Hongera sana Jaji Munuo!

Engineer Mohamed

JF-Expert Member
Jul 27, 2007
451
9
Hongera Jaji Munuo

JAJI Eusabia Munuo wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania ameteuliwa kuwa makamu Rais wa Chama cha Majaji Wanawake Ulimwenguni (IAWJ).

Uteuzi huo uliotangazwa jana kupitia taarifa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu wa Chama Cha majaji Wanawake Tanzania (TAWJA) Jaji E. A Kileo na kueleza kuwa uteuzi huo unaanza mwaka 2008 hadi 2010.

Taarifa hiyo ilisema kuwa uteuzi wa Jaji Munuo umetokana na juhudi zake kiutendaji katika na kusimama kidete katika kutetea haki na usawa kwa watu wote ndani ya jamii.

Tunachukua nafasi hii kumpongeza Jaji Munua kwa heshima kubwa aliyotunukiwa ambayo inazidi kung'arisha sifa kubwa ya Tanzania mbele ya mataifa mengine duniani.

Watanzania wana kila sababu kujivunia uteuzi wa Jaji huyu ambayo unazidi kuandika historia kwa wanawake wa Tanzania kuzidi kuaminika na kupewa majukumu makubwa kimataifa.

Jaji Munuo ni miongoni mwa wanawake wa Tanzania waliokabidhiwa dhamana kubwa kimataifa hivyo rai yetu ni kumtaka aendelee na moyo wake wa uchapaji kazi na ikibidi sasa aongeze mara mbili zaidi ili kuzidi kuwajengea sifa wanawake watanzania na Taifa kwa ujumla.

Miongoni mwa wanawake walioshika dhamana kimataifa kwa uchache ni pamoja na na Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa, Dkt. Asha Rose Migiro, Rais wa Bunge la Afrika, Dkt. Getrude Mongela na Mkurugenzi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo ya Makazi la Umoja wa Mataifa, Profesa Anna Tibaijuka.

Tunazidi kumtakia mafanikio makubwa Jaji Munuo katika kutekeleza jukumu hilo na kila analofanya akumbe kwamba amebeba heshima na ni kilelezo cha mamilioni ya Watanzania.
source http://www.majira.co.tz
kwa niaba ya wana JF wenzangu tunakupa hongera sana kushika wadhifa huo mkubwa.

 
Go Judge, make us Tanzanians proud.... Fly our flag higher and majestically we will walk!!!!!!!!!!
 
...i know this lady in person..ni hakimu mkazi wa kwanza mwanamke...jaji wa pili mwanamke ..baada ya julia maanning...ni jaji wa mahakama ya rufani wa kwanza mwanamke....

..hongera ..mama shushuu...[eusebio munuo]
 
record nimeiona ni nzuri, ila kwenye judiciary husifia mtu kutokana na judgements zake. maana mapro government judges ndio hupewa vyeo kama cha huyu, ila kama unasimamia haki huwezi kukumbukwa kamwe
 
Mtampongeza sana lakini inawezekana kuna kanuni zilizotumika kumchagua, isije kuwa kama JK kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa AU kwa sababu ilikuwa zamu ya EA na katika wote yeye ndo anaonekana walau kidogo, sasa isije kuwa ndo kama ya huya mama

Nalazimika kusema hivi, hiyo kazi nzuri aliyoifanya hapa Tanzania hiko wapi, wakati tumekuwa tukiona kila siku mahakama zetu za kitanzania zote na majaji wake wakipindisha sheria makusudi na kuwaonea wanyonge tu!! sasa mtasema ana mafanikio kwa lipi, Labda mafanikio katika serikali ya Mafisadi tu na sio katika Taifa la watanzania
Please mnaomsifia huyu mama, mnawesa kuweka hata ushahidi wowote wa kesi alizowahi kusimamia na kutenda haki kama inavyotakiwa? Maana Tanzania hakuna haki katika mahakama zetu, zinaendesha na fedha na kujuana tu

Sipendi kupongeza mambo kama haya, haya ndo yalitokea kwa JK lakini angalieni sasa matatizo tunayoyapa!


Naomba record ya utendaji wake wa kazi kwa Taifa la Tanzania .Hongera kwenda wapi na wapi si sifa .Je ameokoa mali zetu ? Alisha wahi kukamata kesi kubwa akaonyesha real anafaa kupongezwa ?Naombeni mwanga juu ya hili .
 
record nimeiona ni nzuri, ila kwenye judiciary husifia mtu kutokana na judgements zake. maana mapro government judges ndio hupewa vyeo kama cha huyu, ila kama unasimamia haki huwezi kukumbukwa kamwe

Kaka hapo umenena,

Mfano hai kabisa ni Jaji (Mstaafu) James Mwalusanya,alikuwa metezi wa ukweli na haki kwa maana halisi(kumbuka kesi za Mtikila kule Dodoma 1990's),ila kilichomtokea mpaka akastaafu Mungu ndo atamlipia,mwingine ni Jaji (Marehemu)Kahwa Lugakingira.Kazi zake kwa kweli ni darasa zuri sana kwa wapigania haki wote wa kweli.Kwa huyu mama sijui chochote kuhusu yeye kwa maana ya utendaji wake katika kulinda haki.Kuwa mwanamke wa kwanza kwa kila jambo haina maana kuwa ni anafanya vizuri kuliko wengine...pengine ni shukrani kwake kwa kubana haki za watu fulani...
 
