Hospitali ya Vichaa

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,023
9,285
kuna hospitali moja maarufu ya vichaa hapo ndani ya Bongo.
Basi baada ya madaktari kuwa wamefanya kazi nzito na ya muda mrefu ya kuwatibu wagonjwa wao wakaamua wawape test kidogo tu ili wajue wagonjwa wana maendeleo gani.

Basi daktari akawakusanya kwenye wodi kisha akawaambia walie kama kuku.
wengine wakalia "kokolikooo". wengine wakalia "moooooo" wengine wakalia "meeee".wakati huo daktari yeye anachukua data za wagonjwa wake kama kawa.

Basi kuna kichaa mmoja yeye alikuwa kimyaa ameuchuna tu. Daktari akahisi labda huyu atakuwa amepona.akamfuata kumuuliza kwa nini halii kama kuku. basi yule Kichaa akamgeukia daktari kisha akamwambia huku kidole amekiweka mdomoni SHIIII!!!! Nataga!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom