Ndachuwa
JF-Expert Member
- Mar 8, 2006
- 6,269
- 4,569
Nampongeza kwa dhati Raisi Obama wa Marekani kwa kusudio lake la kuongeza kodi kwa wale wenye mapato makubwa kuchangia zaidi serikali yao.
Naamini kwa kuwa Raisi wetu Jakaya Kikwete yuko huko Marekani, hotuba ya Obama itamfanya aelewe kile CHADEMA walichokuwa wanatetea katika Bunge la Bajeti kuwa wabunge walipie kodi mapato yao yote na baadhi ya posho wanazolipwa watumishi wa umma (hususani viongozi) ziondolewe. Naamini vile vile kwa kuwa Tanzania tu watu wa kuiga, hata lile wazo la kusamehe kodi Posho wanazolipwa watumishi wa umma litafutwa kwani wanaopokea hizo posho ndio wenye mapato makubwa na walistaili kulipa kodi kubwa zaidi ya wenye mapato madogo kama walimu, manesi n.k.
Hata hivyo sina uhakika kama CCM inafuata sera za Democratic au Republican; kama ni Republican nadhani CCM hawatakuwa tayari kuiga sera za kuboresha maisha ya walala hoi badala yake itaendelea tuu kukumbatia maslahi ya wale wenye kipato kikubwa huku wakikimbiza na mama lishe, wauza mboga, biashara za kifamilia n.k
Naamini kwa kuwa Raisi wetu Jakaya Kikwete yuko huko Marekani, hotuba ya Obama itamfanya aelewe kile CHADEMA walichokuwa wanatetea katika Bunge la Bajeti kuwa wabunge walipie kodi mapato yao yote na baadhi ya posho wanazolipwa watumishi wa umma (hususani viongozi) ziondolewe. Naamini vile vile kwa kuwa Tanzania tu watu wa kuiga, hata lile wazo la kusamehe kodi Posho wanazolipwa watumishi wa umma litafutwa kwani wanaopokea hizo posho ndio wenye mapato makubwa na walistaili kulipa kodi kubwa zaidi ya wenye mapato madogo kama walimu, manesi n.k.
Hata hivyo sina uhakika kama CCM inafuata sera za Democratic au Republican; kama ni Republican nadhani CCM hawatakuwa tayari kuiga sera za kuboresha maisha ya walala hoi badala yake itaendelea tuu kukumbatia maslahi ya wale wenye kipato kikubwa huku wakikimbiza na mama lishe, wauza mboga, biashara za kifamilia n.k