona.

Ndo madaktari wetu na ndo hospitali zetu
 
daah pole sana aisee, huko ndo kucheza na afya za watu sasa! Hivi ni kwa vile wamezoea kuona maiti kila siku kiasi kwamba hawajali uhai wa mtu?

Mimi niliwahi kutibiwa malaria hospitali moja, sikupona nikarudi tena wakasema nifanye vipimo kadhaa ikiwapo UTI na sikupatwa na kitu lakini afya ikazidi kudorora na mbaya zaidi walinidunga midawa ya UTI hata bila kukutwa na hilo tatizo...
Yote tisa kumi ni siku nilofanya kipimo fulani cha dawa sijui mnaita widal blood test? Nikapewa majibu ya mtu mwingine....
Nilihama na hospitali na mpaka leo 'the so called daktari wa magonjwa ya kina mama' ambaye humpati kirahisi (hapi miadi) sitaki hata kumwona.

Ndo madaktari wetu na ndo hospitali zetu

BHT heri ya mwaka mpya
Wacha tuu hawa watu ni wa ajabu sana
Nishaenda sehem mimi nikaambiwa sijui mara sukari imeshuka mara nina malaria
Wakati wanafanya hivyo nikaenda sehemu nyingine kupima wakaniambia hakuna cha sukari kushuka wala nini
Ni uchovu tuu wa kawaida wa mwili na nipate tuu mapumziko
 
BHT heri ya mwaka mpya
Wacha tuu hawa watu ni wa ajabu sana
Nishaenda sehem mimi nikaambiwa sijui mara sukari imeshuka mara nina malaria
Wakati wanafanya hivyo nikaenda sehemu nyingine kupima wakaniambia hakuna cha sukari kushuka wala nini
Ni uchovu tuu wa kawaida wa mwili na nipate tuu mapumziko


heri na kwako bwana Rocky
yaani hizi hospitali hizi, nakumbuka kuna moja maeneo ya mikocheni tuliipa jina la 'hospitali ya wauaji'. wao hata ukienda unaumwa macho unatundikiwa drip kwanza!!!
 
heri na kwako bwana Rocky
yaani hizi hospitali hizi, nakumbuka kuna moja maeneo ya mikocheni tuliipa jina la 'hospitali ya wauaji'. wao hata ukienda unaumwa macho unatundikiwa drip kwanza!!!

Asante sana BHT
Ndo maana wengi wanakimbilia Nairobi kupata vipimo maana hapa kwa kweli ni balaa
Unaweza kwenda na tatizo la figo ukaaambiwa una appendix bila hata kuchunguzwa
 
Unazungumzia mmol/L au mg/dL?
Najaribu kujiaminisha uwepo wa glucometer hovyo kiasi hicho.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom