Hongera Sana January Makamba kwenye ishu ya Mifuko ya Plastiki

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,491
51,073
Kama kuna kitu pengine utakiita ni Legacy katika utumishi wako kwenye wizara ya Mazingira, basi hii sheria ya Mifuko ya Plastiki ni Achievement kubwa sana kwako.

Nchi iligeuka dampo la manailoni, mito iligeuka mhanga kwa watu kutupa mifuko hiyo, Watu walivuta hewa chafu zenye uwezo wa kuathiri afya baada ya mifuko hiyo kuchomwa.

Akina Mama ntilie walipika Wali mtaani kwa kufunikia manailoni!, Hatari ilioje. Leo utafiti unaonyesha Wilaya ya Kinondoni ina tatizo la watu kuwa na upungufu wa nguvu za kiume, sababu mojawapo bila shaka ni hii ya kula chakula kinachopikwa kwa kufunikiwa manailoni ( utafiti unaonyesha kuna uhusiano wa electyle dysfunction na matumizi ya vyakula vilivyomo kwenye mifuko ya plastiki hususan baada ya kupitishwa kwenye joto kali).

Nakuomba bwana Makamba kwa kushirikiana na mamlaka nyingine zinazohusiana na vyakula upige marufuku upishi wa kufunikia nailoni, hii ni hatari kwa afya za walaji

Serikali isikubali kurudi nyuma, hakuna faida zozote za kiuchumi zinazoshinda thamani ya Mazingira!

Katika hili jambo serikali imefanya uamuzi makini na sahihi, na iangalie pia chupa, Kama Bia zinaweza kuuzwa kwenye chupa za glass basi turudi katika utamaduni wa zamani wa soda kuuzwa kwenye chupa za glass pia.
 
Swala la msingi ni kuletwe mifuko mbadala yenye sifa zitakazokidhi haja ya kila mtumiaji vinginevyo itakua ubabaishaji tu.Na pamoja na hilo la mifuko mbadala inatakiwa watu tupate elimu ya utunzaji wa mazingira maana kimsingi ilo ndo muhimu.
 
Kwa kweli kwa upikaji wa chakula na kufunikia mfuko ya nailon ni hatari sana. Though mama ntilie wengi hawajui madhara yake siyo wa kulaumu wanahitaji kuelimishwa madhara au sheria ichukue mkondo wake marufuku kufunikia chakula kwa nailon. Ukweli hawajui madhara ila sheria na elimu ikipitishwa nina uhakika wataacha.
 
Kuna wale wanafunzi huwa wanaweka mihogo kwenye vinairon alafu wananyonya kama juice
 
Kama kuna kitu pengine utakiita ni Legacy katika utumishi wako kwenye wizara ya Mazingira, basi hii sheria ya Mifuko ya Plastiki ni Achievement kubwa sana kwako.

Nchi iligeuka dampo la manailoni, mito iligeuka mhanga kwa watu kutupa mifuko hiyo, Watu walivuta hewa chafu zenye uwezo wa kuathiri afya baada ya mifuko hiyo kuchomwa.

Akina Mama ntilie walipika Wali mtaani kwa kufunikia manailoni!, Hatari ilioje. Leo utafiti unaonyesha Wilaya ya Kinondoni ina tatizo la watu kuwa na upungufu wa nguvu za kiume, sababu mojawapo bila shaka ni hii ya kula chakula kinachopikwa kwa kufunikiwa manailoni ( utafiti unaonyesha kuna uhusiano wa electyle dysfunction na matumizi ya vyakula vilivyomo kwenye mifuko ya plastiki hususan baada ya kupitishwa kwenye joto kali).

Nakuomba bwana Makamba kwa kushirikiana na mamlaka nyingine zinazohusiana na vyakula upige marufuku upishi wa kufunikia nailoni, hii ni hatari kwa afya za walaji

Serikali isikubali kurudi nyuma, hakuna faida zozote za kiuchumi zinazoshinda thamani ya Mazingira!

