Hongereni sana CHADEMA kwa kukataa kushiriki Mkutano wa TCD, mmelinda heshima yenu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,369
217,426
Nikiwa kama Raia wa Kawaida wa Tanzania nachukua nafasi hii kuipongeza Chadema kwa kukataa kushiriki Mkutano ulioiitwa wa wadau wa siasa ulioandaliwa na TCD , hii ni kwa sababu Mkutano huo pamoja na kuhudhuriwa na Rais wa nchi lakini HAUKUWA NA AJENDA , wala hata wajumbe wake hawakujua hata wanachoenda kujadili , ni kama waliburuzwa tu ili kukamilisha malengo ya waandaaji .

Wala hakuna mjumbe aliyehudhuria mkutano huo ambaye anaweza kutoka hadharani na kusema kilichojadiliwa akaeleweka , mpaka naandika hapa bado ni MARUFUKU KWA VYAMA VYA SIASA KUFANYA MIKUTANO YA HADHARA wala MAANDAMANO YA AMANI , miaka ya nyuma baada ya Mwl Nyerere kugundua umuhimu wa Demokrasia , aliwahi kuwaambia viongozi wenzake na wananchi kwamba CHAMA CHA SIASA NI MABARABARANI NA MAJUKWAANI , Kukataza harakati za kisiasa kwa vile ccm haina ajenda, haikubaliki na wala haisaidii chochote kile , hata Jakaya Kikwete aliwahi kuwaasa wanaccm wenzake .

FB_IMG_1574277425198.jpg


Ulikuwa ni mkutano wa kusikiliza hotuba za ufunguzi na zingine hotuba za kejeli kutoka kwa Dr Mahera , mwanaccm ambaye alishirikiana kwa 100% na Dr Magufuli kuvuruga uchaguzi wa 2020 kwa udi na uvumba , ikiwemo kufanya utekaji na mauaji ya wagombea na wafuasi wa vyama vingine , yaliyotokea Pemba , Lindi na kwingineko bado hayajasahaulika , Wala kikao hicho kilichokosa ajenda HAKINA HATA MAAZIMIO YOYOTE , ni heri hata kikao cha harusi ambako mwishoni kunaandaliwa hata zawadi ya bwana harusi , hiki kilikuwa kikao cha hotuba tu , anayejua ajenda zilizojadiliwa ama hata maazimio yake atuwekee hapa tujadili .

Ajenda kuu ya KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI haikugusiwa hata chembe , hizi ndio ajenda za nchi zinazoweza kuondoa maloloso yote ya akina Mahera na Kaijage na kuleta mwanzo mpya nchini , bla bla zozote hazitasaidia chochote .

Itaendelea ......
 
Nikiwa kama Raia wa Kawaida wa Tanzania nachukua nafasi hii kuipongeza Chadema kwa kukataa kushiriki Mkutano ulioiitwa wa wadau wa siasa ulioandaliwa na TCD , hii ni kwa sababu Mkutano huo pamoja na kuhudhuriwa na Rais wa nchi lakini HAUKUWA NA AJENDA , wala hata wajumbe wake hawakujua hata wanachoenda kujadili , ni kama waliburuzwa tu ili kukamilisha malengo ya waandaaji .

Wala hakuna mjumbe aliyehudhuria mkutano huo ambaye anaweza kutoka hadharani na kusema kilichojadiliwa akaeleweka , mpaka naandika hapa bado ni MARUFUKU KWA VYAMA VYA SIASA KUFANYA MIKUTANO YA HADHARA wala MAANDAMANO YA AMANI , miaka ya nyuma baada ya Mwl Nyerere kugundua umuhimu wa Demokrasia , aliwahi kuwaambia viongozi wenzake na wananchi kwamba CHAMA CHA SIASA NI MABARABARANI NA MAJUKWAANI , Kukataza harakati za kisiasa kwa vile ccm haina ajenda, haikubaliki na wala haisaidii chochote kile , hata Jakaya Kikwete aliwahi kuwaasa wanaccm wenzake .

View attachment 2177575

Ulikuwa ni mkutano wa kusikiliza hotuba za ufunguzi na zingine hotuba za kejeli kutoka kwa Dr Mahera , mwanaccm ambaye alishirikiana kwa 100% na Dr Magufuli kuvuruga uchaguzi wa 2020 kwa udi na uvumba , ikiwemo kufanya utekaji na mauaji ya wagombea na wafuasi wa vyama vingine , yaliyotokea Pemba , Lindi na kwingineko bado hayajasahaulika , Wala kikao hicho kilichokosa ajenda HAKINA HATA MAAZIMIO YOYOTE , ni heri hata kikao cha harusi ambako mwishoni kunaandaliwa hata zawadi ya bwana harusi , hiki kilikuwa kikao cha hotuba tu , anayejua ajenda zilizojadiliwa ama hata maazimio yake atuwekee hapa tujadili .

Ajenda kuu ya KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI haikugusiwa hata chembe , hizi ndio ajenda za nchi zinazoweza kuondoa maloloso yote ya akina Mahera na Kaijage na kuleta mwanzo mpya nchini , bla bla zozote hazitasaidia chochote .

Itaendelea ......
Kutakucha tu. Waache waendelee kupiga chenga. Umhimu wa katiba mpya uko palepale. Shime wananchi, tutashinda.
 
Ukimuona Zitto popote ujue yumo January na Nape pembeni yake. Zitto anafauata sana njia za hawa watu wawili lakini hasa January,
 
Back
Top Bottom