Hongera sana Jeshi la Polisi kwa kutumia busara kubwa badala ya nguvu

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,304
12,965
Asubuhi nilitoa mada yenye kichwa "Tunasubiri kuona busara ya jeshi la polisi wakati wa kurejea kwa Lissu"

Niseme wazi kwa mara ya kwanza jeshi la polisi limetumia busara kubwa kutozuia na kuingilia mapokezi ya Tundu Lissu.

Hiki ndicho wengi tulikuwa tuna kitaka. Polisi wakijiweka kando katika shughuli za kisiasa na kijamii huwa hakuna vurugu wala madhara mpaka pale wao wanapofika na mabomu yao, virungu na bunduki kuanza kutumia nguvu kwenye dhughuli zisizo kuwa na vurugu.

Kwakweli kuna haja ya jeshi kuendelea na utamaduni huu. Waacheni watu wafanye shughuli zao za kulia na kucheka bila kuwaingilia kwa kisingizio cha mikusanyiko.

Kwa muda mrefu polisi na CDM wamekuwa kama wake wenza wanao gombea mume kila siku vitisho na ugomvi Polisi wakiwa ndio chanzo. Polisi kwa leo mmeonesha busara kwa mara ya kwanza.

Namsifu pia mkuu mpya wa mkoa wa Dar es Salaam kwa busara kubwa aliyoionesha kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa. Ingekuwa ni yule bwana masifuri leo ingekuwa ni vilio na kusaga meno. Well done!
 
Sote tunajua Jeshi la Police lina weredi, na ukitaka kuhakikisha we ongea na askari mmoja mmoja uone comments zao utashangaa!! Tatizo ni hawa wanasiasa....ila asante WAJUMBE wa Kigamboni amani na iwe kwenu....kazi mliyoifanya ni kubwa mno.

Nafikiri angekuwepo leo asingekubali pua ya mwana CHADEMA isogee pale airport. Sasa hivi tungekuwa tunaongea mengine maana airport ingegeuka uwanja wa vita

Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka!! Tanzania ya amani.
 
Hivi kwa akili ya kawaida unadhani hiyo busara imetoka kwa jeshi la polisi?!!! Thubutuuu!!! Japo kiasi fulani na huyu RC, mpya atakuwa na mchango wake kidogo, tofauti na lingekuwa lile LI ZERO, ZERO!! Pongezi zimuendee incharge mwenyewe, kwani wakati mwingine unajiongeza, ndio haya sasa yana mkuta ALI BASHIR, wale waliokuwa wanakulisha tango poli wengi wao wanaendelea kutanua wewe unapata shida!!! Japo ina bidi tubakize maneno kuna mengi sana mbeleni je busara iliyotumika leo itaendelea kutumika?!! Ni suala la muda.
 
Angalizo.

Kuna mfano hai wa mtu aliyewahi kushabikiwa na watu hapa Tz. Askari wakawa wanazuia hata jambo dogo kama kubebwa kwake, Nyerere akaagiza askari waachane naye wafanye watakavyo ila wasivunje sheria.

Hakubebwa tena na umaarufu ukakata.

Askari wakiendelea na approach hii CDM na Lisu umaarufu wao utakufa natural death.

Nahisi hivyo.
 
Back
Top Bottom