Nakumbuka mwanzoni mwa mwaka 2005 tukiwa tunajiandaa kufanya UE (University Exams) pale Mlimani ,kulitokea kama kamgomo baridi fulani hivi ka Daladala zilizokuwa zikitokea Mwenge kwenda Ubungo kupitia Chuo.
Basi siku hiyo mimi na rafiki zangu wawili tulikuwa tumesimama pale Utawala tukisubiri gari lolote litakalopita hapo tuombe lift litusogeze Ubungo ama Mabibo Hostel yalipokuwa maskani yetu!
Baada ya kusimama pale kwa muda kidogo mara nikaliona Mercedez Benz jeusi linakuja nikalipiga mkono,likapunguza mwendo na kupaki pembeni .Dereva wa gari lile akafungua mlango na kutoka kutufuata ,alikuwa amevaa suruali ya jeans ya blue,raba nyeupe, fulana yenye mistari mithili ya pundamilia na kichwani alikuwa amevaa kofia la pama kama lile la Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayadit.
Baada ya kutusogelea kwa karibu tukamtambua ,mimi na rafiki zangu wale tukamsalimia na yeye akatuuliza kuna shida gani pale Chuo siku ile, kwani ameona hali si ya kawaida na wanachuo wako katika makundi makundi! Tukampa picha ya pale kisha naye akatumbia alikuwa katika zoezi la kukagua barabara iliyojengwa kutoka Survey hadi Gate Maji.
Baada ya maelezo yale akatoa offer ya kutupa lift hadi Mabibo Hostel.Wakati anafungua mlango kuingia kwenye gari lake wale rafiki zangu wakaniambia kwa utani, wewe kaa mbele na Waziri mwenzako sisi tutakaa siti ya nyuma! Yule Dereva akaniuliza kumbe na wewe ni Waziri hapa Mlimani ?,nikamjibu ndio mimi ni Waziri wa Fedha hapa.
Katika mazungumzo yetu huku akiendesha gari lake taratibu na kwa kuwa alikuwa simple siku hiyo nikapata ujasiri nikamuuliza ;vipi Mheshimiwa kuhusu afya yako maana tulisikia juzi kati hapa kuwa umekula sumu Dodoma na ukakimbizwa Ujerumani kwa matibabu ya haraka?,akanijibu ! kisha nikamuuliza tena ,vipi mwaka huu unaingia ulingoni ? akanijibu ,hapana muda wangu bado ,bado navuta pumzi. Huyo Dereva hakuwa mwingine bali ni Dr.John Pombe Magufuli.
Usiku ule nilipomwona Dr.John Pombe Magufuli akiingia ukumbi mpya wa Mikutano wa CCM huku wajumbe wa mkutano mkuu wakimshangilia kwa vifijo na nderemo nilibaki nimeduwaa! Nikajisemea moyoni kumbe Ndugu huyu anajua kuzichanga karata zake vizuri namna hii!
Sikuamini kama kweli Dr.John Pombe Magufuli alikuwa anaelekea kutimiza ndoto yake ya siku nyingi kirahisi namna ile! Hata kwa mtu ambaye kwa mara ya kwanza alikuwa ameingia Tanzania kutoka sayari nyingine na akaibukia kwenye Mkutano Mkuu wa CCM pale Dodoma angeona dhahiri ushindi wa Dr.Magufuli usiku ule.
Yeye binafsi alifurahi kupitiliza na wengi mliona hata hotuba yake ya kuomba kura ilitaka kukosa format nzuri kwa kuwa alikuwa overwhelm!
Anayesema Dr.John Pombe Magufuli kaokota Urais hamjui vizuri Dr.Magufuli ! Ni mtu aliyejua anachotaka na katika mchakato wa kumtafuta mgombea Urais ndani ya CCM alicheza kete zake kama vile Eddie Murphy ( Hakeem) mtoto wa Mfalme wa Bemunda kwenye ile movie y a COMING TO AMERICA alivyom-win Lisa binti ya yule Tajiri mwenye Hotel.
Hata magazeti ya hapa nyumbani ambayo mengi ni ya kishabiki na kufuata mkumbo tu hayakumpa attentionisipokuwa gazeti moja tu la Raia Mwema ndilo lilionekana kunusu harufu ya Dr.John Pombe Magufuli.Nalipongeza gazeti la Raia Mwema na nakiri waandishi wake ni watu mahiri sana,na pia nahisi wako karibu na watu wa KITENGO.