Naomba nimjibu baba H kuhusu hoja yake.Namfikiri anamjaji kila mtu sawa na majaji wengine walioletea sifa mbaya taifa letu.Kama nimtu unachunguza vizuri sio tu kusoma rekodi za huyu mama,bali wafanyakazi wote kuanzia ngazi za chini za mahakama zote alizofanya huyu mama watakuelezea jinsi huyu mama alivyokua mtu wa haki.Hakuna mtu yeyote atakuambia alishawahi kusikia rushwa kwenye kesi aliyosikiliza yeye binafsi.Tunakubali rushwa imekithiri tanzania lakini mtu mmoja au wachache hawawezi kumaliza rushwa ni jukumu la wote.Huyu mama amefanya kazi yake safi na kwa uadilifu mkubwa kutokana na majukumu aliyopewa sasa sioni kwanini watu wasimpongeze.Naamini walikuwepo majaji wengi ulimwenguni lakini mungu amembariki yeye.Hongera saaaana Mama.Hata watu wasipoona ukweli wa kazi yako bado unaendelea kubarikiwa.We are sooo proud of you.Nakuchallenge mtu unaye question hongera hizi ukafuatilie kwakina ufanisi wa huyu mama tena kwa watu wa chini kabisa matarishi,madereva etc watakuelezea jinsi alivyo mtu safii.
 
Naomba record ya utendaji wake wa kazi kwa Taifa la Tanzania .Hongera kwenda wapi na wapi si sifa .Je ameokoa mali zetu ? Alisha wahi kukamata kesi kubwa akaonyesha real anafaa kupongezwa ?Naombeni mwanga juu ya hili .

Huyu kumbukumbu zake ni kubwa. Aliwahi kuisumbua serikali hadi ikafuta sheria ambayo ilikuwa inawanyanyasa wananchi katika masuala ya ardhi kule kwenye mashamba ya kule Babati na Mbulu/Karatu. But she is also pro-government katika maamuzi yake ukiachilia na kitendo cha kumweka mme wake mahabusu kwa masaa kule Arusha. mme wake ni Wakili.
 
Tunaomba CV za huyu mama kwani sisi wa TZ kwa kumwaga misifa kwa mtu hatujambo sana.Ni vyema kila mtu amjue kiundani kwa CV zake na je maamuzi yake ni ya kunung'unisha upande mwingine??
 
Tunaomba CV za huyu mama kwani sisi wa TZ kwa kumwaga misifa kwa mtu hatujambo sana.Ni vyema kila mtu amjue kiundani kwa CV zake na je maamuzi yake ni ya kunung'unisha upande mwingine??

Inabidi turudishe vile vitabu vya "Historia ya Tanzania" katika shule za misingi na pia watu waandike vitabu vya historia ya maisha yao maana vinatunza kumbukumbu kwa wahitaji.Bila hivo tutauliza hata CV ya Mtemi Mnyigumba wa Iringa,Mtemi Isike wa Tabora, Mangi Sina wa kibosho n.k
Tutapoteza kumbukumbu nyingi.
hONGERA Mama Mnuo
 
Huyu kumbukumbu zake ni kubwa. Aliwahi kuisumbua serikali hadi ikafuta sheria ambayo ilikuwa inawanyanyasa wananchi katika masuala ya ardhi kule kwenye mashamba ya kule Babati na Mbulu/Karatu. But she is also pro-government katika maamuzi yake ukiachilia na kitendo cha kumweka mme wake mahabusu kwa masaa kule Arusha. mme wake ni Wakili.


Mama E.Munuo alilizungumzia hili swala gazetini kwa mwandishi/waandishi wa habari mwezi ulopita. Alisema ni moja ya challenge ambazo amewahi kukutana nazo na kwamba ni uzushi. Alisimulia mkasa wenyewe.

Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi, alisema hafahamu kwanini alizushiwa hili. Niliposoma nilipata picha kwamba hili lilimtibua sana.



.
 
