Hongereni sana itv, shame up you tbc.

Sharp lady

Senior Member
Feb 23, 2011
129
13
Ni kwa muda mrefu sasa TBC kama chombo cha serikali cha habari kimeshindwa kabisa kutii kiu ya watazamaji wao na si kwakutokujua wanafanya nini ila kwa makusudi makubwa mnabana au hamtoi kabisa taarifa za msingi na kwa coverage yakutosha kumwezesha mtazamaji kuelewa na kujivunia chombo hiki cha taifa letu. Kwa ushauri tu hiyo kauli mbiu yenu ya ukweli na uhakika ni bora muifutilie mbali kwani hamuitendei haki, mnachagua nini cha kutangaza na kwa manufaa ya nani mnapenda sana kuruka habari za msingi hasa zile zinazolihusu taifa na jamii moja kwa moja, hebu igeni japo kidogo kutoka kwa ITV kwa sababu nikiwaambia mfanye hata nusu ya ufikishaji habari kwa kiwango na ubora kama wafanyavyo BBC hamuwezi kwani hamtaweza kuwafunika vizuri wale muwapendao. ITV inafanyakazi kihalali unaangalia taarifa mpaka unaifurahia unaelewa inahusu nini na point za msingi zote unazipata wanajua kupangilia matukio yao ipasavyo. Hongereni sana ITV mnafanyakazi nzuri sana mko up minute na mnatekeleza wajibu wako ipasavyo. TBC jirekebisheni mnakoenda siko kama huo usiku wenu wa habari ndo kabisa hamna kitu. Watazamaji tunataka taarifa za kina na upminute ndiyo maana watu wanalipia CNN/BBC n.k wapate kupata taarifa ipasavyo. Mnashindwa hata na chipukizi Mlimani TV wenye coverage ndogo??? vijana wanakupa taarifa mpaka unatamani wangekuwa wanawafikia hata nusu ya Tz. TBC fanyeni mabadiliko ya haraka nyie msijivue gamba bali mjitoe ngozi kabisa alafu muache UPENDELEO. Acheni nakutengeneza TBC kibao zisizokidhi haja imarisheni hiyo 1 kwanza. Good day.
 
na japo kwa kupotezea kwa kuweka habari motomoto mwishoni,taarifa inakuwa haileti maana wala mtiririko! mfano naibu spika anasema wabunge upinzani waoneshe mfano wa kukataa posho na mtangazaji anakenua meno badala ya kuuliza walau kama wakishafanya hivyo wabunge wa ccm tutegemee wafanye nn?tunabakia kumalizia kazi ya journalists kwa kujibishana na tv! aibu zenu tbc1,wakati mwingine mjikakamue bwana,hata kashfa za mengi itv huzionesha!
 
Ndiyo maana mashirika yetu mengi ya serikali yamekufa kwa kutofuata misingi ya weledi. Hii ni shida sana.
 
ITV, Channel Ten, Mlimani TV nA sTAR tv, zinafanya vizuri hasa katika mambo yahusuyo jamii na kupigania haki za wanyonge kwa kuonyesha habari na kuielewa na hasa zile habari tata ziwahusuzo wanasiasa wa upinzani.
Uanahabari ni taaluma isiyoheshimika Tanzania kwa sababu hizi za kama wafanyazo TBC na vyombo kama Rai, uhuru, Clouds, wakati wengine wanatekeleza taaaluma zao wanatishiwa kuuwawa na hata kujeruhiwa wengine ndio wanatumika kama ngazi na hutumika kwa stahili ya Diapers au toilet
 
daa! umelenga! utadhani ni chombo cha chama sio umma! nahisi watangazaji wa pale nao hawapo makini. nilishaisusa hii tv
 
na japo kwa kupotezea kwa kuweka habari motomoto mwishoni,taarifa inakuwa haileti maana wala mtiririko! mfano naibu spika anasema wabunge upinzani waoneshe mfano wa kukataa posho na mtangazaji anakenua meno badala ya kuuliza walau kama wakishafanya hivyo wabunge wa ccm tutegemee wafanye nn?tunabakia kumalizia kazi ya journalists kwa kujibishana na tv! aibu zenu tbc1,wakati mwingine mjikakamue bwana,hata kashfa za mengi itv huzionesha!