Kuibuka kwa Dr.John Pombe Magufuli kama mshindi wa kinyanganyiro cha mgombea Urais ndani ya CCM kumenifanya niendelee kuiamini CCM kama taasisi makini na yenye watu makini sana na kwa hili JAKAYA ni fundi.
Dr.Magufuli alitafuta wadhamini ndani ya Chama kama mtu mwenye maelekezo fulani! Sasa utasemaje kuhusu kauli kama ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee Philip Mangula aliyoitoa siku chache kabla ya vikao kuanza Dodoma kuwa, Mgombea wa CCM hajinadi,atanadiwa na Chama.
Kwa hili Hongera sana Jakaya,Hongera sana CCM! Mmethibitishia Ulimwengu kuwa CCM ni taasisi imara na makini na hakuna mtu mmoja mkubwa kuliko CCM! Heshima ilioje!!!!!!!?
Nilichojifunza zaidi ni kuwa Dr.John Pombe Magufuli ni mwanasiasa mjanja sana ambaye anajua kutafuta anachotaka! Na katika hili nimempa A plus kama nilivyompa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya!
Kumbuka mwaka 2007 Uhuru Kenyatta aliulizwa kwa nini hagombei Urais yeye akajibu kuwa hawezi kugombea kwa kuwa hana uhakika wa kushinda na akaamua kumuunga mkono Rais Mwai Kibaki.
Sote tunakumbuka alichomfanyia Raila Amolo Odinga mwaka 2013! na sasa masikini Raila Amolo Odinga upepo unaonyesha nafasi yake ya kuikanyaga Ikulu ya Nairobi kama Rais wa Nchi hiyo imekuwa reduced to ashes!
Kwa kifupi Dr.John Pombe Magufuli amefuzu mafunzo yote ya mwanamapinduzi wa China Sun Tzu katika kitabu chake cha The Art of War. He knows how to choose his battles wisely. Na kuna wisdom ambayo amewashinda wapinzani wake nayo ina state kwamba,Even if you are interested in something,dont show to others that you are dying for it. WATAKUKWAMISHA TUUU!
Hongera sana Dr.John Pombe Magufuli ,Rais wetu ajaye wa Awamu ya Tano.
Basi siku hiyo mimi na rafiki zangu wawili tulikuwa tumesimama pale Utawala tukisubiri gari lolote litakalopita hapo tuombe lift litusogeze Ubungo ama Mabibo Hostel yalipokuwa maskani yetu!
Baada ya kusimama pale kwa muda kidogo mara nikaliona Mercedez Benz jeusi linakuja nikalipiga mkono,likapunguza mwendo na kupaki pembeni .Dereva wa gari lile akafungua mlango na kutoka kutufuata ,alikuwa amevaa suruali ya jeans ya blue,raba nyeupe, fulana yenye mistari mithili ya pundamilia na kichwani alikuwa amevaa kofia la pama kama lile la Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayadit.
Baada ya kutusogelea kwa karibu tukamtambua ,mimi na rafiki zangu wale tukamsalimia na yeye akatuuliza kuna shida gani pale Chuo siku ile, kwani ameona hali si ya kawaida na wanachuo wako katika makundi makundi! Tukampa picha ya pale kisha naye akatumbia alikuwa katika zoezi la kukagua barabara iliyojengwa kutoka Survey hadi Gate Maji.
Baada ya maelezo yale akatoa offer ya kutupa lift hadi Mabibo Hostel.Wakati anafungua mlango kuingia kwenye gari lake wale rafiki zangu wakaniambia kwa utani, wewe kaa mbele na Waziri mwenzako sisi tutakaa siti ya nyuma! Yule Dereva akaniuliza kumbe na wewe ni Waziri hapa Mlimani ?,nikamjibu ndio mimi ni Waziri wa Fedha hapa.
Katika mazungumzo yetu huku akiendesha gari lake taratibu na kwa kuwa alikuwa simple siku hiyo nikapata ujasiri nikamuuliza ;vipi Mheshimiwa kuhusu afya yako maana tulisikia juzi kati hapa kuwa umekula sumu Dodoma na ukakimbizwa Ujerumani kwa matibabu ya haraka?,akanijibu ! kisha nikamuuliza tena ,vipi mwaka huu unaingia ulingoni ? akanijibu ,hapana muda wangu bado ,bado navuta pumzi. Huyo Dereva hakuwa mwingine bali ni Dr.John Pombe Magufuli.
