Hongera Wakenya kwa kukuza lugha ya Kiswahili Sudan Kusini

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,756
48,401
Niko huku Sudan Kusini nasaka mpunga kwenye mishe fulani hivi na nimefaulu kukatiza maeneo mengi na kushududia namna Wakenya wamehusika pakubwa kwenye kubadilisha maisha ya hawa watu waliokua wamezoea vita maporini. Kiswahili kinazidi kutamalaki na kuzagaa, leo hii kuna ushindani mkali baina ya Juba Arabic, Kingereza na Kiswahili na kwa namna fulani Kiswahili kinapenya kwa kasi.

Wasudan wengi wamesomea Kenya na kurudi huku na kushika nyadhifa muhimu muhimu, pia shule nyingi za maana zina walimu Wakenya au hao Wasudan waliorudi baada ya kusomea au kuishi Kenya. Kinatumika mtaani, maofisini na nilishangaa kwenye vyombo vya habari wanachomekea sana maneno ya Kiswahili kwenye mada zao hata wakati wanajadili kwa matumizi ya lugha zao za asili kama vile Dinka.

Ni muda tu, rais hatakua na budi ila kukifanya mojawapo wa lugha za taifa, maana mawaziri wake na wabunge wote, watoto wao wanasomea Kenya na hurudi nyumbani wameiva wakiwa tayari kwenye ujenzi wa taifa.

Uganda tu ndio niliwashangaa nilipokua kwao, wameshupaza shingo, wamekomalia Kingereza fulu, unakuta mtu aidha umuongeleshe kwa Kiganda au Kingereza, hajui neno hata moja la Kiswahili.
 
Hayo maneno yanayochomekewa ya Kiswahili huenda pia yakawa ni ya Kiarabu.
Fuatilia vizuri maana Kiswahili kimejaa Kiarabu.
 
Jambo la kushangaza huko Kenya Kiswahili hamkijui nanakidharau na kutukuza Kiingereza, ushauri wangu ni kwamba, wakenya kwanza anzeni kueneza Kiswahili na kukitukuza nchini kwenu kabla ya kusifia nchi zingine.

Jukumu na kazi ya kueneza Kiswahili duniani ni jukumu la Tanzania, ni kazi aliyoanzisha Nyerere na kuchagizwa na Magufuli, hata hao South Sudan juzi walituma ujumbe Tanzania kuomba Tanzania iwaandalie vitabu na mitaala ya lugha ya Kiswahili ili waanze kufundisha Somo la Kiswahili mashuleni Kama ilivyofanya South Africa.

Kenya ni Kiingereza na lugha za asili, Kiswahili ni lugha ya tatu

Tanzania ni Kiswahili na Kiingereza na lugha za asili ni namba tatu
 
Hayo maneno yanayochomekewa ya Kiswahili huenda pia yakawa ni ya Kiarabu.
Fuatilia vizuri maana Kiswahili kimejaa Kiarabu.

Ha ha ha!! Unachekesha bwana, sasa tufanyeje jameni tulishakikubali ndio lugha ya kutuunganisha ukanda wote huu, hivyo tukikuze kifike kote ili iwe rahisi kupiga biashara.
 
Ha ha ha!! Unachekesha bwana, sasa tufanyeje jameni tulishakikubali ndio lugha ya kutuunganisha ukanda wote huu, hivyo tukikuze kifike kote ili iwe rahisi kupiga biashara.
Kwanini wapoteze muda na rasilimali kwa kujifunza Kiswahili wakati lugha ya dunia ipo?, Waambie waachane ni Kiswahili badale yake wahimize Kiingereza zaidi Kama inavyofanya Kenya.
 
Jambo la kushangaza huko Kenya Kiswahili hamkijui nanakidharau na kutukuza Kiingereza, ushauri wangu ni kwamba, wakenya kwanza anzeni kueneza Kiswahili na kukitukuza nchini kwenu kabla ya kusifia nchi zingine.