SO FAR kwenye judiciary nitamkumbuka sana jaji lukagingira, na yule mwa----simkumbuki aliyekuwa wa kwanza kufuta adhabu ya kifo, otherwise majaji wengi katika afrika ni wa ajabu, wanaigopa serikali kuliko MUNgu, mnakumbuka yule jaji aliyeshikilia biblia aliwa amesimama mbele ya kibaki kumwapisha kuwa rais huku akijua hakushinda uchaguzi
 
Nafikir Ni Wakati Wa Kuwa Na Jaji Mkuu Mwanamke Jamani Miaka Ijayo Kama Si Akiondoka Huyu Ustaadh Wetu Wa Sasa...........
 
SO FAR kwenye judiciary nitamkumbuka sana jaji lukagingira, na yule mwa----simkumbuki aliyekuwa wa kwanza kufuta adhabu ya kifo...

Eenhe, Mwikimbi, tueleze adhabu ya kifo Tanzania ilifutwa lini?

Unaweza kuona hii thread imejaa wapenda Sheria. Ukija na 'michongo' iliyopinda hapa utabanwa mbavu!

Anyway, vinginevyo thread ni kali; mlio uliza ni nini wasifu wa huyu Mama Jaji mmenifurahisha.

Siku chache zilizopita kuna hoja ili criticize hili swala la Jaji Mkuu kuwa Brigedia General wakati huo huo. Wengine wakasema Jaji Ramadhani alisha toka jeshini. Lakini nikadhani hata kama katoka, lazima kuna wakati alikuwa Mjeshi na Jaji wakati huo huo. Nikaanza kutafuta wasifu, resume, biography, na chochote kuhusu historia ya Jaji Ramadhani.

Tafuta, tafuta na wewe. Tafuta, tafuta na wewe. Tunaongelea Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano. Mpaka leo sijui Jaji Ramadhani alifika fikaje kuwa Mkulu, umaarufu wake ni nini, alikuwa mkali shule au kuna decisional law yake maarufu, je anakuwa cited kwa landmark opinions, au ni vipi? Ninachojua ni kwamba alikuwa Jaji Mkuu Zanzibar miaka nenda rudi, halafu akawepo kwenye Mahakama ya Kijeshi wakati wa vita vya Kagera. Sasa sijui alijinoa lini kwenye Sheria ya Tanzania Bara kufikia kupewa u Jaji Mkuu.

Kama walivyo kwisha sema wengine, inawezekana Mama Jaji hapa nae hana ukali wowote bali ilikuwa zamu yetu kama Muungwana na Ukulu wake wa African Union!
 
kuna hukumu moja alitoa jaji mmoja mstaafu anaitwa mwalusendo? ilitolewa dodoma, ilkkuwa crtic kweli kweli nadhani miaka ya 90, huyo jaji baadaye alikuja ku-paralyze na sijui kama yuko hai, wanasheria mnisadie
 
Nafikiri wengi wetu tunanukuu mambo ya mitaani pasipokuwa na refernce zozote. Sheria ya kifo haijafutwa Tz ila raisi anauwezo wakutoa msamaha wa mtu aliyehukumiwa kifo na hivyo bado ipo.

Napenda pia nitoe michango mbalimbali ya jaji huyu katika jamii nje kidogo ya kazi yake.

Amekuwa mhamasishaji wa utunzaji wa mazingira katika makala zake mbalimbali za binadamu na mazingira utakazozipata katika NGo tofauti e.g Envirocare ambazo zinatumika katika uelimishaji vijijini unaweza kusoma baadhi ya makala alizotoa 2002.

Alikuwa mfano mzuri pale tu alivyohamishiwa ofisi ya mahakama moshi wanaoifahama wanakumbuka mazingira yake yalivyokua na alivyohamia yalivyobadilika hii ni kuwepo kwa changamoto yake.

Ni mtunzi wa kitabu cha haki na sheria za wanawake kilichotoka miaka ya themanini kwa waliokisoma kinazungumzia sheria na wajibu wa wanawake pamoja na wanawake wajane.

Ametumika katika semina mbalimbali vijiji kuelimisha wanawake kwenye sheria ya ardhi na pia haki za watoto ukijumuisha na watoto nje ya ndoa.

Biography yake imeandikwa na mwandishi mmoja nafikiri ni Mganda nilikua na research jina lake sijalipata nikipata nitaforward .Haya ni mambo ninayoyafahamu wazi kwakusearch kwenye intern na baadhi ya NGo nilizofanya kazi. Naomba tuwe wasomaji na wachunguzi na sio kulalamika tu.

Watanzania tunakuwa na interest ya kusoma mambo ya wanasiasa na hasa vitimbi lakini hatusomi mambo mengine yanayofanywa katika jamii. Kama hatusomi basi tusiwe wepesi wakulalamika na kujaji watu.
 
