Hospitali ya Taifa ya Muhimbili haijafungwa

kitu muhim inachobidi wananchi waelewe ni kuwa jukumu la huduma za afya kwa wananchi ni la serikali na sii madaktari kama serikali imeshindwa kutekeleza wajibu wake madaktari wasilaumiwe
labda nitoe mfano kama umeme umekatika kwa sababu nguzo imeanguka nani anatakiwa alaumiwe shirika la tanesco ambalo halinyanyui au kubadilisha nguzo au nguzo iliyoanguka. serikali ni tanesco na nguzo/waya ni madaktari
madaktari wanafanya kazi katika mazingira magumu serikali haitoi vifaa. wanasema wajawazito watatibiwa bure ila ukienda hospitalini vifaa hamna. wagonjwa wanaokufa kwa kukosekana vifaa na madawa ni wengi ambao daktari anajua angeweza okoa maisha kama vifaa vingekwepo.
je daktari huwa kwenye hali gani kama mgonjwa anakufa wakati yeye anajua anaweza kutibu emergency drugs kama fluids kama dextrose 10% au 50%,iv lasix nk. vifaa vya kawaida kama large bore hole canula,giving set za blood,catheter,chest tube nk hivi mgonjwa kama havipo mgonjwa anaweza kufa mbele ya macho ya daktari naye anajua cha kufanya ila hajawezeshwa
Inauma sana yanayotokea serikali baada ya kutafuta suluhisho inagombanisha wananchi na madaktari kama inavyofanya wanapunguza ada shule sekondari wakati huo huo hawatoi pesa kwa ajili ya vifaa vya shule matokeo yake
waalim wanaanzisha michango ambayo hawaikubali kinachofata ugomvi kati ya wananchi na waalim. vivohivyo kwa polisi hawatoi stationery ukufika umeibiwa unapewa karatasi ukatoe kopi matokeo ugovi wananchi na polisi bila wananchi kujua tatizo liko wapi hatutapata suluhisho la kudumu
je unaweza jenga nyumba mpya kwenye kiwanja kilekile bila kubomoa ya zamani.
Naamini hamna daktari anayefurahia hili ila mazingira yamewalazimisha
madaktari ISRAEL waligoma siku 158 miezi mitano ndipo mahitaji yao yakaboreshwa
Mungu ibariki Tanzania
Mwenyezi Mungu wape uwezo watanzania kufanya maamuzi sahihi katika kipindi hiki kigumu
Ahsanteni
 
Tamthilia itakuwa na episode nyigi kwa hali inavyoonyesha.Isidingo cha mtoto
 

Wanajamvi!
Mimi si daktari au mbunge ila ni mwananchi wa kawaida tu katika maisha ya kawaida sana!

Ninashindwa kuwaelewa wale wanaosema "MUUOGOPENI MUNGU" huku wakielekeza kauli hii kwa madaktari tu! Kwani anyepaswa kumuogopa Mungu ni daktari pekee na sio mafisadi wanaoimaliza nchi yetu kwa kula fedha za umma kiasi cha kusababisa watu kufanya kazi katika mazingira HATARISHI! Ninapata uchungu kwa kuona watu wanapoteza maisha, lakini hali hii haisababishwi na madaktari ila MAFISADI!

Kwa mtazamo wangu ieleweke kwa sasa taasisi yoyote pindi ikatokea wanafanyakazi katika mazingira hatarishi lazima mgomo utatokea. Siombei bali ikifikia nchi jirani inataka kuishambulia Tanzania kwa kipindi hiki, basi hata WANAJESHI nao watagoma kupigana kwani mazingira yao yatakuwa HATARISHI!

Sijui nani ana haki ya kutomuogopa Mungu katika nchi yetu hii ambayo watu wanajineemesha kwa rasilimali za umma?

Ndugu yangu KENGEMUMAJI! Sijapinga ulilosema ila nimeona nami nitoe yaliyomo moyoni mwangu.............................


PIGANGOMA
Nasikitishwa na mwenendo wa viongozi wa serikali....
Hoja yako ni nzuri, tatizo
watu wengine akili zao ni finyu wanaanza kuwalaumu madaktari badala ya kumkaba
yule mshika mfuko wa kodi zao ambazo kazi yake ni kuwapa huduma bora zikiwemo
za afya, maji, elimu n.k. Kwani daktari aliwaahidi lini na wapi watanzania
kwamba atawapatia huduma bora za afya? Yeye alichagua kusomea fani aliyoona
inaweza kumpatia maslahi bora katika maisha, kama alivyochagua mhandisi,
mhasibu, mwalimu, rubani na wengine. Sasa kwanini tumlaumu mtu aliyechagua
mwenyewe kwa maslahi yake mwenyewe bila kuwekeana mkataba na wananchi, na
kumwacha mwizi mwenyewe? Hebu tufanyie jambo hili utafiti kabla ya kuchangia
upupu na upotoshaji.
 
Itapendeza kama watarudi kwenye meza ya mazungumzo kwa ajili ya maslahi ya nchi.


Mbu sugu hii ndiyo njia pekee ya wao kusikilizwa, lakini wanachokifanya sasa si sahihi na kinawagharimu wananchi wasio na hatia.
 
Back
Top Bottom