Hongera Serikali kwa kukubali kumtendea haki mtoto wa kike

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
Hatimaye serikali imesikia kilio cha wadau wa elimu waliokuwa wakishauri kuitaka serikali iruhusu watoto wanaopata ujauzito wangali mashuleni waendelee na masomo, binafsi naipongeza serikali kwa kuona kuwa ni vyema na haki kuwaandalia utaratibu watoto hao kuendelea na masomo, Na sababu zangu ni hizi zifuatazo:

1. Kwanza sheria zetu nchini zinasema kuwa kufanya mapenzi na mtoto chini ya miaka 18 unakuwa umebaka hata kama karidhia, Sasa inakuwaje aliyebakwa umhukumu kwa kumfukuza shule, Yaani ni sheria gani hiyo mbaya kabisa ya kuadhibu victim?, Mwanafunzi alipaswa afanyiwe counselling, na kumpa msaada wa kisaikoojia baada ya kubeba mimba kwa sababu kakosewa yeye na siyo kumuadhibu zaidi.

2. Pili Akili hazikai tumboni, bali ziko kichwani, hakuna ushahidi kuwa mwanafunzi akiwa na mimba hawezi kusoma, akaelewa, kisha elimu hiyo ikaja kuwa na manufaa kwake, kwa familia yake na Taifa kiujumla.

3. Tatu kumfukuza mwanafunzi shule ni kumuadhibu kwa kumnyima elimu yaani ni kumhukumia Ujinga, Sasa kufanya hivyo ni kukwamisha juhudi za Taifa za kupambana na umasikini, Ujinga na maradhi, maana elimu ni silaha ya kupambana na hivyo vitu vitatu. Sasa Taifa lingepata faida gani wakati linawanyima elimu baadhi ya watu wake makusudi eti hiyo iwe ni adhabu kwao?

4. Nne mimba siyo kosa la kisheria nchini, bali kile kitendo kinacholeta mimba ndiyo kosa la kikanuni katika mashule yetu, Sasa kumfukuza mwanafunzi shule si tu kuwa unakuwa unaharibu future yake peke yake bali unaharibu future hata ya mtoto aliye tumboni mwake pia, maana future ya mtoto iko linked na mama yake. Sasa Taifa gani hilo katili linaadhibu hadi mimba!

5. Sasa imagine tayari umemfunga baba mtu miaka 30 kwa kosa la "kubaka" , kisha ukamfukuza mama yake shule, huyo mtoto atakayezaliwa atakuwa na hali gani?, baba hayupo yuko jela, mama ndo hivyo mmeamua kumuadhibu kwa kumnyima elimu, huyu mtoto akiwa mkubwa atalipenda kwel hili Taifa?, Yaani Taifa limfukuze mama yake shule kisha mtoto huyo ukubwani eti aje kuwa mzalendo wa kulipenda Taifa hilohilo lililomuona yeye ni mzigo na kosa kubwa tangu akiwa mimba?

6. Kuna wale wanaosema eti kumuacha mwanafunzi darasani ni sawa na kupigia chapuo tabia mbaya kwa watoto wengine, hiyo hoja ni muflisi kwa sababu hawa watoto huko nyumbani watokapo mama zao, dada zao, shangazi zao, majirani zao bado wanabeba mimba, kwa nini tusiseme kuwa watajifunzia huko tudhani eti watajifunzia shuleni kwa wenzao wenye mimba?.

7. Kuna wale wanaoleta hoja za dini katika suala hili, kuwa uasherati na uzinifu ni dhambi, ni kweli vitendo hivyo ni dhambi, lakini siyo kazi ya serikali hii ya kisecular kutangaza dini au kuadhibu madhambi ya kidini, Lakini pia wale wanaotaka watoto wafukuzwe shule kwa sababu wametenda "dhambi", Je adhabu ya mtenda dhambi wa makosa hayo huwa ni kumfukuza shule?, Je na wale wanaozini mtaani nao mnataka serikali iwafanyeje?

Kwa hiyo basi kwa hoja za kimantiki, kiuchumi, kihaki na umuhimu wa elimu kwa kila mtu, naipongeza sana serikali kwa uamuzi huu wa busara, huu ni uamuzi tuliousubiri kwa muda mrefu.
KUMNYIMA ELIMU MTOTO WA KIKE ni kukwamisha juhudi za Taifa kwenye kupambana na Umasikini, Ujinga na Maradhi
 
Sasa unaipongeza serikali kwa lipi haswa? Serikali ndo iliyompokonya mtoto wa kike haki yake yake.
Hebu jaribu kutumia akili kidogo.