Katika hili jambo serikali imefanya uamuzi makini na sahihi, na iangalie pia chupa, Kama Bia zinaweza kuuzwa kwenye chupa za glass basi turudi katika utamaduni wa zamani wa soda kuuzwa kwenye chupa za glass pia.

Mifuko Na taka za plastic hazichafui mazingira ila sisi ndo twachafua mazingira,elimu ya mazingira haipo. Wenzetu wanatumia sana mifuko Na Chupa za plastic Lkn Huwezi kuta zimezagaa.Uzitumia kama malighafi kuzalisha dizeli,lami, rooftiles,vigae,pavers,Mbao,tofali,madawati, nk.
 
Kuna wale wanafunzi huwa wanaweka mihogo kwenye vinairon alafu wananyonya kama juice
Hatari sana Kwa afya still wengine ufungiwa vyakula au vitafunio kwenye karatasi au gazeti ule wino ni sumu unaganda kwenye chakula so sumu ikiingia tumboni uleta kansa, mwilini.Mama ntilie wanafunika wali Na nailoni ili usipoe hapo sumu tupu,wanafunga ugali Kwa nylon ili usipoe ni sumu tupu,chips kwenye nyloni sumu ,vyakula chai uji kwenye vikombe na bakuli sahan za plastic sumutupu,magonjwa atuwezi kwepa.
 
Kwa kweli kwa upikaji wa chakula na kufunikia mfuko ya nailon ni hatari sana. Though mama ntilie wengi hawajui madhara yake siyo wa kulaumu wanahitaji kuelimishwa madhara au sheria ichukue mkondo wake marufuku kufunikia chakula kwa nailon. Ukweli hawajui madhara ila sheria na elimu ikipitishwa nina uhakika wataacha.

Huo ni uzembe wa watu wa afya, Kenya wanafanya Kazi kweli kweli marufuku Na kifungo ukikutwa unafungia vyakula nailoni,magazeti ,makaratasi,sahani Na vikombe vya plastic wananusuru watu wasipate magonjwa ya Figo,kansa, ini, nk.
 
Uchafuzi wa mazingira Ni mkubwa Sana hapa nchini. Mifuko ya plastik Ni SEHEMU ndogo Sana ya tatizo. Kwa upande wangu miziki inayopigwa mabaa hasa usiku Ni uchafuzi mkubwa wa mazingira. Unatesa watu wengi unaingilia ufanisi wa kazi kwani bila kulala ufanisi unapungua.
 
Swala la msingi ni kuletwe mifuko mbadala yenye sifa zitakazokidhi haja ya kila mtumiaji vinginevyo itakua ubabaishaji tu.Na pamoja na hilo la mifuko mbadala inatakiwa watu tupate elimu ya utunzaji wa mazingira maana kimsingi ilo ndo muhimu.
Veta wangetoa elimu Na sido watengeneze vifaa vya kuchakata plastic watu wazalishe dizeli,petrol, mafuta ya taa, gesi,vigae, tiles,Mbao,matofali,mabati,viti, madawati, lami,nk tokana Na taka za plastic ikiwemo mifuko chakavu,watu wakipata maarifa kuwa taka ni mali unaweza funga kama marobota ukauza ndani na nje ukapata Pesa nyingi utoona hata mfuko mmoja ukizagaa mtaani itakusanywa na kusakwa mfano wa chuma chakavu then mazingira yatakuwa safi si mitoni wa mitaroni
 
Kuna wale wanafunzi huwa wanaweka mihogo kwenye vinairon alafu wananyonya kama juice
Nakuna wale wakubwa wanawekaga chips mayai namishikaki ikiwa yamoto alafu wanakula kwastiki zakuchokonolea meno
 
Ni kweli uamuzi ni mzuri hii mifuko ilikuwa shidahaa. ila mbadala wake hapo hawajafikilia maana sijui mtu wa kijijini kana analielewa hili.
 
Wale wanawake ambao ikifika usiku wanajifunga mifuko ya plastiki mwili mzima ili wawe weupe sijui watabuni mbinu gani tena
 
Back
Top Bottom