Hospitali Kuu ya Rufaa Zanzibar Mnazi Mmoja shida iko wapi?

Emanueli misalaba

JF-Expert Member
Dec 12, 2016
1,109
1,648
Bila shaka hamjambo wana JF, bila kupoteza muda kama ambavyo kichwa cha habari kinacho jieleza niingie moja kwa moja kwenye kero hii.

Hospitali hii imekuwa ikilalamikiwa na watu wengi sana kutokana na huduma ambazo zinatolewa na wahudumu wake baadhi yao, kuwa wana maneno/ kauli mbaya kwa wagonjwa.

Mwaka jana mfanyakazi mwezangu alipata ajali akapelekwa hospitalini hapo, vipimo vya X- ray vilionyesha amevunjika kidole kidogo cha mkono wa kushoto, matokeo yake mkono mzima akafungwa P.O.P amekaa nalo karibu mwezi mzima, kwenda kutolewa mkono umebadilika rangi umekuwa na rangi kama ya blue.

Baada ya kutolewa alikataa kupata huduma tena kwenye hospitali hii ilibidi aende ya Private huko alifanyiwa operesheni ndogo ya kidole na baada ya wiki mbili akapona.

Mgonjwa mwingine alipekwa Mnazi Mmoja mwaka jana akiwa anatapika damu, alipelekwa Jumapili lakini hakupewa huduma yoyote hadi kesho yake alasiri tena mgonjwa baada ya kukasirika na kuwatolea maneno wahudumu ndipo wakamhudumia.

Mama mmoja mjamzito alihamishiwa hospitali ya Mnazi Mmoja, mwaka huu Mwezi wa Aprili ili akajifungue, alijifungua mapacha ambao umri wao miezi ilikuwa bado, watoto wale wote walifariki kwa sababu ya uzembe wa wahudumu wa afya.

Hospitali hii inalalamikiwa kuwatumia wanafunzi ambao wapo field ambao bado wanahitaji usimamizi wa karibu wa wenye ujuzi.

Kijana mmoja kaenda kwenye hospitali hii kwenye kitengo cha macho na masikio, anaambiwa tiba yake kutibiwa hospitalini hapo hadi mwezi wa kumi 2020 au aende hospitali ya binafsi ya Al-rahma akatajiwa siku ya kliniki kwa wagonjwa wa masikio hospitalini. Al-rahma na bei yake ya matibabu, jamani kweli Mnazi Mmoja hospitali kuu ya rufaa imwambie mgonjwa wa sikio asubirie matibabu miezi minne?

Au Dr huyu anapata asilimia fulani akipeleka wagonjwa kutoka Mnazi Mmoja kwenda Al-rahma? Malalamiko ni mengi mtaani kuhusu hospitali hii, hadi nina maswali mengi sipati majibu.
1. Hivi hospitali ya rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar ina Daktari mkuu?
Kama inaye anajua matatizo ya wafanyakazi walio chini yake, kachukua hatua zipi?

2. Je hospitali hii ina Management (Uongozi)? Kama ina uongozi wahudumu wao wenye kauli chafu kwa wagonjwa wanazijua?

3. Je Waziri wa Afya Zanzibar anajua malalamiko ya wagonjwa wanayopitia?
Kama anajua kachukua hatua zipi?
Swali langu kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayajua matatizo ya baadhi ya wahudumu wa hii hospitali?

4.Je kwenye hii hospitali hamna mashushushu wa kuwasilisha taarifa sehemu husika?

5. Je wengi wao madaktari wa Mnazi Mmoja sifa za kuwa kwenye kuajiriwa wamekidhi au wameingizwa wakiwa CV hazitoshelezi?

Hawa wafanyakazi kuwa na kauli mbaya na uzembe wa aina mbali mbali kwani wanafanya kazi bure, kwani wanafanya kazi ya kujitolea, hawalipwi mishahara ambayo ni kodi ambazo tunakatwa sisi wananchi?
Nitoe ombi kwa Rais mpya Serikali mpya ijayo Hospitali ya rufaa Mnazi Mmoja waitupie darubini na wafanye mabadiliko mbalimbali na ufuatiliaji kwenye hospitali hii ikiwezekana na safari za kuwashtukiza kwenye hospitali hii, mbona kipindi Juma Haji Duni akiwa waziri wa afya walinyooka?

