Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,367
- 3,778
Nimeshangaa na sijaelewa sera ya Serikali kwa kina Mama Wajawazito, tuliambiwa Mama mjamzito kujifungua ni bure ana hudumiwa, sasa Hospitali ya Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, Mama mjamzito anaambiwa akanunue Pamba ile kubwa, Gloves na akanunue Vidonge vya kuongeza damu na dawa zingine eti wao hawana kweli?
Wizara ya Afya chini ya Doroth Gwajima na Mollel mjitathmini mnapo simama majukwaani na kujinadi kwamba mnatoa huduma ya kina Mama wajawazito bure, nilicho kifanya mimi kwakuwa nilikuwa naelekea Arusha nikaambiwa kuwa mdada anajifungua ambaye ni ndugu nilimpa sh elf6 ya Pamba, Gloves elf 1, Dawa za kuongeza damu elf 4,000 nikaambiwa kwakuwa siku zake bado kidogo anunue dawa zimsaidie mtoto asitoke kabla siku hizo chache anasubiri dawa Hawana zinauzwa elf15 x 3 sasa nikampa hela akaenda kununua.
Hivi Serikali haya maneno yenu kuhusu huduma bure kwa wajawazito iko wapi, ni hapa Wilaya ya Hai tu au na kwingine. Sasa nakumbuka mnavyo jinadi mnasema mnalipa watu Pensheni huku mnakwepa kuzungumzia Mafao ya walio na mwaka hawajalipwa wakiwemo Askari Polisi. Tunako kwenda Mtakubali tu kwamba mmezidiwa sera hazifanyi tena kazi.
Wizara ya Afya chini ya Doroth Gwajima na Mollel mjitathmini mnapo simama majukwaani na kujinadi kwamba mnatoa huduma ya kina Mama wajawazito bure, nilicho kifanya mimi kwakuwa nilikuwa naelekea Arusha nikaambiwa kuwa mdada anajifungua ambaye ni ndugu nilimpa sh elf6 ya Pamba, Gloves elf 1, Dawa za kuongeza damu elf 4,000 nikaambiwa kwakuwa siku zake bado kidogo anunue dawa zimsaidie mtoto asitoke kabla siku hizo chache anasubiri dawa Hawana zinauzwa elf15 x 3 sasa nikampa hela akaenda kununua.
Hivi Serikali haya maneno yenu kuhusu huduma bure kwa wajawazito iko wapi, ni hapa Wilaya ya Hai tu au na kwingine. Sasa nakumbuka mnavyo jinadi mnasema mnalipa watu Pensheni huku mnakwepa kuzungumzia Mafao ya walio na mwaka hawajalipwa wakiwemo Askari Polisi. Tunako kwenda Mtakubali tu kwamba mmezidiwa sera hazifanyi tena kazi.