Hospitali ya Rufaa Chato ni aibu na fedheha kwa Serikali, ipelekwe Biharamulo na Majengo yawe Chuo cha afya! Chuki dhidi ya Kagera ziishe

Yaani kwa akili ya kawaida utoke Shinyanga uende Chato badala ya Bugando Mwanza,au utoke Tabora uende Chato badala ya Ndala au Nkinga,utoke Musoma uende Hospital ya CHATO badala ya Bugando.
Kahama - Mwanza = 255km
Kahama - Chato = 211km
 
Hujitambui.
Huyu jamaa anaoneka

Ni mbaguzi sana kutoka tabora hadi chato ni karibu sana.

Mbona vitu vingi watu wa tabora wanachukua katoro ambapo kutoka katoro mpaka chato nauli 2000/ tu huyu jamaa atakuwa alikuwa fisadi subiri samia agenge vya kwenye uongozi wake hivi vya magufuli achane navyo tunahitaji tumpime nayeye ili tuone atajenga au ndo hivyo maana mafisadi wametoa macho hatari sana
 
Kisingino au Singino mkuu?!!!

nje ya mada kidogo, nasikia halmashauri ya Kilwa inataka kuhamishiwa Nangurukuru kutoka Masoko yalipo makao makuu sasa hivi, hii ni kweli? pia nasikia inataka kujengwa stendi pale ya wilaya hapo nangurukuru? nijuze haya kiongozi nitulie.
Mkuu, hii Miradi labda kwa huruma za Rais Samia. Mwenda zake Magufuli alisema kwenye mkutano wa hadhara kwamba tusahau sababu kubwa kwamba tulichagua Mbunge wa Upinzani. Kwamba hawezi wapa chakula watoto wa nje wakati wa kwake wanakufa njaa
 
Wivu umekujaa SANA UTAKUUA TU.

AFU SOMA VIZURI GEOGRAFIA YA MIKOA ULIYOITAJA AFU RUDIA UZI WAKO.
 
Kisingino au Singino mkuu?!!!

nje ya mada kidogo, nasikia halmashauri ya Kilwa inataka kuhamishiwa Nangurukuru kutoka Masoko yalipo makao makuu sasa hivi, hii ni kweli? pia nasikia inataka kujengwa stendi pale ya wilaya hapo nangurukuru? nijuze haya kiongozi nitulie.
Wananchi walitaka miradi ikamilike. Barabara ya Korosho: Kuwezesha Ujenzi wa barabara ya korosho (cashew ring road) – Nangurukuru – Liwale – Nachingwea – Masasi – Newala – Tandahimba – Mtwara – Lindi - Nangurukuru kutoka mapato ya ushuru wa korosho kwa kutumia mfumo wa “development finance” ili kufungua wilaya zinazolima korosho. Lakini kila kitu kimesimama

Tulijua baada ya vyeti hewa, Serikali itaunganisha Wilaya ya Liwale kwa kufungua barabara za Songea-Liwale na Liwale-Morogoro. Lakini sasa nasikia eti Wamarekani wataonunua korosho wameambiwa wajitolee kutengeneza barabara ili waweze fikia maligafi zote Lindi.

Kumbuka tunalipa tozo na kodi kama Arusha, Dar, Chato na Kiembe samaki.
 
Wananchi walitaka miradi ikamilike. Barabara ya Korosho: Kuwezesha Ujenzi wa barabara ya korosho (cashew ring road) – Nangurukuru – Liwale – Nachingwea – Masasi – Newala – Tandahimba ...
Sasa ushauri wako hapo ni upi?? Afu unasema wamarekani tena??
 
Hu
Sema tu ili wakati tunajenga hoja tujue kabisa una interest au hauna interest.
Isijekuwa unafanya attack kwa Mwenda zake kwa sababu unahisi hakuikumbuka Kagera kwenu
Huyu mleta mada ni mbinafsi sana , hivi ikijengwa Chato au kwingine ndani ya nchi hiii si bado ipo Tanzania? Kuna hospitali ngapi zilizojengwa hapa Tanzania ukaanza kuleta majungu yako hapa . Zunguka nchi nzima kumejengwa Mahospitali na zahanati kibao kila mikoa na wilaya . Au ulipotembea umeishia hapo Chato tu na Bukoba tu?
 
Yaani kwa akili ya kawaida utoke Shinyanga uende Chato badala ya Bugando Mwanza,au utoke Tabora uende Chato badala ya Ndala au Nkinga,utoke Musoma uende Hospital ya CHATO badala ya Bugando.
inatagemea nanuborq wa hudumq..mbona watu wanatoka.mwanza wanaenda kytibiwa Mgana hospil?
 