Hospitali ina majengo mazuri, vifaa vizuri na vya kisasa lakini inaangushwa na wafanyakazi wazembe wachache.
 
4.Je kwenye hii hospitali hamna mashushushu wa kuwasilisha taarifa sehemu husika?

Wahitimu wa zile kambi za Janjaweed ndio hupewa kazi pale kama ahsante kwa kuisaidia CCM kuiba kura.

Wengi wa waajiriwa ni watoto wa wakubwa, sifa hazizingatiwi sana pale.

mimi nilimpeleka mwanangu, alianguka na kupoteza fahamu, kumpeleka pale katiwa drip na kuruhusiwa, nilipo lalamika akatokea Dr. mmoja wa kigeni akaniongelesha kwa kimombo nikamjibu, akawa interesting na mimi.

Akaniuliza tatizo la mtoto nikampa lile Book la Daktari, akamuita yule aliyeniandikia dawa akamwambia huyu lazima afanyiwe CT- Scan, ndio akniandikia kipimo kile kisha akaniambia Mnazi mmoja ni mbovu uende Global, bei kule nadhani ni laki 400,000 nikashindwa nikaondoka na mwanangu nikaishia kumshukuru yule Dr. Mgeni kwa kuonesha kujali.

Kuja kuulizia nikaambiwa CT-Scan ni nzima ila jamaa wanapiga dili na Global kwa kupata commision
 
Wahitimu wa zile kambi za Janjaweed ndio hupewa kazi pale kama ahsante kwa kuisaidia CCm kuiba kura.
Wengi wa waajiriwa ni watoto wa wakubwa ,sifa hazizingatiwi sana pale.

mimi nilimpeleka mwanangu, alianguka na kupoteza fahamu, kumpeleka pale katiwa drip na kuruhusiwa, nilipo lalamika akatokea Dr. mmoja wa kigeni akaniongelesha kwa kimombo nikamjibu ,akawa interesting na mimi.

Akaniuliza tatizo la mtoto nikampa lile Book la Daktari, akamuita yule aliyeniandikia dawa akamwambia huyu lazima afanyiwe CT- Scan, ndio akniandikia kipimo kile kisha akaniambia Mnazi mmoja ni mbovu uende Global, bei kule nadhani ni laki 400,000 , nikashindwa nikaondoka na mwanangu nikaishia kumshukuru yule Dr. Mgeni kwa kuonesha kujali.

Kuja kuulizia nikaambiwa CT-Scan ni nzima ila jamaa wanapiga dili na Global kwa kupata commision

Ndugu yangu Battawi hii inazidi kudhihirisha uongozi wa hospitali ya Mnazi Mmoja ni Jipu linahitaji kutumbuliwa.
Ombi langu Serikali ijayo Rais aweke Waziri kwenye wizara ya Afya asiye na haya, mwenye weledi, mzalendo, mchakarikaji na rais jicho lake liwe kwenye hospitali hii kuna madudu mengi sana Mnazi Mmoja, wafanyakazi wa pale wanapaswa kufanyiwa uhakiki wa vyeti vyao, uongozi wa pale ufumuliwe utengenezwe upya.
 
Mkuu usiumie sana ndio CCM hiyo mbona tushaizoea,

Kigezo kikuu cha kazi pale mnazi mmoja nikuwa uwe kada wa CCM. Na ukishakua kada wa CCM unaweza mtukana yoyote kwenye eneo la kazi na wala pasiwe na tatizo. na wala huhitaji coalification nzuri kuajiriwa

Wagonjwa wengi sana wameshapoteza uhai wao kizembe na wengine kupata vilema vya Maisha kwenye ile Hospital. Na si ile tu vituo vya afya vyote vya serekali Zanzibar ndivo vilivo.

Tuungane kuiondoa CCM madarakani ila tuzimalize hizi shida tena nyengine za kipuuzi zinazo tuandamaa.
 
