Hospitali ya AghaKhan Dar waanza kupima kisukari bure
Na Patricia Kimelemeta
HOSPITALI ya Aghakhan imeanza kupima wagonjwa wa kisukari ikiwa ni moja ya mpango wake wa kuwafikia wagonjwa katika jamii inayowazunguza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa mpango huo, Dk Jacob Shabani alisema wananchi wengi wanapata matatizo ya magonjwa yasiyoambukiza lakini
wanashindwa kwenda hospitali kupima.
Alisema kutokana na hali hiyo mpango huo utaweza kuwafikiwa wananchi wengi ambao wanasumbuliwa na ugonjwa huo, lakini wanashindwa kujitambua kwa sababu hawajapatiwa vipimo vya kiafya.
"Tumeamua kuanzisha mpango huo ambao tunaamini tutaweza kufanikiwa kwa kuwafikiwa wananchi wengi na kuwajengea tabia ya kwenda katika vituo vya afya kwa ajili ya kupatiwa matibabu, na ushauri,"alisema Dk Shabani.
Aliongeza kuwa mkakati wao ni kuwapima wagonjwa
zaidi ya 1,000 na kupatiwa ushauri nasaha juu ya kupunguza tatizo hilo. Shabani alisisitiza kuwa, mpango wao wa kuwapima wagonjwa utaendelea hadi mikoani katika hospitali zote za Agha Khan kwa ajili ya kuwapatia huduma hiyo wananchi wa mikoa hiyo.
Na Patricia Kimelemeta
HOSPITALI ya Aghakhan imeanza kupima wagonjwa wa kisukari ikiwa ni moja ya mpango wake wa kuwafikia wagonjwa katika jamii inayowazunguza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa mpango huo, Dk Jacob Shabani alisema wananchi wengi wanapata matatizo ya magonjwa yasiyoambukiza lakini
wanashindwa kwenda hospitali kupima.
Alisema kutokana na hali hiyo mpango huo utaweza kuwafikiwa wananchi wengi ambao wanasumbuliwa na ugonjwa huo, lakini wanashindwa kujitambua kwa sababu hawajapatiwa vipimo vya kiafya.
"Tumeamua kuanzisha mpango huo ambao tunaamini tutaweza kufanikiwa kwa kuwafikiwa wananchi wengi na kuwajengea tabia ya kwenda katika vituo vya afya kwa ajili ya kupatiwa matibabu, na ushauri,"alisema Dk Shabani.
Aliongeza kuwa mkakati wao ni kuwapima wagonjwa
zaidi ya 1,000 na kupatiwa ushauri nasaha juu ya kupunguza tatizo hilo. Shabani alisisitiza kuwa, mpango wao wa kuwapima wagonjwa utaendelea hadi mikoani katika hospitali zote za Agha Khan kwa ajili ya kuwapatia huduma hiyo wananchi wa mikoa hiyo.