Hongera sana Dr Slaa ;Ujasiri wako unatisha

Status
Not open for further replies.

Kilasi Mkuu

JF-Expert Member
Nov 25, 2013
2,325
719
Nimeona nitumie JF kumpongeza Dr Slaa kwa kufanya ziara yenye mafanikio makubwa.Wako watu ambao kwa hisia zao walionekana ni wana ccm,walikutisha usifanye ziara hiyo hasa Kigoma na wakasema unaweza hata kupoteza maisha.
Ripoti tulikuwa tukizipata humu kwenyeJF,wakisema vijana wameandaliwa kukumaliza hali ambayo kwa mtu mwoga angeweza kukimbia.Kuna kipindi tulipokuwa tunafuatilia kupitia humuJF walisema Vijana wanapewa 5000 waandamane kukupinga na kweli walitokea na mabango lakini hukutishika.Kijana mmoja alipo hojiwa alionekana nimtoto wa katibu mwenezi wa ccm huko Kigoma hali iliyo toa taswira kama ccm walikuwa nyuma ya upinzani huo.
Ni mambo ambayo ametuhumiwa hata Zito kuwa anafanya uasi kuhujumu cdm.Lingine ambalo linanishawishi nikwamba,kwa chama kama cdm ndiyo kwanza kinajijenga,isingekuwa rahisi kumuonea kijana kama Zito aliye kuwa hodari na jasiri katika chama.Katika vita kamanda hodari sindiyo anafaa kwanini umfukuze?Siamini kama cdm ni wajinga hivyo kupoteza nguvu kazi kubwa namna hiyo.Huenda kwa sasa wamepima faida na hasara za kijana huyo na wakaona afadhali kukaa mbali nae.Haya ni maoni yangu wakuu kama mfuatiliaji wa humu kwenye JF.
 
Kiujumla wanasiasa wengi wa chadema ni majasiri, lakini kwa dr. Slaa ni zaidi. Amethubutu kuonyesha kwa vitendo hatishiki hata kidogo na propaganda na hata vitisho.
 
Nimeona nitumie JF kumpongeza Dr Slaa kwa kufanya ziara yenye mafanikio makubwa.Wako watu ambao kwa hisia zao walionekana ni wana ccm,walikutisha usifanye ziara hiyo hasa Kigoma na wakasema unaweza hata kupoteza maisha.
Ripoti tulikuwa tukizipata humu kwenyeJF,wakisema vijana wameandaliwa kukumaliza hali ambayo kwa mtu mwoga angeweza kukimbia.Kuna kipindi tulipokuwa tunafuatilia kupitia humuJF walisema Vijana wanapewa 5000 waandamane kukupinga na kweli walitokea na mabango lakini hukutishika.Kijana mmoja alipo hojiwa alionekana nimtoto wa katibu mwenezi wa ccm huko Kigoma hali iliyo toa taswira kama ccm walikuwa nyuma ya upinzani huo.
Ni mambo ambayo ametuhumiwa hata Zito kuwa anafanya uasi kuhujumu cdm.Lingine ambalo linanishawishi nikwamba,kwa chama kama cdm ndiyo kwanza kinajijenga,isingekuwa rahisi kumuonea kijana kama Zito aliye kuwa hodari na jasiri katika chama.Katika vita kamanda hodari sindiyo anafaa kwanini umfukuze?Siamini kama cdm ni wajinga hivyo kupoteza nguvu kazi kubwa namna hiyo.Huenda kwa sasa wamepima faida na hasara za kijana huyo na wakaona afadhali kukaa mbali nae.Haya ni maoni yangu wakuu kama mfuatiliaji wa humu kwenye JF.

Yaani huyu Mzee anatakiwa atunukiwe nishani ya heshima kabisa.

Kumbuka huyu mzee ndiye aliyewapukutisha kina BALALI, Rostam an kina Lowasa na issue zao za EPA, Deep Green na Meremeta.

Huyu Mzee ndiyo kawafanya vijana wengi waweze kuongea na kukemea Hadharani. Kimsingi kawaambukiza ujasiri vijana wengi sana ndani na nje ya Bunge letu.

Huyu Mzee akisimama 2015, lazima mafisadi wakapunzike.
 
Ujasiri wa kuhalalisha gongo?
watu wanaangalia gongo tu bila kujua Dr Slaa alikuwa ana maanisha nini; hebu angalia mambo yafuatayo ili kujua kiongozi mwenye mawazo mbadala wa kuokoa afya za watu na kutengeneza kipato halali kwa wananchi wake;
1)Watu wengi ni maskini wanakunywa gongo kwa kuwa ni bei rahisi kuimudu,
2) fedha za gongo zinachukuliwa na mapolisi kwa njia ya rushwa
3)Gongo inatengenezwa katika mazingira machafu hivyo kuhatarisha afya za wanywaji
4) CDM ikiingia madarakani itawaagiza SIDO watengeneze mitambo ya kutengeneza gongo kwa njia ya usafi
 
Dr. hata ndani ya makambi ya jeshi anakubalika sana. Kutana nao utasikia wakimkubali na ndo maana uchaguzi 2010 alipata kura nyingi maeneo yote wanayoishi wanajeshi, hasa Kibaha yote mpaka Mlandizi, Lugalo na Makongo Gongolamboto. By the way watu wamejengewa hofu hasa kwa kazi za ajira kwa watu wasiokuwa na professional kama hao wa Lumumba wenye elimu ya chuo cha kivukoni
 
Nivizuri kuzungumzia walio baka watoto,na kusokomeza sehemu za siri wanawake wasiyo nahatia,ni vizuri pia kujiuliza chama kilicho unda serikali hiyo kama siyo ccm.Ni aibu kutetea chama cha namna hiyo na ni dhambi kuu haina mfano wake
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom