ungonella wa ukweli
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 4,210
- 555
Habarini wana jf,
Hakika miongoni mwa wananchi wa kuigwa na kupigiwa mfano ni wa jimbo la Singida Mashariki, wametuchagulia mbunge mzalendo, mwenye uelewa wa mambo na pia mwenye uchungu na taifa letu, huyu si mwingine bali ni ndugu Tundu lissu, binafsi nawaonea wivu sana wana Singida Mashariki, Lissu ni jasiri na hana unafiki.
Tungekuwa na kina Lissu wengi bungeni taifa letu lingenyooka kwa maendeleo na pia lingekuwa la kupigiwa mfano Afrika Mashariki. Ingawa wabunge wengi hasa wa CCM wanamuona kama mbunge mkorofi, watanzania wengi mitaani wanamuona lissu kama jasiri na mkombozi wao! Lissu akiwa bungeni kweli utaiona kazi yake, hana muda wa kusinzia kama kina john komba na wengineo.
Hongereni tena wana Singida Mashariki, tutaiga mfano wenu mwaka 2015!
Hakika miongoni mwa wananchi wa kuigwa na kupigiwa mfano ni wa jimbo la Singida Mashariki, wametuchagulia mbunge mzalendo, mwenye uelewa wa mambo na pia mwenye uchungu na taifa letu, huyu si mwingine bali ni ndugu Tundu lissu, binafsi nawaonea wivu sana wana Singida Mashariki, Lissu ni jasiri na hana unafiki.
Tungekuwa na kina Lissu wengi bungeni taifa letu lingenyooka kwa maendeleo na pia lingekuwa la kupigiwa mfano Afrika Mashariki. Ingawa wabunge wengi hasa wa CCM wanamuona kama mbunge mkorofi, watanzania wengi mitaani wanamuona lissu kama jasiri na mkombozi wao! Lissu akiwa bungeni kweli utaiona kazi yake, hana muda wa kusinzia kama kina john komba na wengineo.
Hongereni tena wana Singida Mashariki, tutaiga mfano wenu mwaka 2015!