Kuna mambo yene tija kwa taifa ya kuanzishia uzi lakini sio hili.
 
Kuruhusu wajawazidito waendelee na masoma ni vituko, sasa huyo mtoto atalelewa na nani wakati mama yake yuko shuleni? Yaani bibi ndiye apewe jukumu la kutunza mtoto mpaka mama yake arudi shuleni?
 
Linaonekana ni jambo jema sana ila ni kituko kufundisha wanafunzi kadhaa wana ujauzito na wengine wana watoto nyumbani, maana yake hao wanafunzi tayari wako kwenye mahusiano ya kimapenzi/ndoa na wazazi wenza. Yaani wanafunzi hawatakuwa na hofu ya kufukuzwa shule wakipata mimba, wataona ni jambo la kawaida kupata ujauzito wakiwa wanafunzi. Wanatengenezwa ma single mother wengi huko mbeleni. Nani ataoa mama mwenye mtoto aliyempata kizembe akiwa mwanafunzi? Ataonekana ni muhuni hatatulia kwenye ndoa yake
 
Linaonekana ni jambo jema sana ila ni kituko kufundisha wanafunzi kadhaa wana ujauzito na wengine wana watoto nyumbani, maana yake hao wanafunzi tayari wako kwenye mahusiano ya kimapenzi/ndoa na wazazi wenza. Yaani wanafunzi hawatakuwa na hofu ya kufukuzwa shule wakipata mimba, wataona ni jambo la kawaida kupata ujauzito wakiwa wanafunzi. Wanatengenezwa ma single mother wengi huko mbeleni. Nani ataoa mama mwenye mtoto aliyempata kizembe akiwa mwanafunzi? Ataonekana ni muhuni hatatulia kwenye ndoa yake
Watafanya kama wanavyofanya wanafunzi wa vyuo ambao huwa wanapata mimba na bado wanaendelea na masomo

Kama hoja ni kusoma basi Mimba siyo kikwazo kwenye kumtafuta elimu
 
ASANTE KWA DARASA Haya maoni yako kuna mijinga ambayo haitakuelewa kwa sababu ni mijinga toka tumboni mwa mama zao
 
Mshamba tu wewe
Linaonekana ni jambo jema sana ila ni kituko kufundisha wanafunzi kadhaa wana ujauzito na wengine wana watoto nyumbani, maana yake hao wanafunzi tayari wako kwenye mahusiano ya kimapenzi/ndoa na wazazi wenza. Yaani wanafunzi hawatakuwa na hofu ya kufukuzwa shule wakipata mimba, wataona ni jambo la kawaida kupata ujauzito wakiwa wanafunzi. Wanatengenezwa ma single mother wengi huko mbeleni. Nani ataoa mama mwenye mtoto aliyempata kizembe akiwa mwanafunzi? Ataonekana ni muhuni hatatulia kwenye ndoa yake
 
hakiyanani naona mimba za kuanzia darasa la nne huku mtaani vitoto vitatafunwa bila wasiwasi mana hakuna 30 tena
 
Kituko ni wewe na watu wa aina yako mnaofikri watu wakizaa akili za kusoma zinayeyuka, ni hasara sana kuwa na taifa la vilaza washamba kama nyie.
Halafu bibi wa hao waliozaa wamekuambia wanashindwa kulea hao watoto. Si ajabu ukute hata huzai ila unawashwawashwa na uzazi.
Kuruhusu wajawazidito waendelee na masoma ni vituko, sasa huyo mtoto atalelewa na nani wakati mama yake yuko shuleni? Yaani bibi ndiye apewe jukumu la kutunza mtoto mpaka mama yake arudi shuleni?
 
Hii billion 600 imetutoa mchezoni kabisa, umasikini mbaya sana
Hivyo ni vijsenti tu, dege moja la airbus tulilonunua ni dola milioni 224, Takriban shilingi bilioni 500 na bado tunaagiza ndege nyingine. Hela tunayo

3011751_photo_2021-11-24_08-14-21.jpg
 
Je ikitokea mwanafunzi mwenzake wa kiume kampa mimba, huyo mwanafunzi wa kiume ataendelea na masomo?
 
Kuwa mjamzito au mzazi tayari wewe ni mtu mzima, na kule shule wanasoma watoto.........sasa unapo lazimisha watu wazima wakasome na watoto inaonyesha kabisa kichwani fyuzi haziko sawa.
 
Back
Top Bottom