Wakuu heshima mbele.
Kwa masikitiko makubwa,
Na kwa haki yangu ya Kikatiba ya kutoa maoni.
Naomba kutoa mtazamo wangu juu ya huduma zitolewazo katika Hospitali ya Mwananyamala.
Kwa sasa limekuwa jambo la kawaida kusikia katika vyombo vya habari kuwa kuna mjamzito amepatwa na tatizo la kufariki wakati akitaka kujifungua au mtoto wake aliyejifungua kufariki.
Na mara nyingi chanzo cha vifo hivyo ni ukosefu wa huduma, kuchelewa kupatiwa huduma au kunyimwa huduma na Manesi kwa kukosa hela ya kutoa rushwa.
Kwa mtazamo wangu, tatizo hili limeendelea kukuwa siku hadi siku kwa sababu sisi kama jamii tumelifumbia macho huku ndugu zetu wakiendelea kupukutika kama vile sio binadamu.
Madaktari,Manesi na Wauguzi wa Hospitali hii wameshajihalalishia vitendo vyao vya kuuwa wajawazito na watoto wachanga na hivyo kuigeuza Hospitali hiyo kuwa ni MACHINJIO YA BINADAMU WASIO NA HATIA.
WanaJF, kwa kuwa kwa umoja wetu tumefanikiwa kukemea maovu mengi hapa nchini, ni rai yangu kuwaomba tuungane kwa pamoja kukomesha tatizo hili la WAZAZI KUUWAWA katika Hospitali hii kwa kulikemea na kulijadili OPENLY.