Hospitali ya Taifa ya Muhimbili haijafungwa

Mwanajamii

JF-Expert Member
Mar 5, 2008
7,063
68
Afisa uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili amesema kuwa pamoja na barua waliyoipokea toka kwa madaktari bingwa kwamba na wao wamesitisha utoaji huduma, Hospitali hiyo bado haijafungwa kama baadhi ya wananchi wanavyoposha na kueneza taarifa ambazo si sahihi.

Alisema kuwa huduma zinaendelea kutolewa na madaktari wachache waliopo na kusisitiza kuwa kamwe Hospitali hiyo haitafungwa katika kipindi hiki cha mgomo wa madaktari.

Binafsi nilipita katika Hospitali hiyo jana majira ya saa 9 alasiri na kushuhudia uchache wa watu katika barabara na korido za Hospitalini hapo tofauti na tulivyozoea.

Source: Radio One asubuhi hii.

My take: Chonde chonde madaktari wakati kamati ya bunge ya huduma za jamii ikisikiliza madai yenu, rudini kazini mkaokoe maisha ya watanzania wenzetu.
 
Huyu afisa uhusiano wa Muhimbili ni mtu muongo sana,jana nimeangalia habari itv jitu zima linaongopa wazi wazi na kutoa taarifa zinazokinzana kabisa na hali halisi,hata baadh ya wagonjwa wachache walithibitisha ilo kwa kuongea huku wakilia kwa machungu,hii kitu iliniuma mpaka basi,hali ni mbaya kuliko tunavyofikiria pale muhimbili,na pia utaendeleaje kusifia kua ni hospital ya rufaa wakati haina dk bingwa hata mmoja na huduma zinatolewa na wauguzi kwa sasa?
 
Afisa uhusiano always ni mtu ambaye ataongea defensive statements kumfavor mwajiri wake, ambaye ni serikali!
Ni kuwadi wa Kabaila huyu!
 
Hivi kina Pinda na wenzie wa Afya wanasubri nn kujiuzulu tumechoshwa na usanii wao watanzania wanazidi kutaabika na kuumia jamani jamani jamani watanzania tunaangamia nyie mnaona raha kukaa kwenye viyoyozi na kuzunguka na ma vx na v8...!!

Pinda tumia busara za kijiuzulu washauri na wenzio wa wizara ya afya nao wajiuzuru.
Pinda kauli yako ndio imekutia kikaangani ondoka upishe kiti mwenye busara akakikalie tusonge mbele tuendeshe nchi yetu
 
hawa madaktari ni wauwaji wakubwa,wamekosa ubinadam hata kidogo.
 
Madaktari wamefikia hatua ya kuuza utu wao kwa madai ya fedha huku wakiacha wananchi wanakufa Hospitalini... kwa tulio waamini wa dini yoyote hakuna atakayeunga mkono hili... Hawa madaktari tunaishi nao uraiani na tunajua hadhi ya maisha yao, hawana shida kiasi cha kutufikisha katika hali hii ambayo hata hivyo suala lao liko kwenye mchakato. Madaktari msiangalie ya duniani tu... MUOGOPENI MUNGU!
 
wakati kamati ya bunge ya huduma ya jamii inawahoji pande zote mbili za mgogoro,madaktari wangepaswa kurudi kazini.
 
Wagomee na mishahara ya mwezi wa kwanza ambayo hawajaifanyia kazi,.waache utapeli.........
 
madaktari wasilipwe mshahara wa mwezi january kwa sababu hawakuufanyia kazi.wamesbabisha mauaji kwa kuwanyima wagonjwa matibabu
 
Angetutangazia kuwa Hospitali ya Muhimbili sasa imegeuzwa ZAHANATI tungemuelewa, itakuwaje Hospitali ya RUFAA bila ya madaktari bingwa?
 
Itapendeza kama watarudi kwenye meza ya mazungumzo kwa ajili ya maslahi ya nchi.
 
Kufungwa kwa hospitali maanake hakuna huduma hata moja na hakuna mgonjwa hata mmoja. Muhimbili bado kuna huduma ndogo ndogo ambazo hazihitaji madaktari bingwa. Wote ni mashahidi hospitali ndogo tunazotibiwa mitaani zote zina madaktari bingwa?
 
Madaktari wamefikia hatua ya kuuza utu wao kwa madai ya fedha huku wakiacha wananchi wanakufa Hospitalini... kwa tulio waamini wa dini yoyote hakuna atakayeunga mkono hili... Hawa madaktari tunaishi nao uraiani na tunajua hadhi ya maisha yao, hawana shida kiasi cha kutufikisha katika hali hii ambayo hata hivyo suala lao liko kwenye mchakato. Madaktari msiangalie ya duniani tu... MUOGOPENI MUNGU!


Wanajamvi!
Mimi si daktari au mbunge ila ni mwananchi wa kawaida tu katika maisha ya kawaida sana!

Ninashindwa kuwaelewa wale wanaosema "MUUOGOPENI MUNGU" huku wakielekeza kauli hii kwa madaktari tu! Kwani anyepaswa kumuogopa Mungu ni daktari pekee na sio mafisadi wanaoimaliza nchi yetu kwa kula fedha za umma kiasi cha kusababisa watu kufanya kazi katika mazingira HATARISHI! Ninapata uchungu kwa kuona watu wanapoteza maisha, lakini hali hii haisababishwi na madaktari ila MAFISADI!

Kwa mtazamo wangu ieleweke kwa sasa taasisi yoyote pindi ikatokea wanafanyakazi katika mazingira hatarishi lazima mgomo utatokea. Siombei bali ikifikia nchi jirani inataka kuishambulia Tanzania kwa kipindi hiki, basi hata WANAJESHI nao watagoma kupigana kwani mazingira yao yatakuwa HATARISHI!

Sijui nani ana haki ya kutomuogopa Mungu katika nchi yetu hii ambayo watu wanajineemesha kwa rasilimali za umma?

Ndugu yangu KENGEMUMAJI! Sijapinga ulilosema ila nimeona nami nitoe yaliyomo moyoni mwangu.............................


PIGANGOMA
Nasikitishwa na mwenendo wa viongozi wa serikali....
 
Kwa kuwa hii ni hospitali kuu ya rufaa nchini hakuna huduma za rufaa sasa hivyo ni sawa kusema imefungwa.
Kufungwa kwa hospitali maanake hakuna huduma hata moja na hakuna mgonjwa hata mmoja. Muhimbili bado kuna huduma ndogo ndogo ambazo hazihitaji madaktari bingwa. Wote ni mashahidi hospitali ndogo tunazotibiwa mitaani zote zina madaktari bingwa?
 
Back
Top Bottom