Mdau umesema kweli wanaiaibisha sana taaluma ya uanahabari/uwandishi hata kupangilia matukio wanashindwa? angalia kama kipindi cha usiku wa habari baadaya ya kumulika issue za msingi kwa umakini wao wanawahi taarifa hoi zisizonamvuto daa kweli kazi yakulindana ngumu.
 
Shida ya kufanya kazi kwa maagizo ya waliokuweka

Tena wakiwa waliokuwa giza wana akili kidunchu na unaeagizwa unamzidi lakini kwa sababu ya njaa unafanya kazi huku brain yako ikiwa invisible.
 
daa! umelenga! utadhani ni chombo cha chama sio umma! nahisi watangazaji wa pale nao hawapo makini. nilishaisusa hii tv

utadhani hawalipwi na kodi zetu kazi kupaka wanja na kuchekacheka tu cha maana hakionekani.
 
habari zenye tija na maslahi kwa taifa siku hizi wanaita uchochezi....
 
ITV, Channel Ten, Mlimani TV nA sTAR tv, zinafanya vizuri hasa katika mambo yahusuyo jamii na kupigania haki za wanyonge kwa kuonyesha habari na kuielewa na hasa zile habari tata ziwahusuzo wanasiasa wa upinzani.
Uanahabari ni taaluma isiyoheshimika Tanzania kwa sababu hizi za kama wafanyazo TBC na vyombo kama Rai, uhuru, Clouds, wakati wengine wanatekeleza taaaluma zao wanatishiwa kuuwawa na hata kujeruhiwa wengine ndio wanatumika kama ngazi na hutumika kwa stahili ya Diapers au toilet

nakuunga mkono sana mdau kama star tv utadhani wanawaandishi kila kona yaani wana taarifa nzuri na tena ukakuta tukio wameliwahi utafurahi mwenyewe sasa hawa wenzetu na accessibility yote waliyonayo bado hawaonekaniki poor TBC
 
Wao kazi yao ni kujipendekeza kurusha habari za Citizen tv au KTN kama zilivyo ilhali Citizeni huwa hawarushi za kwao, sijui hazina kwaliti.
 
Mdau umesema kweli wanaiaibisha sana taaluma ya uanahabari/uwandishi hata kupangilia matukio wanashindwa? angalia kama kipindi cha usiku wa habari baadaya ya kumulika issue za msingi kwa umakini wao wanawahi taarifa hoi zisizonamvuto daa kweli kazi yakulindana ngumu.
Unajua kuna miaka ambayo Taifa lilipata Graduater fake miongoni mwao nadhani ni hao watumishi wa KUFANYA KAZI KWA MAAGIZO NA SIO KAMA TAALUMA.
 
Unajua kuna miaka ambayo Taifa lilipata Graduater fake miongoni mwao nadhani ni hao watumishi wa KUFANYA KAZI KWA MAAGIZO NA SIO KAMA TAALUMA.

Nimeipenda hii, inaonyesha kuna haja ya kutibu kuanzia mizizi kabisa na huwenda nusu yao wako pale waka pollute na wale wazuri wakakutana tena na maagizo wanayopewa ndo wakajikuta hawana direction kabisa mradi siku ipite. Wanaitaji kuoshwa ni aibu kubwa sana kwa taifa.
 
ITV kwenye kupitia magazeti mtoeni ahmed segule hajui kabisa kuongoza kipindi cha mapitio ya magazeti hajifunzi makosa kila siku anarudia rudia makosa anaonyesha kama mawazo hayapo hapo kwenye hiyo shuguli aliyopewa anafikiria kungine anataka kumaliza haraka aondoke juzi anasema mbowe msemaji wa kambi ya upinzani na sio hiyo tu mara nyingi anakosea na hachambui magazerti kwa ufasaha na akionyesha gazeti kwenye kamera ili sisi watazamaji tuone anaonyesha kama vile hataki tusome kilichoandikwa, joyce mhavile kama unasoma hapa jf tekeleza hilo, channel 10 wanajitahidi sana kwenye mapitio ya magazeti pongezi channel 10
 
Back
Top Bottom