Majs
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 229
- 481
Habari waungwana,
Binafsi huwa naamini TBC 1 na TBC Taifa huwa na vipindi vingi vizuri ukiacha habari na baadhi ya vipindi vya kisiasa ambayo bado inajadilika lakini pia kuwa chombo cha serikali ni rahisi kuwa upande uliopo kwani sehemu nyingi duniani chombo cha habari cha taifa(Serikali) huwa kinasimama upande wa serikali.
Pamoja na kupenda vipindi vyake vingi kuanzia kilimo, biashara, technolojia, lugha na Zaidi TBC nahisi ndio televisheni yenye makavazi mengi na bora namba moja nchini, vipindi vinatengezwa popote Tanzania na vingine ukiangalia unaona gharama ya kuvitengeza ni kubwa kuliko matarajio jinsi watakavyonufaika hasa vinavyoelimisha.
Pamoja na yote lakini muonekano ulikuwa unachosha mpaka kukatisha tamaa. Ukifungua TV nyingine muonekano mzuri lakini mwendo wa muziki na burudani kwa ujumla, wengine mahubiri na mawaidha.
Karibuni naona muonekano bora wa TBC 1 kulinganisha na awali, angalau picha imekuwa angavu na haichoshi kama zamani. Naamini wataendelea kuboresha ili walingane na umri wao kwenye tasnia ya habari hasa luninga, nyingi zilizokuja miaka ya karibuni ziliwapita tena nyingine zikionekana kuwa na mitaji midogo mpaka unajiuliza wanakwama wapi. Mna gari la kisasa la matangazo bora kuliko yote nchini lakini ikija kwenye mubashara, Azam, ITV na wengineo wanawaacha mbali sana.
Hongereni lakini boresheni Zaidi.
Binafsi huwa naamini TBC 1 na TBC Taifa huwa na vipindi vingi vizuri ukiacha habari na baadhi ya vipindi vya kisiasa ambayo bado inajadilika lakini pia kuwa chombo cha serikali ni rahisi kuwa upande uliopo kwani sehemu nyingi duniani chombo cha habari cha taifa(Serikali) huwa kinasimama upande wa serikali.
Pamoja na kupenda vipindi vyake vingi kuanzia kilimo, biashara, technolojia, lugha na Zaidi TBC nahisi ndio televisheni yenye makavazi mengi na bora namba moja nchini, vipindi vinatengezwa popote Tanzania na vingine ukiangalia unaona gharama ya kuvitengeza ni kubwa kuliko matarajio jinsi watakavyonufaika hasa vinavyoelimisha.
Pamoja na yote lakini muonekano ulikuwa unachosha mpaka kukatisha tamaa. Ukifungua TV nyingine muonekano mzuri lakini mwendo wa muziki na burudani kwa ujumla, wengine mahubiri na mawaidha.
Karibuni naona muonekano bora wa TBC 1 kulinganisha na awali, angalau picha imekuwa angavu na haichoshi kama zamani. Naamini wataendelea kuboresha ili walingane na umri wao kwenye tasnia ya habari hasa luninga, nyingi zilizokuja miaka ya karibuni ziliwapita tena nyingine zikionekana kuwa na mitaji midogo mpaka unajiuliza wanakwama wapi. Mna gari la kisasa la matangazo bora kuliko yote nchini lakini ikija kwenye mubashara, Azam, ITV na wengineo wanawaacha mbali sana.
Hongereni lakini boresheni Zaidi.