Usiku ule nilipomwona Dr.John Pombe Magufuli akiingia ukumbi mpya wa Mikutano wa CCM huku wajumbe wa mkutano mkuu wakimshangilia kwa vifijo na nderemo nilibaki nimeduwaa! Nikajisemea moyoni kumbe Ndugu huyu anajua kuzichanga karata zake vizuri namna hii!
Sikuamini kama kweli Dr.John Pombe Magufuli alikuwa anaelekea kutimiza ndoto yake ya siku nyingi kirahisi namna ile! Hata kwa mtu ambaye kwa mara ya kwanza alikuwa ameingia Tanzania kutoka sayari nyingine na akaibukia kwenye Mkutano Mkuu wa CCM pale Dodoma angeona dhahiri ushindi wa Dr.Magufuli usiku ule.
Yeye binafsi alifurahi kupitiliza na wengi mliona hata hotuba yake ya kuomba kura ilitaka kukosa format nzuri kwa kuwa alikuwa overwhelm!
Anayesema Dr.John Pombe Magufuli kaokota Urais hamjui vizuri Dr.Magufuli ! Ni mtu aliyejua anachotaka na katika mchakato wa kumtafuta mgombea Urais ndani ya CCM alicheza kete zake kama vile Eddie Murphy ( Hakeem) mtoto wa Mfalme wa Bemunda kwenye ile movie y a COMING TO AMERICA alivyom-win Lisa binti ya yule Tajiri mwenye Hotel.
Hata magazeti ya hapa nyumbani ambayo mengi ni ya kishabiki na kufuata mkumbo tu hayakumpa attentionisipokuwa gazeti moja tu la Raia Mwema ndilo lilionekana kunusu harufu ya Dr.John Pombe Magufuli.Nalipongeza gazeti la Raia Mwema na nakiri waandishi wake ni watu mahiri sana,na pia nahisi wako karibu na watu wa KITENGO.
Kuibuka kwa Dr.John Pombe Magufuli kama mshindi wa kinyanganyiro cha mgombea Urais ndani ya CCM kumenifanya niendelee kuiamini CCM kama taasisi makini na yenye watu makini sana na kwa hili JAKAYA ni fundi.
Dr.Magufuli alitafuta wadhamini ndani ya Chama kama mtu mwenye maelekezo fulani! Sasa utasemaje kuhusu kauli kama ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee Philip Mangula aliyoitoa siku chache kabla ya vikao kuanza Dodoma kuwa, Mgombea wa CCM hajinadi,atanadiwa na Chama.
Kwa hili Hongera sana Jakaya,Hongera sana CCM! Mmethibitishia Ulimwengu kuwa CCM ni taasisi imara na makini na hakuna mtu mmoja mkubwa kuliko CCM! Heshima ilioje!!!!!!!?
Nilichojifunza zaidi ni kuwa Dr.John Pombe Magufuli ni mwanasiasa mjanja sana ambaye anajua kutafuta anachotaka! Na katika hili nimempa A plus kama nilivyompa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya!
Kumbuka mwaka 2007 Uhuru Kenyatta aliulizwa kwa nini hagombei Urais yeye akajibu kuwa hawezi kugombea kwa kuwa hana uhakika wa kushinda na akaamua kumuunga mkono Rais Mwai Kibaki.
Sote tunakumbuka alichomfanyia Raila Amolo Odinga mwaka 2013! na sasa masikini Raila Amolo Odinga upepo unaonyesha nafasi yake ya kuikanyaga Ikulu ya Nairobi kama Rais wa Nchi hiyo imekuwa reduced to ashes!
Kwa kifupi Dr.John Pombe Magufuli amefuzu mafunzo yote ya mwanamapinduzi wa China Sun Tzu katika kitabu chake cha The Art of War. He knows how to choose his battles wisely. Na kuna wisdom ambayo amewashinda wapinzani wake nayo ina state kwamba,Even if you are interested in something,dont show to others that you are dying for it. WATAKUKWAMISHA TUUU!
Hongera sana Dr.John Pombe Magufuli ,Rais wetu ajaye wa Awamu ya Tano.