Hongera Raisi Wetu Magufuli kwa kutokomeza ufisadi, hadi watani zetu hawana sera tena

Elimu ya hapa na pale

JF-Expert Member
Aug 23, 2016
846
824
Wapendwa hii ni kwa wale tu tunaopinga ufisadi.

Baada ya vyama mbalimbali kulifumbia macho swala la ufisadi na rushwa na wapiga madili. Naomba nimpongeze Rais wetu MAGUFULI kwa kujitoa muhanga na kupambana na tabia chafu zilizo kuwa zimeligarimu taifa letu kwa mda mrefu.

Nimeangalia kwa upande wa wa pili sehemu mbalimbali kwenye mikutano yao ya siasa, neno rushwa na ufisadi hawataji tena.

Kwa hali hii nakupongeza raisi wetu, wala usiwaze kulegeza kamba wala usiwachekee. Mungu wa mbinguni Atakubariki wewe na nchi yako. Amina
 
Sasa ni muda wa kuwachukulia hatua hao Mafisadi.........Kuanzia ununuzi wa Rada, Mikataba ya IPTL, ufisadi wa ESCROW na wacheza show wote wa scandal ya LUGUMI.......hakika baada ya kufanya haya, hii Nchi itakuwa ya maziwa na asali na Mungu atambariki na kumpa Rehema za ajabu.
 
Kutokomeza ufisadi??
Are y serious??

Ufisadi gan huo, huu wa kikuda wa vimilion vidogo dogo, vihela vya mboga??

Hiv unajua ni kwa kias gan wapuuz wachache wameigharimu hii nchi alaf wanakula bata tu.

Anyway,

Lugumi, escrow, iptl huu nahis hii ni mifupa iliyomshinda
 
Sasa ni muda wa kuwachukulia hatua hao Mafisadi.........Kuanzia ununuzi wa Rada, Mikataba ya IPTL, ufisadi wa ESCROW na wacheza show wote wa scandal ya LUGUMI.......hakika baada ya kufanya haya, hii Nchi itakuwa ya maziwa na asali na Mungu atambariki na kumpa Rehema za ajabu.

Alisema hana uwezo wa kufukua makaburu.
 
Barabara za mchina alizosimamia vimeshafumuka alifanya ufisadi wa kutosha
 
Kutokomeza ufisadi??
Are y serious??

Ufisadi gan huo, huu wa kikuda wa vimilion vidogo dogo, vihela vya mboga??

Hiv unajua ni kwa kias gan wapuuz wachache wameigharimu hii nchi alaf wanakula bata tu.

Anyway,

Lugumi, escrow, iptl huu nahis hii ni mifupa iliyomshinda
Mafisadi Uliowataja hapo mwaka 2020 watahamia chadema na wewe utawasafisha kama ulivyowasafisha wa Richmond 2015
 
Wapendwa hii ni kwa wale tu tunaopinga ufisdi.

Baada ya vyama mbalimbali kulifumbia macho swala la ufisadi na rushwa na wapiga madili. Naomba nimpongeze Rais wetu MAGUFULI kwa kujitoa muhanga na kupambana na tabia chafu zilizo kuwa zimeligarim taifa letu kwa mda mrefuuu.
Nameangalia kwa upande wa wapili sehemu mbalimbali kwenye mikutano yao ya siasa, neno rushwa na ufisadi hawataji tenaa.
Kwa hali hii nakupongeza raisi wetu, wala usiwaze kuregeza kamba wala usiwachekeee. Mungu wa mbinguni Atakubariki wewe na inchi yako. Amina.
Rudisha hela za maafa mbwaa wewe. Na mahakama ya mafisadi imejaa bui bui mpaka leo furniture hazijawahi kukaliwa kiazi wewe
 
Mafisadi wako ccm na ndio wawezeshaji wakuu wa chama!sasa kama huyo mtukufu wenu ni mpambanaji kweli awadake wale wa escrow tu!
 
