Hongereni TBC kwenda Uganda kuongeza ujuzi wa uandaaji wa vipindi

MANILABHONA

JF-Expert Member
Apr 1, 2015
462
348
Nimefurahi kuona TBC walivyofanya uamuzi wa kwenda Uganda kujifunza namna ya uandaaji wa vipindi vya TV na urushaji wa matangazo. Kongole kwao.

Kwa kweli ilifika mahali watanzania walio wengi hawapendi kuangalia televisheni za humu ndani kutokana na kukosa ubora wa vipindi, kukosa maudhui.

Baadhi ya televisheni zikageuka kuwa majukwaa ya kisiasa au ya mikutano ya kisiasa. Wengi tulijiuliza hivi waandaaji wa vipindi vyetu wanabahatika kuangalia televisheni nyingine hata za hapo kenya tu au uganda au hata rwanda. Sasa TBC mkirudi murudi mkiwa mmejifunza siyo 'business as usual'.

Mnatia aibu, aibu, aibuuuuuu! Fanyeni tathmini ya vipindi mnavyorusha wenyewe si kwa kuuliza watu. watanzania hatuna kawaida ya kukueleza ukweli hata kama tunaona unaharibu.

Wanaoangalia tv za humu ndani wengi ni wale ambao hawana namna, TBC kipindi pekee huangaliwa ni Zilipendwa, pengine na taarifa ya habari.
 
Mm bado nina tatizo na MD wa TBC Dr. RIOBA, yuko kisiasa zaidi na hata akileta mjadala anauleta in a way usikwazane na viongozi wa serekali na mtu akichangia kama yeye hapendi huwa anamkatiza.

Sipendi utendaji wako kama unanisikia ubadilike aya uondoke mana kazi ya uandishi wa habari km ilivoelezea ni kuelimisha na elimu haiji kwa kusifu pekee.

Kujua changamoto ndo kuelimisha na kusolve tatizo. Pia kama muda ni ndogo ekeni mda mrefu ili mijadala ilete Tija au la mjadala itakuwa hauna mana. Nakala kila wakati hazina mana ekeni mijadala ya maan kwa mda toshelevu
 
Michuano ya euro inaanza June 11 wamejipangaje
Kenya KBC Zanzibar ZBC huwa wanaonyesha mpira sana, kumbuka kwa mfano Simba walipokuwa South Africa dhidi ya Kaizer Chiefs KBC walionyesha mechi, TBC hata mechi za timu ya taifa wameshindwa, Uganda nao hakuna cha kujifunza kule. Waende Kenya.
 
Back
Top Bottom