Hu

Huyu mleta mada ni mbinafsi sana , hivi ikijengwa Chato au kwingine ndani ya nchi hiii si bado ipo Tanzania? Kuna hospitali ngapi zilizojengwa hapa Tanzania ukaanza kuleta majungu yako hapa . Zunguka nchi nzima kumejengwa Mahospitali na zahanati kibao kila mikoa na wilaya . Au ulipotembea umeishia hapo Chato tu na Bukoba tu?
Huyo jama hafai
 
Hakuna Hoja uliyoileta hapo zaidi ya Ushuzi tu.
jamaa ameandika uzi kwa kuweka mbele maslahi yake na ya watu wa kwao huko kagera, anadai watu wa Shinyanga,Mwanza na Geita wana Bugando,haoni Bugando ilikua inahudumia watu wa lake zone yote hivo kuhelemewa
angejikita katika kuomba Hospitali ya rufaa huko kwao kagera lakini sio kuponda hiyo ya chato,nchi hii ni tajiri haishindwi kujenga hospitali za rufaa kila mkoa, tatizo ni viongozi wazembe wanapiga hela, sio vibaya hiyo hosp kuwepo hapo chato na sio vibaya kagera ikijengwa pia
 
Isikupe tabu sana mkuu as hata KIA na KMC ya kanda viko Kilimanjaro wakati ofisi zingine ziko Arusha makao makuu ya kanda kask. Hii nchi wako wanaopewa na wako wanaotafuta ..tujiulize tu mie na weye tuko kundi lipi hapo?
KIA ipo mpakani mwa Kilimanjoro and Arusha na Arusha ni mkoa na Kilimanjaro ni Mkoa vina hadhi sawa hakuna makao makuu ya kanda huku. KCMC hii hospitali sio ya Serikali bali ni mali ya KKKT wao woliijenga kilimanjaro kwa sababu zao wenyewe sio Serikali mfano wako hauna mashiko.
 
KIA ipo mpakani mwa Kilimanjoro and Arusha na Arusha ni mkoa na Kilimanjaro ni Mkoa vina hadhi sawa hakuna makao makuu ya kanda huku. KCMC hii hospitali sio ya Serikali bali ni mali ya KKKT wao woliijenga kilimanjaro kwa sababu zao wenyewe sio Serikali mfano wako hauna mashiko.
Hadhi ndo nini?
 
Hu

Huyu mleta mada ni mbinafsi sana , hivi ikijengwa Chato au kwingine ndani ya nchi hiii si bado ipo Tanzania? Kuna hospitali ngapi zilizojengwa hapa Tanzania ukaanza kuleta majungu yako hapa . Zunguka nchi nzima kumejengwa Mahospitali na zahanati kibao kila mikoa na wilaya . Au ulipotembea umeishia hapo Chato tu na Bukoba tu?
Ni kweli. Tungejenga hospitali zote za rufaa mpakani na Malawi so long as ziwe huu upande wa Ta zania hamna shida.
 
Nikikuuliza una akili sawa nitakuwa nimekosea!

Hujui kwamba Chato kuna Hospitali ya Wilaya ambayo ipo muda mrefu na hiyo ya Kanda ni Hospitali mpya inajengwa/imejengwa.

Nauliza maswali kama wanayoulizwa watu kwenye kesi inayoendelea ya Mbowe na wenzake.
Huku ndio naita kukurupuka at best.

Sina uhakika kama umesoma post yangu na kuilewa.

Kwa kifupi ni hivi hadhi ya Hospitali sio majengo ni huduma inayotolewa.

Hospitali ya kanda ina kila aina ya huduma (au karibu zote, maana kwetu kuna baadhi ya operation ni Muhimbili tu inaweza fanya) pamoja na hayo hospitali ya kanda ina kila aina ya daktari bingwa na ni University hospital.

Sasa hiyo hospitali inayojengwa Chato ambayo ni operation tayari imekidhi ivyo vigezo ya kuitwa hospitali ya kanda?

Vigezo vya huduma wanazotoa hapo ni vya hadhi ya hospitali ya wilaya ata kama kuna hospitali nyingine ya wilaya.

Ndio maana ukaambiwa mpango ni kuifanya iwe hospitali ya kanda, lakini binafsi nitashangaa kama wataendelea nao.

Chato kama eneo aina sifa ya kuwa na hospitali ya kanda not only it is not an epicentre kama mleta mada alivyosema hata kwa morale ya wafanyakazi.

Sasa sio unakurupuka na kuleta ujuaji wako, bila ya kuelewa post za wenzako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom