Hongereni sana Law School of Tanzania kwa kulinda ubora wa fani ya sheria hapa Nchini

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,671
40,913
Kwa moyo wa dhati nipende kuwashukuru watendaji wote wa Law School of Tanzania (shule ya sheria ) kwa kuzingatia weledi katika kufundisha na hatimaye kutoa wanasheria ambao watatumika serikalini pamoja na sekta binafsi.

Napenda nikiri wazi kabisa kwamba shule hii ni moja wapo ya taasisi chache za Serikali zinazozingatia weledi.

Watendaji wake hawafungwi na jina la mwanafunzi wala uwezo wake kiuchumi.

Wanazingatia kujiweka mbali na ukaribu na wanafunzi utaopelekea kutoa upendeleo katika usahihishaji.

Wanazingatia mno ubora wa mwanafunzi katika kutoa kile alicho nacho kichwani kwake.

Nawaomba wasiache hata mara moja ubora huu kwani kwa kufanya hivyo wataliangamiza Taifa kwa kutoa wanasheria wasiokuwa na uwezo hivyo kuharibu taaluma ya sheria.

Mungu aendelee kuwatia nguvu kwa kusimamia taaluma zenu kwa manufaa ya Taifa.
 
Mnatuchanganya, mwingine ameandika siasa chafu za law shool.

Masaa 17 baadae unakuja wewe na counter thread ya kuwaambia hongereni. Sisi tusioyajua ya ndani, tushike lipi?
 

Attachments

  • JamiiForums609741434.jpg
    JamiiForums609741434.jpg
    17.8 KB · Views: 9
Pongezi za dhati kwa uongozi na watendaji law school ni moja ya shule bora kwa sasa kutokana na kuwa na maadili ya kiutendaji tofauti ba vyuo au shule nyingine ukifaulu law school utakuwa wakili bora nchini

Watendaji wa law school hawana upendeleo kwa yoyote toka ufundishaji utungaji wa mitihani usahishaji na kuna bodi ya kuchunguza hatua zote hizi kuhakikisha hakuna mwanafunzi aliyeonewa au kupendelewa

Naiopongeza sana bodi ya shule uongozi watendaji na wizara utaratibu wa law school uigwe na vyuo vingine.
 
Mleta mada nini kimekufanya uje na huu uzi, sio umeona malalamiko yamezidi ndio maana? Naamini utakuwa umesoma gazeti la Mwananchi la leo, wengi mno wanafeli.

Sioni sababu kwanini wanafunzi wengi wafeli kiasi hicho, ni either walimu ni incompetent, au kama ni competent, basi wanawafelisha makusudi hao wanafunzi, na kama muda wa masomo ni mfupi wauongeze, lakini sio huu utapeli wanaoufanya wa kula bure ada za wanafunzi.

Sijawahi kuona shule inayosifiwa kwa kufelisha wanafunzi wengi hapa duniani zaidi ya hiyo Law School, sifa yao kuu imekuwa ni kufelisha, na ajabu wajinga mnawapongeza.
 
Uliyeleta mada hii una tabia ya kusifu na kuabudu serikali ya kijani. A.K.A chawa wa kijani. Tunakujua.

No surprise, hujaweza kukemea vitendo viovu hapo LST kama rushwa na upendeleo. Vipo sana tu.

Umejikita kusifia blindly bila ku reason kama msomi. Kweli ukiwa lumumba fc akili unaiacha mlangoni.
 
Masahihisho:
Law school haitoi wanasheria bali inatoa mawakili.
Watu kama nyie ndio mnaofeli halafu mnasingizia chuo.

Law school inatoa wanasheria wenye sifa ya kuwa mawakili.

Haitoi mawakili.

Anayetoa uwakili ni Jaji Mkuu.

Ukifaulu Law School, bado hauwi wakili moja kwa moja , lazima utume maombi kwa jaji mkuu ambaye atakuita kukufanyia interview baada ya muda wa mapingamizi kupita.

Unaweza ukafaulu law school na usiapishwe kuwa wakili kama jaji mkuu atakubaliana na mapingamizi yaliyetwa juu yako.

Hivyo Law School haitoi mawakili bali wanasheria wenye sifa ya kuwa mawakili.
 
Back
Top Bottom