Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,037
- 22,728
Nawapa hongera sana Wabunge wa CCM chini ya kamanda wao Spika Makinda. Mshikamano wanaouonesha hivi sasa ndio unaotakiwa kwani unaondoa kabisa matumaini ya Watanzania kuwa anaweza akatokea mkombozi miongoni mwao. Kikao hiki cha Bunge kimetuthibitishia kuwa ndani ya CCM hakuna wa kumnyooshea mwingine kidole kwani wote ni wazi wameoza na anaedai vinginevyo ni mnafiki na huenda kaoza zaidi.
Sitaki tena kusikia eti fulani na fulani ndani ya CCM ni afadhali, la hasha, hao wanaoonekana afadhali ndio hatari zaidi na hivi sasa yatubidi tuanze kuwaanika ili wananchi wakae nao mbali ! Ukweli kuwa CCM imegeuka na kuwa kimbilio la wezi na mafisadi umedhihirika hivi sasa kuliko wakati wowote mwingine katika historia ya Tanzania. Wazalendo, kwa matendo ya wabunge wa CCM, njia ya kuelekea mageuzi yabakia sasa nyeupee !
Kwa kuanzia lazima sasa tuwataje kwa majina yao waliodaiwa wapiganaji ndani ya CCM kumbe ni mazimwi wala watu na wasaliti wakubwa waliovaa ngozi ya kondoo. Mimi leo naanza na Spika wa zamani Samweli Sitta, historia ya utumishi wake siku za nyuma ? alivyotetea matumizi makubwa ya ofisi ya Spika ? matibabu na kodi kubwa ya nyumba ? mnakumbuka alivyozima Richond ? alivyowaka mkewe alipotuhumiwa kwa rushwa ? ni mengi !
tuendeleee............
Sitaki tena kusikia eti fulani na fulani ndani ya CCM ni afadhali, la hasha, hao wanaoonekana afadhali ndio hatari zaidi na hivi sasa yatubidi tuanze kuwaanika ili wananchi wakae nao mbali ! Ukweli kuwa CCM imegeuka na kuwa kimbilio la wezi na mafisadi umedhihirika hivi sasa kuliko wakati wowote mwingine katika historia ya Tanzania. Wazalendo, kwa matendo ya wabunge wa CCM, njia ya kuelekea mageuzi yabakia sasa nyeupee !
Kwa kuanzia lazima sasa tuwataje kwa majina yao waliodaiwa wapiganaji ndani ya CCM kumbe ni mazimwi wala watu na wasaliti wakubwa waliovaa ngozi ya kondoo. Mimi leo naanza na Spika wa zamani Samweli Sitta, historia ya utumishi wake siku za nyuma ? alivyotetea matumizi makubwa ya ofisi ya Spika ? matibabu na kodi kubwa ya nyumba ? mnakumbuka alivyozima Richond ? alivyowaka mkewe alipotuhumiwa kwa rushwa ? ni mengi !
- Sita
- Mwakyembe
- Nape
- Kilango
- Ole Sendeka
tuendeleee............