Jukumu na kazi ya kueneza Kiswahili duniani ni jukumu la Tanzania, ni kazi aliyoanzisha Nyerere na kuchagizwa na Magufuli, hata hao South Sudan juzi walituma ujumbe Tanzania kuomba Tanzania iwaandalie vitabu na mitaala ya lugha ya Kiswahili ili waanze kufundisha Somo la Kiswahili mashuleni Kama ilivyofanya South Africa.

Kenya ni Kiingereza na lugha za asili, Kiswahili ni lugha ya tatu

Tanzania ni Kiswahili na Kiingereza na lugha za asili ni namba tatu
Wewe jamaa mimi hukuonea Huruma maishani mwako Sana. Yani umejaa hasira na chuki hakuna kikupendezacho. Naonea Bibi wako Huruma Sana boss. Uko na shida.🤣🤣🤣
 
Niko huku Sudan Kusini nasaka mpunga kwenye mishe fulani hivi na nimefaulu kukatiza maeneo mengi na kushududia namna Wakenya wamehusika pakubwa kwenye kubadilisha maisha ya hawa watu waliokua wamezoea vita maporini. Kiswahili kinazidi kutamalaki na kuzagaa, leo hii kuna ushindani mkali baina ya Juba Arabic, Kingereza na Kiswahili na kwa namna fulani Kiswahili kinapenya kwa kasi.

Wasudan wengi wamesomea Kenya na kurudi huku na kushika nyadhifa muhimu muhimu, pia shule nyingi za maana zina walimu Wakenya au hao Wasudan waliorudi baada ya kusomea au kuishi Kenya. Kinatumika mtaani, maofisini na nilishangaa kwenye vyombo vya habari wanachomekea sana maneno ya Kiswahili kwenye mada zao hata wakati wanajadili kwa matumizi ya lugha zao za asili kama vile Dinka.

Ni muda tu, rais hatakua na budi ila kukifanya mojawapo wa lugha za taifa, maana mawaziri wake na wabunge wote, watoto wao wanasomea Kenya na hurudi nyumbani wameiva wakiwa tayari kwenye ujenzi wa taifa.

Uganda tu ndio niliwashangaa nilipokua kwao, wameshupaza shingo, wamekomalia Kingereza fulu, unakuta mtu aidha umuongeleshe kwa Kiganda au Kingereza, hajui neno hata moja la Kiswahili.
Wakenya pia waongeze juhudi kwenye kujifunza Kiswahili. Kiswahili cha Wakenya wengi kinatia huruma, si sanifu na si fasaha
 
Jambo la kushangaza huko Kenya Kiswahili hamkijui nanakidharau na kutukuza Kiingereza, ushauri wangu ni kwamba, wakenya kwanza anzeni kueneza Kiswahili na kukitukuza nchini kwenu kabla ya kusifia nchi zingine.

Jukumu na kazi ya kueneza Kiswahili duniani ni jukumu la Tanzania, ni kazi aliyoanzisha Nyerere na kuchagizwa na Magufuli, hata hao South Sudan juzi walituma ujumbe Tanzania kuomba Tanzania iwaandalie vitabu na mitaala ya lugha ya Kiswahili ili waanze kufundisha Somo la Kiswahili mashuleni Kama ilivyofanya South Africa.

Kenya ni Kiingereza na lugha za asili, Kiswahili ni lugha ya tatu

Tanzania ni Kiswahili na Kiingereza na lugha za asili ni namba tatu
Takriban 95% ya Wakenya wanajua kuongea kiswahili. Nadhani chini ya 35% ya Wakenya ndio wanaoweza kuongea kwa kiingereza. Kwa hivyo kiswahili ndio lugha ya kwanza hapa Kenya. Tembea Kenya ujionee, usingoje kuelezewa.
 
Muhimu kukuza hii lugha ya kiswahili, inaweza kusaidia kuleta amani sehemu kama Sudan ya kusini, Burundi, DRC.
Amani haiwezi kuwepo kusipo kuwepo viongozi wenye utashi,, kama huku Tanzania hakuna kiongozi mwenye utashi,, wote wachumia matumbo yao,, bora akuae abaki madarakani,,
 
Back
Top Bottom