Kama mnakumbuka wenzangu miaka ya 2000 kule Same Kilimanjaro alikuwa akizungumza na na watekelezaji wa sheria na pia viongozi wa dini na wakimila. Umuhimu wa kuzingatia haki za binadamu pasipo kuingilia mila na desturi.

Nilikuwepo kwenye semina hiyo natulipewa maswali na mambo yakudiscuss na baada ya hapo kila mtu kutoa maoni na mtazamo wa kila grp na baadaye mama mwenye kushiriki katika mjadala na kutoa majibu. Alionyesha upeo wake wa ufahamu wa sheria na umuhimu wa familiaya kisheria aliyokua anaulizwa na watawala wa sheria vijijini. Akijibu hakuwa ananukuu mahali ukijumuishwa na maswali yote.

Jinsi tunavyojenga familia bora ndio jinsi tunavyokuza viongozi bora wa kuendesha taifa bora. Tulizungumza jinsi tunavyoshindwa kulea watoto na hasa watoto wa nje ya ndoa na baadaye tunakuwa walalamishi tu lakini kilamtu angewajibika katika nafasi yake tungejenga taifa lenye watu wenye mtizamo tofauti kabisa.

Tukazungumzia ni jinsi gani jamii inalifumbia macho swala la ukeketaji kwa kina mama,na baadaye tunataka mwanamke awe mwenye kujiamini anayeweza kumudu ushindani wa sasa na tunasahau hadhari za ukeketaji zinafyoacha permanent scar kwa maisha etc. Jaji aliweza kuhusianisha mambo mbalimbali ambayo baadaye tungekua tunatilia maanani watanzania tungekua mbali.

Unajua ukitaka kutoa mchango wako nenda kijijini lakini bahati mbaya wengi wetu tunasikiliza huyu amefanya hiki kwenye redio na kuangalia TV ndio tunaona archievement ya mtu tungekua tunatilia amkazo vijijini hata miji mikubwa isingejaa hivyo maana kila mtu anakimbia vijijini.

Nataka kuonyesha ni jinsi gani mtu unaweza ukatoa michango yako vijiji usijulikane lakini ukifanya miji mikubwa watu ndio wanakuona umefanya makubwa.
 
Du baada yakutupwa chini na serikali ya JK kwenye ujaji mkuu Mungu akasema hapana. Nakufungulia mlango mkubwa kuliko watakavyodhani. Mama mshukuru Mungu, ni wazi uliachwa kwasababu yakutokukubali kuwa mtu wakutumika. Inawezekana ni jaji pekee uliyekuwa kwenye short list ambaye ulikuwa huna watu waku-lobby kwaajili ya hiyo post. Walikutoa kwa kisingizio kwamba una maliza muda wako; ingawaje baada ya uteuzi wa jaji mkuu wa sasa wali-extend muda wako ili wakuongezee kazi (uwasaidie kufanya kazi wale wapya waliopewa post bila ujuzi). Hukuweka kinyongo na umeendelea kuzifanya kazi hizo bila kinyongo. Hukuendekeza makundi.

Nimesoma kwenye tovuti ya IAWJ nikagundua hii nafasi ilikuwa ni nafasi ya kupigiwa kura na nchi wananchama wa IAWJ. Ni wazi umestahili hii post.

Nakumbuka huyu ndie Jaji aliyetetea/advocate (zama zile) sheria ya ardhi-wanawake kumiliki ardhi. Inawezekana umetofautiana na watu hapa na pale lakini juhudi zako katika kumtetea mtoto wa Kike, watoto wa nje ya ndoa, wanawake, na jamii kwa ujumla imeonekana. Nakumbuka ulipokuwa Hakimu Arusha uli-challenge pale watu walipotaka kuwafunga watoto waliokuwa wametoroka shule na kwenda kuvuta bangi/sigara. Ulionyesha wazi kumfunga mtoto hakutamsaidia kuwa a good productive citizen.

Nakumbuka watoto wako walisoma shule za msingi za serikali, ulipogundua watoto wako wanakaa chini, na wengine kubanana kwenye madawati ulikwenda kwenye shule yao ya msingi-Arusha. Uli-mchallenge mkuu wa shule kuanzisha mfuko kwaajili ya madawati. Nakumbuka kupokelewa official letter ya ombi lako na kusomwa ofisi kuu. Ni kwa uzalendo wako hukuwaamisha watoto wale shule bali uliona umuhimu wakutafuta solution. Thank you for all you have done. Uongezewe pale unapopungukiwa,,,,,Go mama Go ooo!!!

Nafikiri uteuzi wake umewekwa rasmi May 2012 nafikiri before that walipendekeza tu jina likaenda kupigiwa kura na nchi wanachama kama inavyoonyesha hapa.

H@ki Ngowi: TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA MAJAJI WANAWAKE DUNIANI.
 
Back
Top Bottom