Wapendwa hii ni kwa wale tu tunaopinga ufisdi.

Baada ya vyama mbalimbali kulifumbia macho swala la ufisadi na rushwa na wapiga madili. Naomba nimpongeze Rais wetu MAGUFULI kwa kujitoa muhanga na kupambana na tabia chafu zilizo kuwa zimeligarim taifa letu kwa mda mrefuuu.
Nameangalia kwa upande wa wapili sehemu mbalimbali kwenye mikutano yao ya siasa, neno rushwa na ufisadi hawataji tenaa.
Kwa hali hii nakupongeza raisi wetu, wala usiwaze kuregeza kamba wala usiwachekeee. Mungu wa mbinguni Atakubariki wewe na inchi yako. Amina.
mkuu amefanya la maana sana kutokomeza ufisadi, lakini kusema ukweli, kuna baadhi ya hatua hakutakiwa kuzichukua ghafla bali polepole, kufanya kila kitu ghafla hivi kumeleta side effects kwenye uchumi ndio maana hali ilivyo sasaivi haina tofauti na hali iliyokuwepo baada ya vita vya kagara. maisha yalikua magumu hivihivi. hakuna hela mtaani, hakuna hela za kufanyia kazi serikalini, kukopa tu na kuongeza deni. huwezi kung'oa mti uliomea katikati ya nyumba yako bila umakini, ukifanya mchezo utadondosha na nyumba yote ukose vyote sasa. Tumuombee.
 
Kama kuna mafisadi mbona hajawafunga.Acheni mbwembwe za sifazisizo za kweli.Semeni kingine
 
Lupyeee bwana! Ina maana fisadi akihama CCM na kwenda Chadema serikali haiwezi kumkamata? Mbona huwa mnasema serikali itawasaka na kuwatafuta mafisadi popote walipo kuwakamata na kuwapeleka mahakama ya mafisadi. Na pia mnasema serikali ina mkono mrefu. Ina maana fisadi akiwa Chadema hakamatiki? Kwa hiyo na yale 'makaburi' anayoyagwaya mzee yako Upinzani? Basi upinzani wa Tanzania ni kiboko. Wapeni na nchi kabisa. Bahati yenu, msingeshtuka na kwenda kunyang'anya computer zao, leo mngekuwa mnalia kilio cha Obama na Hillary dhidi ya Putini. Ngoja, 2020 wataweka kambi Israel, tuone kama mtakwenda kuwanyang'anya computer zao.
 
Lugumi ni ufisadi mpya kabisa ambao umeendelea kipindi cha magufuli, anyway nadhani amekomesha ufisadi mdogo mdogo wa watumishi wa umma lakini ufisadi mkubwa unaowahusu wanasiasa bado hajaukomesha maana hata iptl bado inalipwa mamilioni
 
Wapendwa hii ni kwa wale tu tunaopinga ufisadi.

Baada ya vyama mbalimbali kulifumbia macho swala la ufisadi na rushwa na wapiga madili. Naomba nimpongeze Rais wetu MAGUFULI kwa kujitoa muhanga na kupambana na tabia chafu zilizo kuwa zimeligarimu taifa letu kwa mda mrefu.

Nimeangalia kwa upande wa wa pili sehemu mbalimbali kwenye mikutano yao ya siasa, neno rushwa na ufisadi hawataji tena.

Kwa hali hii nakupongeza raisi wetu, wala usiwaze kulegeza kamba wala usiwachekee. Mungu wa mbinguni Atakubariki wewe na nchi yako. Amina


Ikiwa serikali imefirisika mpaka inaiba pesa za rambirambi sasa za kufisadi zinatoka wapi wakati nchi imefirisika
 
Umejuaje Kama ufisadi umetokomezwa? Hamna kesi haina maana hamna ufisadi.

Ndio maana kuna member huwa anauliza mlienda shule kusomea ujinga?
 
Back
Top Bottom