Huwa nashindwa kuelewa ni kwanini Hawa watoa huduma kwa wananchi wanakuwa na roho mbaya hivi
Azarel umeona, halafu sasa si kwamba wanafanya kazi bure, wanalipwa mishahara ambayo ni kodi za wananchi, sasa sijui ni madaktari ambao hawa wito wa kidaktari baada ya kukosa kazi udaktari ukawa ni plan B?

Rais ajaye ashughulikie uongozi wa Hospitali hii
 
Mkuu usiumie sana ndio CCM hiyo mbona tushaizoea,

Kigezo kikuu cha kazi pale mnazi mmoja nikuwa uwe kada wa CCM. Na ukishakua kada wa CCM unaweza mtukana yoyote kwenye eneo la kazi na wala pasiwe na tatizo. na wala huhitaji coalification nzuri kuajiriwa.
Wagonjwa wengi sana wameshapoteza uhai wao kizembe na wengine kupata vilema vya Maisha kwenye ile Hospital. Na si ile tu vituo vya afya vyote vya serekali Zanzibar ndivo vilivo.

Tuungane kuiondoa CCM madarakani ila tuzimalize hizi shida tena nyengine za kipuuzi zinazo tuandamaa.
Chadema na CUF huwa wanaajiriwa wapi?
 
Azarel umeona, halafu sasa si kwamba wanafanya kazi bure, wanalipwa mishahara ambayo ni kodi za wananchi, sasa sijui ni madaktari ambao hawa wito wa kidaktari baada ya kukosa kazi udaktari ukawa ni plan B?

Rais ajaye ashughulikie uongozi wa Hospitali hii
Huwa nashindwa kuelewa ni kwanini Hawa watoa huduma kwa wananchi wanakuwa na roho mbaya hivi

Tatizo kubwa linaanza kwenye mazingira ya Kuajiriwa. CCM sikuzote wamekua wakitengeneza mazingira kuaminisha kama unapoajiriwa kwenye kazi za utumishi wa umma kuwa kama wamekusaidia, hivo uendelee kuwshukuru na kuwatii kwa kuwa wao wamekupa ajira.
Sasa hapo muajiriwa hmuheshimu mwana CCM tu, wengine wote huwaona takataka
 
na ndio CCM wanayoipandia majukwaa kila siku wakijisifu kuwa wanatoa matibabu bure
Na mfumo wenu huko pia inafaa muubadili.Kama hospitali ya daraja la juu ya serikali inakuambia kachukue kipimo fulani hospitali ya private basi hali sio nzuri huko.Kama mnaona tatizo ni serikali ya chama tawala huko basi sio mbaya mkakiweka chama kingine madarakani.Ila kama tatizo ni mfumo wenu wa maisha ya kila siku basi hapo hata mkibadili serikali mambo yatakuwa yaleyale tu.Nimesema hivyo maana nimeona huduma za afya huku na huko ni tofauti ilhali chama kilichopo madarakani ni kilekile.
 
Na mfumo wenu huko pia inafaa muubadili.Kama hospitali ya daraja la juu ya serikali inakuambia kachukue kipimo fulani hospitali ya private basi hali sio nzuri huko.Kama mnaona tatizo ni serikali ya chama tawala huko basi sio mbaya mkakiweka chama kingine madarakani.Ila kama tatizo ni mfumo wenu wa maisha ya kila siku basi hapo hata mkibadili serikali mambo yatakuwa yaleyale tu.Nimesema hivyo maana nimeona huduma za afya huku na huko ni tofauti ilhali chama kilichopo madarakani ni kilekile.


Mfumo wa Maisha upi mkuu wakati nchi tokea ipate uhuru inatawaliwa na CCM!

Na usifananishe ccm ya Bara na Zanzibar, Zanzibar ndio imeoza kabisa.
 
Mkuu Zanzibar bila ya kuwa na kadi ya CCM huna ajira kwenye Serekali.
Nahio kadi haitoshi pia unachunguzwa family background.
Ni.kweli ila..wapinzani.na vizazi vyao wapo tena wengi tu..kiasi kwamba wanatuhumiwa kufanya madudu ili kuiumiza serikali!

Kweli serikali ijayo ifumue pale..mpaka. ..Hamadi..naye ni waziri wa afya na katokea upinzani ila ndio yale yale !!
 
Back
Top Bottom